image

Dua za kuomba wakati unapokuwa na hasira ama ukiwa umekasirika

Post hii itakueleza ni dua gani unatakiwa uzisome wakati unapokiwa na hasira ama pale unapokasirika.


DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA.
Hashira ni katika matendo ambayo shetani anayapenda sana yatokee kwa mwadadamu. Kwa sababu ya hasira maovu mengine huenda yakatokea kama matusi, kupigana, vifo na mengineyo mengi. Uislamu kama dini iliyokamilika imetowa muongozo mzima juu ya namna ya kukabiliana na hali ya hasira pindi inapotokea. Katika makala hii tunakwenda kuona njia za kukabiliana na hali ya hasira pindi inapotokea.

Njia za kuzuia Hasira
1.Kumlani shetani kwa kusema ‘’a’udhubillahi minashaytwanir- rajiim”: Katika hadithi iliyosimuliwa na Sulayman Ibn Sard amesema: “nilikuwa nimekaa na Mtume (s.a.w), na kulikuwa na watu wawili wanagombana. Mmoja uso umekuwa mwekundu kwa hasira na mishipa ya shingo imemsimama. Mtume (s.a.s) akasema, ‘ninayajuwa maneno ambayo kama atayasema, hasira zote alizo nazo zitaondoka. Kama atasema “a’udhubillahi minash-shaytwaanir- rajiim” hasira zake zote zitaondoka. (amepokea BUkhari)

2.kubakia kimya
Kubakia kimya wakati wa kuwa na hasira ni jambo la busara, kwani ukiendelea kubakia kimya ndio hasira zitatulia. Amesema Mtume (s.a.s) “kama mmoja wenu atapatwa na hasira na abakie kimya (Amepokea Ahmad).

3.Kutokutembea:
Hasira zikitokea kama umesimama usiendelee kwenda au kusimama kwanza kaa chini. Amesema Mtume (s.a.s) “kama mmoja wenu amepatwa na hasira na akiwa amesimama basi na akae chini, hasira zake zitaondoka, na kama hazitaondoka basi na alale” (Amepokea Ahmad).

Kwa ufupi zipo njia nyingi ila hizi tatu ndio nitaishia kwenye makala hii. Tufahamu kuwa kumlani shetani ni njia ya kumkimbiza kwani yeye ndie anayesababisha hasira. Ni vyema ukachukuwa Udhu unapokuwa na hasira na kumlani shetani kwa wingi. Kubakia kimya wakati wa hasira, kukaa kama umesiamama ama kulala ni katika njia za kuondoa hasira

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1899


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA
NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA. Soma Zaidi...

AINA ZA HADITHI
Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi. Soma Zaidi...

Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo
Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi. Soma Zaidi...

KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA
عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ عُقْبَةَ بْنِ عَمْرٍو الْأَنْصَارِيِّ الْبَدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عل?... Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa salamu katika uislamu
MAkala hii itakwenda kukufundisha jinsi ya kutoa salamu kwenye uislamu Soma Zaidi...

Dua sehemu 03
Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 21: Sema Namuamini Allah Kisha Kuwa Mwenye Msimamo
Soma Zaidi...

Wajbu wa wazazi kwa watoto wao
Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao. Soma Zaidi...

DUA 61 - 84
61. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 31: Upe Ulimwengu Kisogo Allaah Atakupenda
Soma Zaidi...

Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.
Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume Soma Zaidi...

Nafasi ya Sunnah (suna) katika Uislamu.
Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu Soma Zaidi...