picha

Fahamu dawa za kisukari

Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka.

Fahamu dawa za kisukari.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kuna aina mbili za kisukari, kuna sukari daraja la kwanza na sukari daraja la pili, kwa kawaida mgonjwa wa sukari daraja la kwanza hana insulii kabisa na sukari daraja la pili mgonjwa anakuwa na insulini ila kongosho likizalisha insulini seli haziwezi kukubali ile insulini, kabla ya kuendelea tunapaswa kufahamu kabisa maana ya insulini, ni kichocheo ambacho usaidia kurekebisha sukari mwilini, kama sukari ni nyingi kichocheo hicho uweka sukari kwenye usawa na nyingine upelekwe sehemu kutunzwa ili ije kutumika baadae pale sukari ikipunguaa mwilini.

 

2.Dawa ambayo utumika kwenye matibabu ya sukari ni insulini hasa utumika kwenye sukari daraja la kwanza, kwa mgonjwa wa kisukari insulini utolewe kabla ya kula au baada ya kula ili kuweza kuweka sukari sawa mwilini kwa sababu kongosho linakuwa halizalishi insulin,baada ya kutumika ufanya kazi kuanzia dakika kumi na tano inaenda mpaka thelathini hapo ndipo inafikia kilele na ufanya kazi mpaka kwenye dakika tisini hivi na uisha mwilini kuanzia masaa matatu mpaka matano kwa sababu wagonjwa huwa tofauti na hali zao pia huwa tofauti kwa hiyo maagizo ya watanzania wa afya ni lazima.

 

3. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kila mtu huwa na insulini alivyozaliwa nayo kwa hiyo tunapokula vyakula vya wanga na kwa kiasi kikubwa vina kiwango kikubwa cha sukari ambayo usaidia kuleta nguvu mwilini, kwa hiyo bila vyakula vya wanga nguvu hiyo hatutaweza kuipata kwa hiyo kwa  hiyo  sukari inayoingia mwilini siyo yote inahitajika kwa hiyo insulini uweka sukari sawa na ile ambayo haiitajiki uwekwa kwenye sehemu yake ikiwa kama sukari ukiisha hiyo akiba iliyowekwa uweza kutumika tena,

 

4.kama insulini tuliyozaliwq nayo inafanya kazi na insulini ya bandia ufanya kazi vile vile hasa kwa wagonjwa wenye shida ya sukari hasa sukari daraja la kwanza ambalo mtu anazaliwq bila insulini kwa hiyo maisha yake yote anakuwa anatumia insulini bandia na maisha yanaenda kawaida .

 

5. Pia kuna matokeo ambayo yanaweza kutokea katika matumizi ya insulini katika kuweka sukari sawa na matokeo hayo ni kama sukari kubwa chini kabisa,kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba kama sukari ikiwa nyingi mwilini na insulini ikatumika badala ya kushusha ikawa kawaida inawezekana ikashuka kabisa,na pengine sukari inawezekana kusababisha mgonjwa kuongeza uzito, hali hii utokea kwa sababu ya kutokuwepo na insulini ya kurekebisha sukari, kwa hiyo sukari inakuwa nyingi kwenye damu hali inayosababisha maji yote kukusanywa kutoka sehemu mbalimbali za mwili ili kuja kuyeyusha sukari kwenye damu, kwa hiyo kwa sababu ya kukosa maji kwenye sehemu mbalimbali za mwili mtu huanza kuhisi kiu kwa hiyo anakula sana na kunywa sana hali inayosababisha mgonjwa kuongezeka uzito.

 

6. Kupata vidonda kwenye mwili au vidonda kuchelewa kupona.

Kwa kawaida tunafahamu kwamba kwenye mwili wa mgonjwa wa kisukari mda mwingi sukari inakuwa nyingi mwilini hali inayoifanya hata mwili wenyewe kubadilika kwa sababu ikitokea mgonjwa anayetumia insulini akapata kidonda kupona kwake sio rahisi kwa sababu ni kama mwili mzima umejaa sukari kwa hiyo na bakteria wanapenda sana sehemu yenye sukari hali inayosababisha vifo da kutopona haraka.kwq hiyo wagonjwa wa sukari wanapaswa kuwa makini ili wasipatwe na vidonda kwa sababu huwa wanapata shida sana.

 

7. Matokeo mengine ya kutumia insulini ni kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu ambayo mgonjwa anapitishiwa sindano mara kwa mara, kwa sababu dawa hizi ni za kila siku kwa hiyo mgonjwa anadungwa sindano mara kwa mara na pia kwenye sehemu hiyo makovu yanakuwepo mengi.

 

8. Pia dawa hizi haipaswi kutumiwa kiholela endapo mtu amefunguliwa na sukari kwa sababu kuna mda wa kutumia kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/31/Saturday - 08:32:46 pm Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1413

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Madhara ya Tiba mionzi

Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo.

Soma Zaidi...
Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.

Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.

Soma Zaidi...
Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini

Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.

Soma Zaidi...
Tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Dawa ya UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya UTI

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya parental Artusnate dawa ya kutibu malaria sugu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye.

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi uumeni

kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones

Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin.

Soma Zaidi...