Dondoo za afya 21-40
Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya
? DONDOO NAMBA 21 - 40
Basi tambua haya;-
21.Maji hutumika kupooza ingini. Halikadhalika hutumika kupooza mwili pia.
22.Upungufu wa vitamini A hupelekea kukauka kwa ngozi, uoni hafifu na kuathirika kwa koo na ngozi
23.Upungufu wa vitamin B1 hupelekea kukosa hamu ya kula, udhaifu wa miguu, kupungua kwa hisia kwenye neva kudhoofu kwa misuli na kuathirika kwa akili.
24.Upungufu wa Vitamin B2 hupelekea kupata ugonjwa wa pellagra yaani vidonda vya mdomo na ulimi, ukuaji hafifu, kupasuka kwa nbgozi hasa sehemu za sikio na pua.
25.Upungufu wa Vitamin B12 husababisha matatizo katika uzalishaji wa seli hai nyekundu za damu. Na kusababisha aina ya ugonjwa wa anaemia
26.Upungufu wa vitamini C husababisha kutoka damu kwenye mafinzi, kuchelewa kupona kwa majeraha, maumivu ya viungo na kudhoofu kwa mishipa ya damu hasa kwenye ngozi.
27.Upungufu wa vitamin D husababisha kuleta matege.
28.Upungufu wa vitamin k husababisha kuchelewa kuganda kwa damu kwenye jeraha
29.Upungufu wa madini ya Iodine hupelekea kupata ugonjwa wa Goitre yaani kukuwa kwa tezi ya thyroid.
30.Upungufu wa madini ya potasium hupelekea udhaifu wa misuli kutokuweza kukunja kwa ufasaha.
31.Upungufu wa madini ya magnesium hupelekea utengenezwaji hafifu wa meno na mifupa na misuli hishindwa kukunja kwa ufasaha.
32.Upungufu wa madini ya sodium husababisha kukaza kwa misuli.
33.Upungufu wa madini ya clorine hupelekea mwili kushindwa kuzalisha asidi ya hydrocloric. Asidi hii husaidia katika mmeng’enyo wa chakula mwilini.
34.Upungufu wa madini ya phosphorous hupelekea udhaifu wa meno na mifupa na mwili kwa ujumla.
35.Madini ya calcium yakipungua mwilini husababisha udhaifu wa meno na mifupa.
36.Katika mabo yanayopunguza kinga ya mwili yaani uwezo wa mwili kupambana na maradhi ni misongo ya mawazo, utaratibu mmbovu wa lishe au kutopata lishe bora na mlo kamili, mazingira na madawa.
37.Upigapo chafya ziba mdomo kwa kitu kilicho safi.
38.Kwa mama anayenyonyesha ahakikishe ziwa lake halina kemikali yaani losheni au mafuta ili mtoto asije nyonya kemikali zile.
39.Ugonjwa wa mnjano yaani hepatitis B ni katika magonjwa yanayouwa watu wengi duniani. Karibia watu 620,000 hufa kila mwaka, na karibia watu milioni 350 wameathirika na ugonjwa huu. (WHO)
40.Ugonjwa wa manjano husababishwa na vitusi viitwavyo Hepatitia b (HBV) ambao hawa hushambulia ini na kusababishwa uvimbe. Uvimbe huu unapelekea kupata kansa ya ini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Faida za kiafya za kufunga
Simulizi yetu ya leo tutajifunza kuhusu faida za kiafya za kufunga kwa mtazamo wa kitabibu, kama anavyoeleza daktari. Tutaangalia namna kufunga kunavyoathiri na kusaidia viungo na mifumo mbalimbali ya mwili. Somo letu la leo litahusu… faida za kiafya za kufunga katika figo, moyo, ini, mfumo wa kinga, kisukari, presha ya damu na mmeng’enyo wa chakula.
Soma Zaidi...Ukoma (Leprosy): Je, unagundulika vipi leo?
Ukoma, unaojulikana kitaalamu kama Hansen’s disease, ni ugonjwa wa muda mrefu unaosababishwa na bakteria Mycobacterium leprae. Ugonjwa huu huathiri ngozi, neva za pembeni (peripheral nerves), utando wa juu wa njia ya upumuaji, na macho. Licha ya dhana potofu za kale, Ukoma leo unagundulika kwa urahisi na kutibika kikamilifu kwa dawa za antibayotiki, na mgonjwa anapoanza tiba, hawezi tena kuambukiza wengine.
Soma Zaidi...