Aina 12 za swala za sunnah na idadi ya rakaa zake wakati wa usiku na mchana

Aina za Swala za Sunnah.

Aina 12 za swala za sunnah na idadi ya rakaa zake wakati wa usiku na mchana

Aina 12 za swala za sunnah na idadi ya rakaa zake wakati wa usiku na mchana

Aina za Swala za Sunnah.
Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.
Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:



i.Swala ya Maamkizi ya Msikiti.
- Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.



ii.Swala za Qabiliyyah na Ba'adiyyah.
- Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba'adiyyah) ya swala za Faradh.
- Ziko aina mbili; 'Mu'akkadah' (zilizokokotezwa) na 'Ghairu Mu'akkadah' (Hazikukokotezwa).



iii.Swala ya Witiri.
- Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.
- Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.



iv.Swala ya Tahajjud (Qiyaamul-layl).
- Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11.
- Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur'an.
Rejea Qur'an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).



v.Swala ya Tarawehe (Qiyaamu Ramadhan).
- Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur'an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.
- Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11.



vi.Swala ya Idil-Fitr na Al-Udhuhaa.
- Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.
- Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.



vii.Swalatudh-Dhuhaa.
- Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.
- Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.



viii.Swalatul-Istikharah.
- Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.



ix.Swala ya Kukidhi Haja.
- Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.



x.Swalatut ' Tawbah.
- Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.
Rejea Qur'an (3:135-136).



xi.Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi.
- Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke.



xii.Swala ya Kuomba (Swalatul-Istisqaa).
- Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.
- Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2232


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Hadithi Ya 30: Allaah Amefaridhisha Mambo Ya Dini Tusiyapuuze
Soma Zaidi...

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi
Soma Zaidi...

NASAHA ZANGU NNE KWAKO KUHUSU QURAN, MAUTI, DUA NA MENGINE
Soma Zaidi...

umuhimu wa swala katika uislamu
Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Maudhui ya Qur-an na Mvuto wa Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango
Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUNUS
Soma Zaidi...

quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...

Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu Soma Zaidi...