picha

Fahamu kuhusu kundi la diuretics

Post hii inahusu zaidi kundi la diuretics,ni kundi mojawapo kati ya makundi ya dawa zinazosaidia katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Fahamu kuhusu kundi la diuretics.

1. Diuretics ni mojawapo ya kundi kwenye dawa za kutibu magonjwa ya moyo,kundi hili pia Lina dawa mbalimbali ambazo utumika kwenye matibabu, kundi hili la dawa ni kuzalisha mkojo Ili kuweza kutoa sumu mwilini ambazo ni chanzo cha kusababisha kuwepo au kuongezeka kwa tatizo kwenye moyo.

 

2. Dawa hizi ambazo zipo kwenye Kundi hili la diuretics zikitumika uweza kufanya kazi kupitia kwenye Figo na baadae kuongeza kiwango cha kuzalishwa kwa mkojo , kwa hiyo baada ya kutolewa mkojo nje uweza kusababisha moyo kuendelea na kazi yake kama kawaida,kwa sababu sumu utoka nje kupitia kwenye mkojo.

 

3. Dawa hizi kwenye kundi la diuretics ni pamoja na furosemide, bendofurothiazide, potassium sparing diuretics- spirolactone na amiloride hizi dawa ni kutokana na kundi Moja la diuretics lakini ufanya Kazi tofauti tofauti kutegemea na tatizo la mgonjwa.

 

4. Vili vile dawa hizi huwa na maudhi madogo madogo katika matumizi na maudhi hayo ni pamoja na kukojoa sana au pengine kizunguzungu na kutapika hasa kwa watumiaji ambayo wanaaoanza kutumia dawa,pia dawa hizi zina tabia ya kupandisha sukari juu  ,kwa hiyo wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari hasa ya kupanda wanapaswa kuwa makini katika matumizi ya dawa hii.

 

5. Vili vile kwa sababu dawa hii Inafanya mtu akojoe sana Ina tabia vile vile ya kupunguza madini mwilini kwa sababu madini mengi upitia kwenye mkojo na kutolewa nje, kwa hiyo ni vizuri na kuwa makini kwa wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini.

 

6. Vile vile dawa hizi zinapaswa kutumiwa kadri ya wataalamu wa afya sio kuzitumia kiholela na pia watu wenye tatizo la kisukari hasa ya kupanda na wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini wanapaswa kuwa macho katika matumizi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2732

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Faida za dawa za NMN

Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya aminophylline kutibi maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE

Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital

Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.

Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa.

Soma Zaidi...