Fahamu dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine.
Dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba dawa hii ya carvedilo imo kwenye makundi ya dawa za matibabu ya magonjwa ya moyo ,dawa hii uhusika na kupunguza mapigo ya moyo kama yanakwenda mbio na matatizo mbalimbali yanayoendana na hali hiyo ,kwa upande wa matumizi dawa hii utegemea mgonjwa pia na utaalamu wa wahudumu wa afya.
2. Kwa kawaida dawa hii uwa kwenye mfumo wa vidonge na pia utumika kila siku hasa kwa watumiaji wenye tatizo la kudumu ila kwa wale ambao tatizo limetokea kwa mda au kwa sababu fulani dawa hizi zinawezwa kuacha kutumika hasa pale tatizo lilionekana kuisha .
3. Pia kama zilivyo dawa nyingine na dawa hii ya carvedilo ina maudhui madogo madogo kama vile kuwepo kwa kizungu Zungu hasa kwa wanaoanza kutumia dawa, uchofu wa mara kwa mara ,presha kushuka, kichefuchefu na kutapika, uzito kuongezeka, pia kwa walio wachache wanaweza kupata shida ya kushindwa kupumua na pengine sukari kushuka, kwa hiyo ikitokea haya maudhui madogo madogo yakitokea kwa kiwango cha chini ni vizuri kuyavumilia na kisha baada ya mda mfupi.
5. Kwa upande wa maudhi madogo madogo yakiendelea na kusababisha madhara makubwa hasa upungufu wa sukari na kupumua vibaya ni vizuri kutoa taarifa kwa wataalamu wa afya ili waweze kubadilisha dawa na kumfanya mgonjwa aendelee vizuri.
6. Dawa hii inatumika kwa watu mbalimbali ila kwa wale wenye matatizo ya kushuka kwa sukari,na kupumua vibaya wanapaswa kuzitumia kwa uangalifu mkubwa au kwa upande wa wenye sukari ni vizuri kupima sukari kabla ya kutumia dawa.
7. Kwa hiyo dawa hizo zinapaswa kutumika kwa utaratibu na ushauri wa wataalamu wa afya na sio kutumia dawa hii kiholela.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa.
Soma Zaidi...Dawa ya vidonda vya tumbo
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital
Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.
Soma Zaidi...