Fahamu aina ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu
Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin.
Fahamu kuhusu dawa ya procaine benzyl penicillin.
1. Ni aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, kwa sababu yenyewe udili na bakteria ambao ushambulia mwili na kusababisha madhara ya mda mrefu na kwa hiyo ikiingia mwili inawezekana kukaa kwa masaa Ili kuweza kudili na bakteria ambao wameleta madhara ya mda mrefu.
2. Kwa kawaida dawa hii utumika kutibu maambukizi mbalimbali ya bakteria ambayo ujitokeza kwenye mwili wa binadamu na pia utumika kwa watu wazima na watoto kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia kwenye kundi hili Kuna dawa nyingine ambayo Kwa kitaamu huiitwa fortified procaine penicillin nayo ufanya kazi kama procaine benzyl penicillin.
3. Dawa hii kwa kawaida huwa kwenye mfumo wa unga na huwa kwenye ki chupa Fulani hivi na pia uchanganywa na maji maalumu kwa ajili ya dawa ambayo Kwa kitaamu huiitwa sterile water,na uchanganywa kwa pamoja , yaani dawa na maji na pia utikiswa kumhakikishia kuwa unga umachanganyika kabisa na maji .
4. Dose kwa mgonjwa utegemea mtoto na mtu mzima,uzito na umri wa mtu,na pia dawa hii inaweza kutolewa kwa kupigwa sindano kwenye mapaja au Tako, na kwa wakati mwingine uweza kupitia kwenye damu, kwa hiyo mchanganyiko wa kupitia kwenye paja au Tako ni tofauti na ule mchanganyiko wa kupitia kwenye mishipa ya damu.
5. Dawa hii pia utumiwa na watu mbalimbali ila kwa wale wote wenye aleji na dawa ya penicillin hawapaswi kutumia dawa hii, kwa hiyo watatumia dawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya.
6. Pia dawa hii Ina maudhi madogo madogo baada ya kuitumia, maudhi yenyewe ni kama maumivu kwenye jointi, unaweza kupata upungufu wa damu ukiitumia kwa mda mrefu, kwa hiyo wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari,pia dawa hazipaswi kutumiwa kiholela Bali ni kwa ushauri wa wataalamu wa afya.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 web hosting 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Ni dawa gani hatari kwa mjamzito?
Ukiwa mjamzito uwe makini sana katika kuchagua matumizi ya dawa. Vinginevyobinawwza kuwa hatari. Hapa nitakujuza dawa ambazo ni hatari kutumia kwa ujauzito wako.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Nani anapaswa kutumia vidonge vya zamiconal.
Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi.
Soma Zaidi...Ijue dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya kutibu maumivu ya mgongo (back none pain) na kiuno
Fahamu dawa ya back bone pain kwa matibabu ya mgongo, ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza maumivu ya mgongo.
Soma Zaidi...