picha

Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI

DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?

Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.

Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)

 

Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-

 

 

1.Kupatwa na homa.

2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu

3.Maumivu ya misuli

4.Kuota upele

5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.

6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.

7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri

8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo

9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.

10.Kutokwa na Jasho la usiku

11.Kuharisha

 

Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.

 

 

Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.

Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.

 

 

Baada ya maambukizi ya Awali

Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:

 

 

1.Homa

2.Uchovu

3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU

4.Kuhara

5.Kupungua uzito

6.Kikohozi

7.Kupumua kwa pumzi

 

 

Kuendelea kwa UKIMWI

Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-11-03 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2823

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 ai web app    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Namna ya kuepuka Ugonjwa wa ngiri.

Posti hii inahusu zaidi namna au njia za kuepuka na Ugonjwa huu wa ngiri ambao uleta madhara kwa watoto, vijana na watu wazima, kwa hiyo ili tuweze janga hili ni lazima tufanye yafuatayo.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Swali langu ni hivi ,napata maumivu kwa mbali kwenye njia za mkojo pia napoteza ham na uwezo wa kushiriki tendo la ndoa kadiri siku zinavoenda je,hizi ni dalili za tezi dume?

Hivi umeshawahikujiuliza kuhusu tezi dume. Wacha nikujuze kitu kimoja, ni kuwa tezi dume huwapata watu kuanziamiaka 40 na kuendelea. Na ifahamike kuwa tezi dume sio busha ama ngiri maji. Pia itambulikekuwa rozi dumehutibika.

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya matiti na chuchu

Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo ya tumbo

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya mapafu

Saratani ya Mapafu ni aina ya Kansa inayoanzia kwenye mapafu. Mapafu yako ni viungo viwili vya sponji kwenye kifua chako ambavyo huchukua oksijeni unapovuta na kutoa kaboni dioksidi unapotoa nje.

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
Kuona damu kwenye mkojo

Kuona damu kwenye mkojo kunaweza kusababisha wasiwasi. Ingawa katika hali nyingi kuna sababu zisizofaa, Damu kwenye mkojo (hematuria) pia inaweza kuonyesha ugonjwa mbaya.

Soma Zaidi...