Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na ubinaadamu wao.
Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
- Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na kwingineko Duniani.
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na
ubinaadamu wao.
- Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
au kwa matumizi mengineyo pia.
- Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
wakubwa zao.
- Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
zao katika kutimiza matashi yao.
- Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini
waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.
- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama
kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.
- Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki,
mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.
- Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.
- Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno,
kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo.
- Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
kwa bwana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 ai web app 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani
(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.
Soma Zaidi...