picha

Fahamu dawa za kisukari

Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka.

Fahamu dawa za kisukari.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kuna aina mbili za kisukari, kuna sukari daraja la kwanza na sukari daraja la pili, kwa kawaida mgonjwa wa sukari daraja la kwanza hana insulii kabisa na sukari daraja la pili mgonjwa anakuwa na insulini ila kongosho likizalisha insulini seli haziwezi kukubali ile insulini, kabla ya kuendelea tunapaswa kufahamu kabisa maana ya insulini, ni kichocheo ambacho usaidia kurekebisha sukari mwilini, kama sukari ni nyingi kichocheo hicho uweka sukari kwenye usawa na nyingine upelekwe sehemu kutunzwa ili ije kutumika baadae pale sukari ikipunguaa mwilini.

 

2.Dawa ambayo utumika kwenye matibabu ya sukari ni insulini hasa utumika kwenye sukari daraja la kwanza, kwa mgonjwa wa kisukari insulini utolewe kabla ya kula au baada ya kula ili kuweza kuweka sukari sawa mwilini kwa sababu kongosho linakuwa halizalishi insulin,baada ya kutumika ufanya kazi kuanzia dakika kumi na tano inaenda mpaka thelathini hapo ndipo inafikia kilele na ufanya kazi mpaka kwenye dakika tisini hivi na uisha mwilini kuanzia masaa matatu mpaka matano kwa sababu wagonjwa huwa tofauti na hali zao pia huwa tofauti kwa hiyo maagizo ya watanzania wa afya ni lazima.

 

3. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kila mtu huwa na insulini alivyozaliwa nayo kwa hiyo tunapokula vyakula vya wanga na kwa kiasi kikubwa vina kiwango kikubwa cha sukari ambayo usaidia kuleta nguvu mwilini, kwa hiyo bila vyakula vya wanga nguvu hiyo hatutaweza kuipata kwa hiyo kwa  hiyo  sukari inayoingia mwilini siyo yote inahitajika kwa hiyo insulini uweka sukari sawa na ile ambayo haiitajiki uwekwa kwenye sehemu yake ikiwa kama sukari ukiisha hiyo akiba iliyowekwa uweza kutumika tena,

 

4.kama insulini tuliyozaliwq nayo inafanya kazi na insulini ya bandia ufanya kazi vile vile hasa kwa wagonjwa wenye shida ya sukari hasa sukari daraja la kwanza ambalo mtu anazaliwq bila insulini kwa hiyo maisha yake yote anakuwa anatumia insulini bandia na maisha yanaenda kawaida .

 

5. Pia kuna matokeo ambayo yanaweza kutokea katika matumizi ya insulini katika kuweka sukari sawa na matokeo hayo ni kama sukari kubwa chini kabisa,kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba kama sukari ikiwa nyingi mwilini na insulini ikatumika badala ya kushusha ikawa kawaida inawezekana ikashuka kabisa,na pengine sukari inawezekana kusababisha mgonjwa kuongeza uzito, hali hii utokea kwa sababu ya kutokuwepo na insulini ya kurekebisha sukari, kwa hiyo sukari inakuwa nyingi kwenye damu hali inayosababisha maji yote kukusanywa kutoka sehemu mbalimbali za mwili ili kuja kuyeyusha sukari kwenye damu, kwa hiyo kwa sababu ya kukosa maji kwenye sehemu mbalimbali za mwili mtu huanza kuhisi kiu kwa hiyo anakula sana na kunywa sana hali inayosababisha mgonjwa kuongezeka uzito.

 

6. Kupata vidonda kwenye mwili au vidonda kuchelewa kupona.

Kwa kawaida tunafahamu kwamba kwenye mwili wa mgonjwa wa kisukari mda mwingi sukari inakuwa nyingi mwilini hali inayoifanya hata mwili wenyewe kubadilika kwa sababu ikitokea mgonjwa anayetumia insulini akapata kidonda kupona kwake sio rahisi kwa sababu ni kama mwili mzima umejaa sukari kwa hiyo na bakteria wanapenda sana sehemu yenye sukari hali inayosababisha vifo da kutopona haraka.kwq hiyo wagonjwa wa sukari wanapaswa kuwa makini ili wasipatwe na vidonda kwa sababu huwa wanapata shida sana.

 

7. Matokeo mengine ya kutumia insulini ni kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu ambayo mgonjwa anapitishiwa sindano mara kwa mara, kwa sababu dawa hizi ni za kila siku kwa hiyo mgonjwa anadungwa sindano mara kwa mara na pia kwenye sehemu hiyo makovu yanakuwepo mengi.

 

8. Pia dawa hizi haipaswi kutumiwa kiholela endapo mtu amefunguliwa na sukari kwa sababu kuna mda wa kutumia kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1624

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Dawa ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za minyoo

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia tiba ya jino.

Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Ijue dawa ya kutibu ugonjwa wa ukoma

Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu ukoma,na dawa hiyo ni dawa ya Dapsoni, hii dawa usaidia kuzuia nerve zisiendelee kupoteza kazi yake pia na ngozi iendelee kuwa kawaida

Soma Zaidi...
Kazi ya Dawa ya salbutamol

Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.

Soma Zaidi...
Dawa inaitwa koflame ukitumia inashida kwa mama mjamzito? Maumivu ya mgongo na nyonga zinasumbua

Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto

Soma Zaidi...