Fahamu dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine.
Dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba dawa hii ya carvedilo imo kwenye makundi ya dawa za matibabu ya magonjwa ya moyo ,dawa hii uhusika na kupunguza mapigo ya moyo kama yanakwenda mbio na matatizo mbalimbali yanayoendana na hali hiyo ,kwa upande wa matumizi dawa hii utegemea mgonjwa pia na utaalamu wa wahudumu wa afya.
2. Kwa kawaida dawa hii uwa kwenye mfumo wa vidonge na pia utumika kila siku hasa kwa watumiaji wenye tatizo la kudumu ila kwa wale ambao tatizo limetokea kwa mda au kwa sababu fulani dawa hizi zinawezwa kuacha kutumika hasa pale tatizo lilionekana kuisha .
3. Pia kama zilivyo dawa nyingine na dawa hii ya carvedilo ina maudhui madogo madogo kama vile kuwepo kwa kizungu Zungu hasa kwa wanaoanza kutumia dawa, uchofu wa mara kwa mara ,presha kushuka, kichefuchefu na kutapika, uzito kuongezeka, pia kwa walio wachache wanaweza kupata shida ya kushindwa kupumua na pengine sukari kushuka, kwa hiyo ikitokea haya maudhui madogo madogo yakitokea kwa kiwango cha chini ni vizuri kuyavumilia na kisha baada ya mda mfupi.
5. Kwa upande wa maudhi madogo madogo yakiendelea na kusababisha madhara makubwa hasa upungufu wa sukari na kupumua vibaya ni vizuri kutoa taarifa kwa wataalamu wa afya ili waweze kubadilisha dawa na kumfanya mgonjwa aendelee vizuri.
6. Dawa hii inatumika kwa watu mbalimbali ila kwa wale wenye matatizo ya kushuka kwa sukari,na kupumua vibaya wanapaswa kuzitumia kwa uangalifu mkubwa au kwa upande wa wenye sukari ni vizuri kupima sukari kabla ya kutumia dawa.
7. Kwa hiyo dawa hizo zinapaswa kutumika kwa utaratibu na ushauri wa wataalamu wa afya na sio kutumia dawa hii kiholela.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu dawa ya marcolides dawa ya kuuwa bakteria, kwenye mfumo wa hewa
Post hii inahusu zaidi dawa ya macrolide ni mojawapo ya dawa ya kutibu au kupambana na bakteria na upambana na bakteria wafuatao streptococcus pyogenes, staphylococcus aureus na haihusiki na haemophilia influenza ambao usababisha maambukizi kwenye mfumo w
Soma Zaidi...Kazi ya Dawa ya salbutamol
Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin
Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.
Soma Zaidi...Fahamu Dawa itwayo Diazepam
Diazepam ni nini? Diazepam ni Dawa ambayo Huathiri kemikali kwenye ubongo ambazo zinaweza kukosa uwiano na kusababisha wasiwasi. Diazepam hutumiwa kutibu matatizo ya wasiwasi, dalili za kuacha pombe, au misuli. Diazepam wakati mwingine hutumiwa pamoja n
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha
Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Soma Zaidi...