picha

Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio

Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.

Fahamu dawa ya kutuliza aleji .

1. Kama tunavyofahamu kila mtu Kuna kitu ambacho huwa anakitumia na hakipatani na mwili wake kwa sababu Kuna wakati mwingine mwili huwa na viupele mtu anaanza kujikuna, au pengine kifua kinaanza kubana na mambo kama hayo kwa hiyo hali hiyo ikibadilika dawa ya hydrocortisone usaidia kuzuia aleji hasa zinazosababisha na dawa.

 

2. Dawa hiyo ufanya Kazi ya kutuliza aleji kwa kupambana na hali hiyo au kitu hicho na kukizuia kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu, kwa wagonjwa wa asthma mara nyingi huwa na aleji ambazo uwasababishia kifua kubana na pengine kupumua vibaya kwa kutumia dawa ya hydrocortisone hali uweza kuwa ya Kawaida .

 

3. Dawa hizi utolewa kwa kupulizia mgonjwa kwenye mfumo wa hewa na nyingine zinaweza kupitia kwenye mishipa na pia Kuna nyingine ambazo upewa kwa kumeza na pia zote ufanya kazi Ile Ile ya kusaidia mtu mwenye aleji.

 

4. Dawa hii ya hydrocortisone Ina milligrams tano ambazo utolewa kwa watoto na milligrams kumi kwa watu wazima na pia utolewa kila baada ya masaa sita mpaka dozi inaisha ,pia dozi yenyewe pamoja na kutegemea umri na pia utegemea uzito wa mtu mmoja na mwingine.

 

5. Pia dawa hii utolewa kwa watu mbalimbali ila Kuna watu ambao Wana aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia au kwa wale wenye presha ya kupanda wanapaswa kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya.

 

6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio na pia wakati mwingine kuishiwa nguvu na maumivu ya kichwa kwa hiyo tunapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2758

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

dawa ya kutibu infection kwenye kizazi nisaidie doctor

Je unasumbuliwa na maambukizi na mashambulizi ya virusi na bakteria kwenye sehemu za siri ama via vya uzazi?. Posti hii inakwenda kuupa ushauri.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutibu maumivu ya mgongo (back none pain) na kiuno

Fahamu dawa ya back bone pain kwa matibabu ya mgongo, ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza maumivu ya mgongo.

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
Dawa na matibabu ya presha ya kushuka

Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Ijue Dawa ya lignocaine

Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu

Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.

Soma Zaidi...