Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.
1. Kama tunavyofahamu kila mtu Kuna kitu ambacho huwa anakitumia na hakipatani na mwili wake kwa sababu Kuna wakati mwingine mwili huwa na viupele mtu anaanza kujikuna, au pengine kifua kinaanza kubana na mambo kama hayo kwa hiyo hali hiyo ikibadilika dawa ya hydrocortisone usaidia kuzuia aleji hasa zinazosababisha na dawa.
2. Dawa hiyo ufanya Kazi ya kutuliza aleji kwa kupambana na hali hiyo au kitu hicho na kukizuia kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu, kwa wagonjwa wa asthma mara nyingi huwa na aleji ambazo uwasababishia kifua kubana na pengine kupumua vibaya kwa kutumia dawa ya hydrocortisone hali uweza kuwa ya Kawaida .
3. Dawa hizi utolewa kwa kupulizia mgonjwa kwenye mfumo wa hewa na nyingine zinaweza kupitia kwenye mishipa na pia Kuna nyingine ambazo upewa kwa kumeza na pia zote ufanya kazi Ile Ile ya kusaidia mtu mwenye aleji.
4. Dawa hii ya hydrocortisone Ina milligrams tano ambazo utolewa kwa watoto na milligrams kumi kwa watu wazima na pia utolewa kila baada ya masaa sita mpaka dozi inaisha ,pia dozi yenyewe pamoja na kutegemea umri na pia utegemea uzito wa mtu mmoja na mwingine.
5. Pia dawa hii utolewa kwa watu mbalimbali ila Kuna watu ambao Wana aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia au kwa wale wenye presha ya kupanda wanapaswa kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya.
6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda mbio na pia wakati mwingine kuishiwa nguvu na maumivu ya kichwa kwa hiyo tunapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kundi la diuretics,ni kundi mojawapo kati ya makundi ya dawa zinazosaidia katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...