picha

Fahamu dawa za kisukari

Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka.

Fahamu dawa za kisukari.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kuna aina mbili za kisukari, kuna sukari daraja la kwanza na sukari daraja la pili, kwa kawaida mgonjwa wa sukari daraja la kwanza hana insulii kabisa na sukari daraja la pili mgonjwa anakuwa na insulini ila kongosho likizalisha insulini seli haziwezi kukubali ile insulini, kabla ya kuendelea tunapaswa kufahamu kabisa maana ya insulini, ni kichocheo ambacho usaidia kurekebisha sukari mwilini, kama sukari ni nyingi kichocheo hicho uweka sukari kwenye usawa na nyingine upelekwe sehemu kutunzwa ili ije kutumika baadae pale sukari ikipunguaa mwilini.

 

2.Dawa ambayo utumika kwenye matibabu ya sukari ni insulini hasa utumika kwenye sukari daraja la kwanza, kwa mgonjwa wa kisukari insulini utolewe kabla ya kula au baada ya kula ili kuweza kuweka sukari sawa mwilini kwa sababu kongosho linakuwa halizalishi insulin,baada ya kutumika ufanya kazi kuanzia dakika kumi na tano inaenda mpaka thelathini hapo ndipo inafikia kilele na ufanya kazi mpaka kwenye dakika tisini hivi na uisha mwilini kuanzia masaa matatu mpaka matano kwa sababu wagonjwa huwa tofauti na hali zao pia huwa tofauti kwa hiyo maagizo ya watanzania wa afya ni lazima.

 

3. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba kila mtu huwa na insulini alivyozaliwa nayo kwa hiyo tunapokula vyakula vya wanga na kwa kiasi kikubwa vina kiwango kikubwa cha sukari ambayo usaidia kuleta nguvu mwilini, kwa hiyo bila vyakula vya wanga nguvu hiyo hatutaweza kuipata kwa hiyo kwa  hiyo  sukari inayoingia mwilini siyo yote inahitajika kwa hiyo insulini uweka sukari sawa na ile ambayo haiitajiki uwekwa kwenye sehemu yake ikiwa kama sukari ukiisha hiyo akiba iliyowekwa uweza kutumika tena,

 

4.kama insulini tuliyozaliwq nayo inafanya kazi na insulini ya bandia ufanya kazi vile vile hasa kwa wagonjwa wenye shida ya sukari hasa sukari daraja la kwanza ambalo mtu anazaliwq bila insulini kwa hiyo maisha yake yote anakuwa anatumia insulini bandia na maisha yanaenda kawaida .

 

5. Pia kuna matokeo ambayo yanaweza kutokea katika matumizi ya insulini katika kuweka sukari sawa na matokeo hayo ni kama sukari kubwa chini kabisa,kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba kama sukari ikiwa nyingi mwilini na insulini ikatumika badala ya kushusha ikawa kawaida inawezekana ikashuka kabisa,na pengine sukari inawezekana kusababisha mgonjwa kuongeza uzito, hali hii utokea kwa sababu ya kutokuwepo na insulini ya kurekebisha sukari, kwa hiyo sukari inakuwa nyingi kwenye damu hali inayosababisha maji yote kukusanywa kutoka sehemu mbalimbali za mwili ili kuja kuyeyusha sukari kwenye damu, kwa hiyo kwa sababu ya kukosa maji kwenye sehemu mbalimbali za mwili mtu huanza kuhisi kiu kwa hiyo anakula sana na kunywa sana hali inayosababisha mgonjwa kuongezeka uzito.

 

6. Kupata vidonda kwenye mwili au vidonda kuchelewa kupona.

Kwa kawaida tunafahamu kwamba kwenye mwili wa mgonjwa wa kisukari mda mwingi sukari inakuwa nyingi mwilini hali inayoifanya hata mwili wenyewe kubadilika kwa sababu ikitokea mgonjwa anayetumia insulini akapata kidonda kupona kwake sio rahisi kwa sababu ni kama mwili mzima umejaa sukari kwa hiyo na bakteria wanapenda sana sehemu yenye sukari hali inayosababisha vifo da kutopona haraka.kwq hiyo wagonjwa wa sukari wanapaswa kuwa makini ili wasipatwe na vidonda kwa sababu huwa wanapata shida sana.

 

7. Matokeo mengine ya kutumia insulini ni kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu ambayo mgonjwa anapitishiwa sindano mara kwa mara, kwa sababu dawa hizi ni za kila siku kwa hiyo mgonjwa anadungwa sindano mara kwa mara na pia kwenye sehemu hiyo makovu yanakuwepo mengi.

 

8. Pia dawa hizi haipaswi kutumiwa kiholela endapo mtu amefunguliwa na sukari kwa sababu kuna mda wa kutumia kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1664

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE

Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Theophylline katika kutibi mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya theophylline ni dawa inayofanya kazi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutibu mafua

Post hii inahusu dawa za kutibu mafua ambazo ni cough seppessants na nasal congestion ni dawa ambazo zimependekezwa kwa ajili ya kutibu mafua.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kutumia dawa za ARV

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .

Soma Zaidi...