image

Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin

Fahamu dawa ya ampicillin.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba hii ni dawa ambayo usaidia kutibu maambukizi ya bakteria na pia ni dawa ambayo imo kwenye makundi ya penicillin kama tulivyoona hapo kwenye utangulizi na pia dawa hii inaweza kusaidia pia kupambana na bakteria ambao utoa asidi Ili kuweza kuzuia kazi ya dawa, kama dawa husika haipo ampicillin inaweza kutumika.

 

2. Kwa kawaida ampicillin usaidia katika matibabu ya maambukizi ya bakteria kwenye Koo,sikio,mkojo na pia usaidia katika matibabu ya nimonia, dawa hii huwa na container lake kila container Ina milligrams mia mbili hamsini na na nyingine huwa na miigram mia tano na pia milligrams utolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia dawa hii utolewa kila baada ya masaa sita , kabla ya kutumia dawa hii ni vizuri kutumiwa dakika thelathini kabla ya kula chakula.

 

3. Dawa pia IPO kwenye mfumo wa unga au poda na huwa na maji maalumu yametengwa kwa ajili ya kuchanganya poda hiyo na maji, maji hayo kwa kitaamu huiitwa water for injection, kwa hiyo dawa hiyo uchanganywa na maji na utikiswa na kuhakikisha kwamba poda haionekani tena na pia mgonjwa uweza kupewa dawa hiyo, kwa upande wa dozi utegemea umri na uzito wa mgonjwa. Pia dawa hiyo inawezekana kutolewa kwenye paja au Tako na pia kwenye mishipa ya damu.

 

Tunapaswa kufahamu kwamba mchanganyiko wa dawa inayopitia kwenye damu na kwenye paja au Tako ni tofauti kwa sababu ya kwenye mishipa inaenda Moja kwa moja kwenye damu kwa hiyo tunaongeza maji zaidi ya Ile inayopitia kwenye nyama ( Tako na paja).

 

4. Kwa wakati mwingine kuna syrup hizi ni kwa upande hasa wa watoto, mchanganyiko  ni kutumia milligrams mia ishilini na tano kwenye mills tano na pia mtoto anapewa, mara nyingi hizi dawa zinakuja zimechanganywa Moja kwa moja na chupa  Huwa na maagizo namna ya kutumia, kwa hiyo wazazi wa mtoto uweza kupewa maagizo na jinsi ya kumpatia mtoto dawa hiyo.

 

5. Dawa hii ya ampicillin na yenyewe Ina tabia kama dawa zote au makundi ya penicillin kwa hiyo kila mtu anaweza kutumia dawa hii ila kwa wale ambao Wana aleji na ampicillin hawapaswi kutumia dawa hii na pia wale wenye aleji ya penicillin hawapaswi kutumia kwa sababu dawa hii imo miongoni mwa makundi ya penicillin na pia kwa wale wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au waitumie kwenye uangalizi maalumu Ili wasije kuleta tatizo kubwa zaidi kwa sababu dawa hii Ina tabia ya kupunguza damu hasa kwa watumiaji wa mara kwa mara.

 

6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kujitokeza wakati wa kuitumia maudhi hayo ni pamoja na maumivu kwenye joint, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo , kizunguzungu na upungu wa damu au kama Kuna mtu ana kidonda au sehemu inayotoa damu anaweza kuendelea kutoa damu kwa mda mrefu wakati akiwa anatumia dawa hii. Kwa hiyo haya maudhi madogo madogo yakitokea ni kawaida wakati wa kutumia dawa hii ila yakiongezeka na kuleta madhara zaidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kubadilishiwaa dawa.

 

7. Pia ni vizuri kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya sio kutumia dawa hii kiholela kwa sababu matokeo yake yanaweza kuwa mabaya hasa kwa watu wenye damu kidogo wakitumia dawa hii wakiwa nyumbani wanaweza kuleta tatizo juu ya tatizo na pia kwa wale wenye sickle cell yaani wenye matatizo ya kuishiwa damu wanapaswa kuitumia dawa hii wakiwa kwenye uangalizi maalumu au wapime wingi wa damu kabla ya kutumia ai tatizo kama litakuwa kubwa zaidi na kuleta madhara ni Bora wabadilidhiwe na kupewa dawa ambazo hazitaleta madhara kwao.

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2927


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)
Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea k Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya propranolol ambayo hutibu magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili
Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa. Soma Zaidi...

Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.
Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa. Soma Zaidi...

Chini ya Tumbo langu Kuna uchungu lakini si sana shinda ni ni?
Nini kinasababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu? Soma Zaidi...

Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa ya Moyo DIGOXIN
Digoxin ni nini? Digoxin inatokana na majani ya mmea wa digitalis. Digoxin husaidia kufanya mapigo ya moyo kuwa na nguvu na kwa mdundo wa kawaida zaidi. Digoxin hutumiwa kutibu kushindwa kwa moyo. Digoxin pia hutumiwa kutibu mpapatiko wa atiria, ugonjw Soma Zaidi...

Fahamu dawa za kisukari
Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones
Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo. Soma Zaidi...

Dawa za mitishamba za kutibu meno
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno Soma Zaidi...