Fahamu kuhusu kundi la diuretics
Post hii inahusu zaidi kundi la diuretics,ni kundi mojawapo kati ya makundi ya dawa zinazosaidia katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Fahamu kuhusu kundi la diuretics.
1. Diuretics ni mojawapo ya kundi kwenye dawa za kutibu magonjwa ya moyo,kundi hili pia Lina dawa mbalimbali ambazo utumika kwenye matibabu, kundi hili la dawa ni kuzalisha mkojo Ili kuweza kutoa sumu mwilini ambazo ni chanzo cha kusababisha kuwepo au kuongezeka kwa tatizo kwenye moyo.
2. Dawa hizi ambazo zipo kwenye Kundi hili la diuretics zikitumika uweza kufanya kazi kupitia kwenye Figo na baadae kuongeza kiwango cha kuzalishwa kwa mkojo , kwa hiyo baada ya kutolewa mkojo nje uweza kusababisha moyo kuendelea na kazi yake kama kawaida,kwa sababu sumu utoka nje kupitia kwenye mkojo.
3. Dawa hizi kwenye kundi la diuretics ni pamoja na furosemide, bendofurothiazide, potassium sparing diuretics- spirolactone na amiloride hizi dawa ni kutokana na kundi Moja la diuretics lakini ufanya Kazi tofauti tofauti kutegemea na tatizo la mgonjwa.
4. Vili vile dawa hizi huwa na maudhi madogo madogo katika matumizi na maudhi hayo ni pamoja na kukojoa sana au pengine kizunguzungu na kutapika hasa kwa watumiaji ambayo wanaaoanza kutumia dawa,pia dawa hizi zina tabia ya kupandisha sukari juu ,kwa hiyo wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari hasa ya kupanda wanapaswa kuwa makini katika matumizi ya dawa hii.
5. Vili vile kwa sababu dawa hii Inafanya mtu akojoe sana Ina tabia vile vile ya kupunguza madini mwilini kwa sababu madini mengi upitia kwenye mkojo na kutolewa nje, kwa hiyo ni vizuri na kuwa makini kwa wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini.
6. Vile vile dawa hizi zinapaswa kutumiwa kadri ya wataalamu wa afya sio kuzitumia kiholela na pia watu wenye tatizo la kisukari hasa ya kupanda na wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini wanapaswa kuwa macho katika matumizi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili
Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa.
Soma Zaidi...Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria
Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.
Soma Zaidi...Fahamu matumizi ya Ampicillin.
Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici
Soma Zaidi...Fahamu dawa za kutibu mafua
Post hii inahusu dawa za kutibu mafua ambazo ni cough seppessants na nasal congestion ni dawa ambazo zimependekezwa kwa ajili ya kutibu mafua.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Soma Zaidi...