picha

Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI

DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?

Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.

Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)

 

Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-

 

 

1.Kupatwa na homa.

2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu

3.Maumivu ya misuli

4.Kuota upele

5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.

6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.

7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri

8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo

9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.

10.Kutokwa na Jasho la usiku

11.Kuharisha

 

Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.

 

 

Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.

Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.

 

 

Baada ya maambukizi ya Awali

Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:

 

 

1.Homa

2.Uchovu

3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU

4.Kuhara

5.Kupungua uzito

6.Kikohozi

7.Kupumua kwa pumzi

 

 

Kuendelea kwa UKIMWI

Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3129

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰3 web hosting     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Hofu ya kijamii (Social Anxiety): Dalili na tiba.

wazo la kuzungumza mbele ya hadhara au hata kwenye mikutano midogo linakupa jasho na mapigo ya moyo kwenda mbio? Hii inaweza kuwa ni Social Anxiety Disorderβ€”hofu kubwa ya kutathminiwa au kuhukumiwa na wengine. Makala haya yanakusaidia kutambua kama una hali hii na mbinu za kitaalamu za kuishinda ili uweze kuishi maisha ya kujiamini

Soma Zaidi...
Namna madonda koo yanavyotokea

Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.

Soma Zaidi...
Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa vericose veini

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa vericose veini

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo ya tumbo

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.

Soma Zaidi...
MATIBABU YA FANGASI

Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi.

Soma Zaidi...