picha

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma

Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae.

Ufahamu ugonjwa wa ukoma.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba Ugonjwa huu unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa kugusana na mtu mwingine au kwa hewa kwa hiyo ni vizuri kuepuka kugusana na watu wenye ukoma na pia kuepukana kugusana na watu wenye ukoma bila sababu na tuwe na tahadhari wakati wa kugusana nao.

 

2. Kuna Dalili mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza kwa mtu mwenye Ugonjwa wa ukoma kama vile Neva za mwili  kushindwa kufanya kazi hali ambayo Usababisha hata vidole vya mikono au miguu kudondoka bila mgonjwa mwenyewe kuwa na taarifa kwa hiyo hali hii upelekea wagonjwa kujitenga na jamii wakijiona kama wana  mapungufu na sio kama watu wengine.

 

3. Pia mgonjwa anahisi mwili wake unawaka moto hasa hasa kwenye sehemu za Maambukizi kwa hiyo mgonjwa uhisi kuwa na hali ya kutotulia kwa sababu ya hali anayoisikia.

 

4. Kutohisi maumivu kwenye sehemu yenye Maambukizi kwa kuwa hakuna mawasiliano kwenye mwili wa mgonjwa hata sehemu zinazokatika Maumivu yanakuwa hayapo 

 

5. Kutokuwepo kwa maumivu kwenye vidonda,tunaelewa kwamba kama kuna vidonda kwenye sehemu ya mgonjwa mara nyingi Maumivu huwa hayapo hali ambayo uwafanya wagonjwa kutoona umuhimu wa kutibu tatizo lao kwa sababu hata kwenye vidonda hakuna maumivu kwa hiyo vidonda uongezeka hali inayopelekea kuongezeka kwa Maambukizi.

 

6.Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwapeleka wagonjwa wa ukoma hospitalini ili wapate dawa kwa sababu kuna dawa ambazo utibu huu Ugonjwa na wengi wamepona kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwahi matibabu mapema maana kadri unavyowahi na matibabu huwa ya kawaida.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3700

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 ai web app     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Nini hasa chanzo cha pumu, na je inarithiwa?

Ugonjwa wa pumu ni moja katika magonjwa hatari yanayoweza kutokea kwa ghafla, na endapo itacheleweshwa kudhibitiwa inaweza sababisha athari mbaya zaidi

Soma Zaidi...
Kisonono sugu: Sababu za kutosikia dawa na tiba yake.

​Kisonono (Gonorrhea) ni maambukizi ya zinaa (STI) yanayosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae. Ingawa kimsingi ugonjwa huu hutibika kwa urahisi kwa antibiotics, kuibuka kwa kisonono kisichosikia dawa (drug-resistant gonorrhea) kumegeuka kuwa tishio kubwa la afya ya jamii. Makala haya yanachunguza kwa nini baadhi ya maambukizi huwa sugu, hatari zake, na umuhimu wa kufuata taratibu za kitabibu ili kupata uponyaji kamili.

Soma Zaidi...
Fangasi watambulikao kama invasive candidiasis

Hawa huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenda maeneo mengine nyeti sana ya mwili.

Soma Zaidi...
Kazi ya figo: Dalili za awali za kushindwa kufanya kazi.

​Katika ulimwengu wa sasa wenye kasi kubwa, uchovu wa mwili umekuwa changamoto sugu kwa wengi. Makala hii inachunguza kwa kina vyanzo mbalimbali vya uchovu—kuanzia mambo ya mtindo wa maisha, matatizo ya kisaikolojia, hadi magonjwa ya msingi ya kiafya. Lengo ni kutoa ufahamu wa kina kuhusu jinsi ya kutambua dalili, sababu za kisayansi, na mikakati madhubuti ya kurejesha nishati yako ya mwili na akili.

Soma Zaidi...
Dalili za UTI upande wa wanawake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake

Soma Zaidi...
Dalili za Mgonjwa wa kisukari

Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.

Soma Zaidi...