Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.
Madhara ya uzito kuwa mkubwa.
1 kwanza kabisa tunafahamu kwamba uzito mkubwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu, kuna watu wengine ni kawaida kuwaa wanene kwa sababu familia yao yote wanafanana hivyo wanakuwa na miili mikubwa pia na uzito mkubwa,ila kama kwa asilimia mwili ulikuwa mdogo na kwa sababu ya mtindo wa maisha mwili umeongezeka ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa umepunguza uzito kwa namna moja au nyingine kwa sababu kuna madhara mbalimbali yanaweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa kama tutakavyoona.
2. Kuwepo kwa maumivu makali kwenye mgongo.
Maumivu hayo uanzia kiunoni na kushuka kueneza kwenye mgongo hali hiyo utokea kwa sababu pingili za kwenye mgongo Uweza kuelemewa na kusababisha pingili kuchoka na kusababisha maumivu kwenye mgongo hali ambayo kwa wakati mwingine usababisha pingili za kwenye utu wa mgongo kusagika.
3. Kuna wakati mwingine kama unene umekuwa mkubwa sana usababisha matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na kushindwa kubeba ujauzito kwa wanawake kwa hiyo ni vizuri kabisa kupunguza uzito ili kuweza kupunguza na matatizo mengine ya maisha yakiwemo kushindwa kubeba mimba.
4. Kuwepo kwa shinikizo la damu.
Kwa kawaida unene na uzito ukiwa mwingi pia usababisha na kuwepo kwa Tatizo la shinikizo la damu kwa sababu mishipa huwa midogo na kusababisha moyo kutumia nguvu ili kuweza kusukuma damu kwa nguvu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
5. Kuwepo kwa kufa ganzi kwenye sehemu mbalimbali.
Kuna kipindi kunakuwepo na ganzi kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa sababu ya hewa ya oxygen gas inakuwa haifiki sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha kuwepo kwa ganzi kwenye mikono, miguu na sehemu nyingine.
6. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kwamba tunapunguza uzito na kuwa kwenye hali ya kawaida kwa sababu kuwepo kwa uzito mkubwa ni chanzo cha kuwepo pia kwa magonjwa mbalimbali.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 ai web app 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walioingiliwa na uchafu puani.(foreign body).
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa alieye ingiwa na uchafu puani (foreign body)
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu vitamini D na kazi zake mwilini
Hapa utajifunza kuusu vitamini D, kazi zake, upungufu wake na chanzo cha kupata vitamini D.
Soma Zaidi...Vyakula vya fati na mafuta
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya fati na mafuta
Soma Zaidi...Mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe
Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana.
Soma Zaidi...Huduma ya kwanza kwa aliyeungua moto
Post hii inahusu namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyeungua moto, kuingia moto ni kitendo Cha kubabuka ngozi ya juu inaweza kuwa kwa kemikali,umeme na just,
Soma Zaidi...Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.
Soma Zaidi...