FAHAMU KUHUSU DAWA YA PYRANTEL PAMOATE


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.


Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate.

1. Pyrantel pamoate ni aina mojawapo ya dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo ukaa kwenye utumbo mdogo yaani kwa kitaalamu kwenye intestinal nematode hiyo ndiyo kazi yake na pia inaweza kufanya kazi kama dawa za Albendazole na mebendazole kwa sababu ya kupambana na aina ya minyoo inayotibiwa na na dawa hizo ambayo ni hookworm na pinworn.

 

2. Dawa hii pia ipo kwenye mfumo wa vidonge na pia utafunwa na kumezwa bila maji na pia utumika kabla ya kula kitu chochote ili kuweza kukabiliana vizuri na minyoo ambayo iko tumboni, kwa matumizi yake au namna ya kutumia ni kwa kadiri ya maagizo ya daktari au mtaalamu wa afya.

 

3. Pia dawa hii utumika kwa watu wote wakubwa na wadogo isipokuwa watoto wadogo chini ya miaka miwili na akina Mama wajawazito wenye mimba changa hawapaswi kutumia dawa hii kwa kuepukana na mimba kutoka, kwa hiyo wajawazito wanapaswa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya hasa wakiwa kliniki na sio kununua dawa na kutumia kwa sababu wanaweza kujiletea matatizo makubwa.

 

4. Pia dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika, kizunguzungu, kuchoka mara kwa mara kwa watumiaji wa dawa za pyrantel pamoate wakiona dalili kama hizi ni vema kabisa kufahamu kwamba ni matokeo ya dawa na pia hali ikiwa mbaya ni vema kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

5. Pia jamii inapaswa kuelewa kwamba dawa hii haitumiki kiholela ni kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya na kujua matumizi yake, endapo ikitumika visivyo inaweza kuleta matokeo mabaya kwa watumiaji hasa wajawazito na watoto chini ya miaka miwili, kwa hiyo kwa upande wa wajawazito ni vizuri kufuata masharti ya kliniki hasa mimba ikiwa changa katika matumizi ya dawa na pia mtoto anapaswa kupelekwa kliniki ikitokea kama anaumwa ili apewe dawa zake.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Maktaba ya vitabu    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

image Dawa ya Panadol au paracetamol katika kutuliza maumivu
Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa. Soma Zaidi...

image Dapsone na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Dapsone na kazi zake, hii ni dawa ambayo utumika katika kutibu ugonjwa wa ukimwi, dawa hii ufanya kazi kwa mchanganyiko wa dawa nyingine kama vile Rifampicin na clofaximine. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi. Soma Zaidi...

image Fahamu aina ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu
Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin. Soma Zaidi...

image Fahamu tiba ya jino
Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo utolewa na jino haliwezi kuuma , kufa ganzi au kutoboka kwa hiyo ifuatavyo ni tiba ya jino. Soma Zaidi...

image Fahamu Dawa itwayo Diazepam
Diazepam ni nini? Diazepam ni Dawa ambayo Huathiri kemikali kwenye ubongo ambazo zinaweza kukosa uwiano na kusababisha wasiwasi. Diazepam hutumiwa kutibu matatizo ya wasiwasi, dalili za kuacha pombe, au misuli. Diazepam wakati mwingine hutumiwa pamoja na dawa zingine kutibu kifafa. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa
Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa za cyclophosphamide na mustargen.
Post hii inahusu zaidi dawa za cyclophosphamide na mustargen katika kupambana na ugonjwa wa Kansa. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea. Soma Zaidi...