Fahamu kuhusu kundi la diuretics
Post hii inahusu zaidi kundi la diuretics,ni kundi mojawapo kati ya makundi ya dawa zinazosaidia katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Fahamu kuhusu kundi la diuretics.
1. Diuretics ni mojawapo ya kundi kwenye dawa za kutibu magonjwa ya moyo,kundi hili pia Lina dawa mbalimbali ambazo utumika kwenye matibabu, kundi hili la dawa ni kuzalisha mkojo Ili kuweza kutoa sumu mwilini ambazo ni chanzo cha kusababisha kuwepo au kuongezeka kwa tatizo kwenye moyo.
2. Dawa hizi ambazo zipo kwenye Kundi hili la diuretics zikitumika uweza kufanya kazi kupitia kwenye Figo na baadae kuongeza kiwango cha kuzalishwa kwa mkojo , kwa hiyo baada ya kutolewa mkojo nje uweza kusababisha moyo kuendelea na kazi yake kama kawaida,kwa sababu sumu utoka nje kupitia kwenye mkojo.
3. Dawa hizi kwenye kundi la diuretics ni pamoja na furosemide, bendofurothiazide, potassium sparing diuretics- spirolactone na amiloride hizi dawa ni kutokana na kundi Moja la diuretics lakini ufanya Kazi tofauti tofauti kutegemea na tatizo la mgonjwa.
4. Vili vile dawa hizi huwa na maudhi madogo madogo katika matumizi na maudhi hayo ni pamoja na kukojoa sana au pengine kizunguzungu na kutapika hasa kwa watumiaji ambayo wanaaoanza kutumia dawa,pia dawa hizi zina tabia ya kupandisha sukari juu ,kwa hiyo wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari hasa ya kupanda wanapaswa kuwa makini katika matumizi ya dawa hii.
5. Vili vile kwa sababu dawa hii Inafanya mtu akojoe sana Ina tabia vile vile ya kupunguza madini mwilini kwa sababu madini mengi upitia kwenye mkojo na kutolewa nje, kwa hiyo ni vizuri na kuwa makini kwa wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini.
6. Vile vile dawa hizi zinapaswa kutumiwa kadri ya wataalamu wa afya sio kuzitumia kiholela na pia watu wenye tatizo la kisukari hasa ya kupanda na wale wenye tatizo la upungufu wa madini mwilini wanapaswa kuwa macho katika matumizi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 ai web app 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Faida za vidonge vya zamiconal
Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi.
Soma Zaidi...Madhara ya Tiba mionzi
Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.
Soma Zaidi...Dawa ya fangasi na dalili za fangasi
hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi
Soma Zaidi...Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa
Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.
Soma Zaidi...