image

Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Dawa za kutibu magonjwa ya moyo.

1. Kwanza kabisa kabla hatujaanza kuchambua dawa moja baada ya nyingine tunapaswa kufahamu kabisa kuhusu magonjwa ya moyo, ambapo kwa lugha ya kitaalamu magonjwa ya moyo huitwa cardiac failure , magonjwa ya moyo ni hali ambayo utokea kama moyo umeshindwa kufanya kazi yake vizuri kwa mfano moyo kushindwa kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

2. Kwa kawaida kuna dalili mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza kama moyo haufanyi kazi vizuri na dalili hizi ni pamoja na uchovu wa mara kwa mara, kushindwa kupumua vizuri, na wakati mwingine kifua kubana , kukonda kusiko kwa kawaida hata kama mgonjwa anakuwa anatumia chakula na dalili nyingine zinaweza kujitokeza kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine.

 

3. Kutokana na kuwepo kwa magonjwa ya moyo kuna dawa mbalimbali ambazo utumika kutibu magonjwa ya moyo na lengo la dawa hizi ni kuhakikisha kwamba moyo unafanya kazi yake ipasavyo na kuhakikisha kwamba maumivu mbalimbali hayatokei kwa mgonjwa na pia dawa hizo zinatofautiana kutoka kwa dawa moja kwenda kwa nyingine kadri ya tatizo lilivyo.

 

4. Kuna dawa za moyo ambazo usaidia kama presha iko juu kitendo hiki kwa kitaalamu huitwa high blood pressure, hali hiyo uitwa magonjwa ya moyo kwa sababu kuna kipindi moyo unatumia nguvu kubwa kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili, hali hii ya moyo kutumia nguvu kusukuma damu utokea kwasababu ya mishipa ya damu kuwa nyembamba na kusababisha damu kutoweza kufika sehemu mbalimbali za mwili kusababisha moyo kutumia nguvu hali inayosababisha shinikizo la damu. Kwa hiyo kuna dawa za kutibu hali hiyo ya shinikizo la damu.

 

5. Pia kuna dawa za moyo ambazo usaidia kwenye matibabu ya kupambana  na shinikizo kali la damu ambalo usababisha kiharusi, kwa kitaalamu huitwa stroke na myocardial infarction, kwa kawaida tunafahamu kwamba iwapo shinikizo la damu limekuwa sugu usababisha kiharusi ,kwa hiyo pia tutaweza kuona dawa za kutibu hali hiyo.

 

6 pia kuna dawa vile vile ambazo usaidia kutibu hali ya presha kuwa chini, kuna  kipindi baada ya presha kubaki kwenye hali yake ya kawaida yenyewe inashuka hali inayosababisha matatizo kwa mgonjwa kama matibabu hayajatolewa, kwa hiyo tutaweza kuona dawa za kutibu hali hiyo.

 

7. Pamoja na kujua aina mbalimbali za magonjwa ya moyo tutaona jinsi dawa zinazotumika kutibu magonjwa ya moyo jinsi zinavyofanya kazi , kwanza dawa hizi uondoa chumvi kwenye moyo na maji yaliyozalishwa kwenye moyo  na kusababisha moyo kuwa kawaida na kuweza kufanya kazi vizuri,kwa hiyo ili moyo ufanye kazi unahitaji chumvi na maji sawia  yaani viwe vya kawaida, kwa hiyo maji yakiwa mengi kuzidi na chumvi ikizidi kwenye moyo ni hatari sana.

 

8. Pia dawa hizo usaidia kupandisha presha kama imeshuka na kuiweka kwenye hali ya kawaida, dawa ambayo kwa kawaida utumika uhakikisha kwamba presha hatishuki ovyo ovyo.

 

9. Pia dawa hizo upanua mishipa ya damu kama ni midogo na kusababisha damu kuweza kupita vizuri na kwenda kwenye sehemu mbalimbali za mwili na kushusha presha na ikiwa ya kawaida.

 

10. Baada ya kufahamu kazi za dawa hizi za magonjwa ya moyo na kufahamu magonjwa mbalimbali ya moyo ni vizuri kufahamu kwamba kila ugonjwa wa moyo huwa na dawa zake maalum ambazo utumika kutibu ugonjwa huo kwa hiyo ni vizuri kabisa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya.

 

11. Kwa hiyo baada ya kufahamu tofauti za magonjwa ya moyo ni vizuri kupima kwanza ili kufahamu kwamba upo kwenye kundi gani na kupewa dawa kadri ya tatizo.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1313


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Dawa za kutibu ugonjwa wa macho
Somo Hili linakwenda kukuletea dawa za kutibu ugonjwa wa macho Soma Zaidi...

Dawa ya fangasi ukeni
Makala hii itakueleza dawa ya kutibu fangasi wa ukeni Soma Zaidi...

Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin Soma Zaidi...

Fahamu matumizi ya Ampicillin.
Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici Soma Zaidi...

DAWA YA FANGASI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi Soma Zaidi...

Matibabu ya Fangasi ukeni na dawa za fangasi wanaoshambulia uke.
Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni Soma Zaidi...

Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio
Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo. Soma Zaidi...

Ijue Dawa ya lignocaine
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji. Soma Zaidi...

Dawa ya UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya UTI Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji
Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii imetoka kwenye kundi la vasodilators, na pia usaidia sana kwenye matibabu ya magonjwa ya moyo. Soma Zaidi...

dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo
MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi. Soma Zaidi...