Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin.
1. Ni aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, kwa sababu yenyewe udili na bakteria ambao ushambulia mwili na kusababisha madhara ya mda mrefu na kwa hiyo ikiingia mwili inawezekana kukaa kwa masaa Ili kuweza kudili na bakteria ambao wameleta madhara ya mda mrefu.
2. Kwa kawaida dawa hii utumika kutibu maambukizi mbalimbali ya bakteria ambayo ujitokeza kwenye mwili wa binadamu na pia utumika kwa watu wazima na watoto kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia kwenye kundi hili Kuna dawa nyingine ambayo Kwa kitaamu huiitwa fortified procaine penicillin nayo ufanya kazi kama procaine benzyl penicillin.
3. Dawa hii kwa kawaida huwa kwenye mfumo wa unga na huwa kwenye ki chupa Fulani hivi na pia uchanganywa na maji maalumu kwa ajili ya dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa sterile water,na uchanganywa kwa pamoja , yaani dawa na maji na pia utikiswa kumhakikishia kuwa unga umachanganyika kabisa na maji .
4. Dose kwa mgonjwa utegemea mtoto na mtu mzima,uzito na umri wa mtu,na pia dawa hii inaweza kutolewa kwa kupigwa sindano kwenye mapaja au Tako, na kwa wakati mwingine uweza kupitia kwenye damu, kwa hiyo mchanganyiko wa kupitia kwenye paja au Tako ni tofauti na ule mchanganyiko wa kupitia kwenye mishipa ya damu.
5. Dawa hii pia utumiwa na watu mbalimbali ila kwa wale wote wenye aleji na dawa ya penicillin hawapaswi kutumia dawa hii, kwa hiyo watatumia dawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya.
6. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo baada ya kuitumia, maudhi yenyewe ni kama maumivu kwenye jointi, unaweza kupata upungufu wa damu ukiitumia kwa mda mrefu, kwa hiyo wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari,pia dawa hazipaswi kutumiwa kiholela Bali ni kwa ushauri wa wataalamu wa afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.
Soma Zaidi...Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.
Soma Zaidi...Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.
Soma Zaidi...