Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtot

Kaswende wakati wa ujauzito.

1. Kaswende ni ugonjwa ambao uenezwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Treponema pallidum ambaye kwa kawaida upitia kwenye njia ya kujamiiana kwa mtu ambaye ana ugonjwa huo akijamiiana na mtu ambaye hana ugonjwa huo,kwa kawaida wadudu hao wakiwa kwenye damu ya mama uweza kuingia kwa mtoto kupitia kwenye kondo la nyuma na kuweza kushambuliwa mtoto, ikiwa mama hatajulikanaa mapema kama ana ugonjwa huo mtoto anaweza kupata matatizo mbalimbali kama vile kuzaliwa akiwa kipofu au mtoto kufia tumboni.kwa hiyo ni vizuri kabisa akina Mama wakiwa wajawazito waweze kupima kaswende na iwapo mama akiwa na ugonjwa huo

 aanze matibabu mara moja.

 

2. Kwa kawaida ni vizuri kabisa akina mama wajawazito wanaoanza mahudhurio ya kliniki waweze kwenda na waume zao ili nao waweze kupima kaswende kwa sababu ukimtibu Mama pekee yake na huko na baba ana ugonjwa huo unakuwa umefanya kazi bure kwa hiyo ni vizuri kabisa kupima wote na wakigundulika wana ugonjwa huo ni vizuri kabisa kupewa dawa na wote waanze matibabu ili kuweza kunusuru maisha ya mtoto, pia kuna tatizo moja ambalo utokea ikiwa wote baba na Mama wamekuja kupima na wakagundulika wote wana maambukizi ni vizuri kabisa kuwashauri kabla ya kuwapima ili watoe hali ya kuanza kuulizana kwamba ni nani aliyeleta ugonjwa huu bali wote watibiwe na kuokoa maisha ya mtoto.

 

3. Pia  jinsi na njia ambazo uweza kusababisha kusambaa kwa kaswende kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, ya kwanza ni kufanya ngono zembe hali hii utokea pale mtu mwenye kaswende anapofanya ngono na mtu ambaye hana kaswende bila kupima afya zao na bila kutumia kondomu yaani ngono ya nyama kwa nyama, kwa hiyo watu wanashauliwa kama wanataka kufanya ngono zembe ni vizuri kabisa kupima afya zao ili kuweza kufahamu kama wana maambukizi au kama hawakuweza kupima ni vizuri kutumia kondomu, kwa hiyo jamii inapaswa kuelimika kuhusu ugonjwa huu hatari na kujihadhari kwa sababu madhara yake ni makubwa ingawa kwa bahati nzuri unatibika ila kinga ni nzuri  hasa hasa vijana wanapaswa kufahamu jambo hili kwa sababu wenyewe ndio tegemeo la taifa la kesho pia ndio wapo kwenye mategemeo ya kupata watoto wenye afya nzuri sio wenye kaswende na matatizo yote yanayohusiana na mambo kama hayo.

 

4. Njia ya pili ambapo ugonjwa huu unasambaa ni kujamiiana na mwanaume ambaye anajamiiana na wanaume wengine,

Tunavyojua kwa sasa hali ya ulimwengu ilivyo Kuna wanaume wanaojamiiana na wanaume wengine na pia huko ana mke mwenye mimba na anategemea kupata mtoto mwenye afya nzuri, kwa njia hii pia kaswende inaweza kueneza kutoka kwa mwanaume kwenda kwa mwanaume na kutoka kwa mwanaume kwenda kwa mwanamke na pia mwanamke kama ana mimba ana asilimia zote za kumwambikiza mtoto. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuachana na njia hizi za kujamiana hasa wanafamilia kama wanategemea kupata watoto kwa sababu hali kama hiyo ni hatari kwa familia na jamii nzima kwa sababu watoto wenye ulemavu wanapatikana na pia watoto wanapoteza maisha wakiwa mimba. Kwa hiyo jamii inapaswa kuelimika na kuhakikisha wanapunguza maambukizi ya kaswende hasa kwa wajawazito.

 

5. Pia wanawake wenye kiwango kikubwa cha virusi vya ukimwi,

Kwa kawaida mama akiwa na maambukizi na hatumii dawa inawezekana pengine anakuwa hajui kama ana maambukizi kwa sababu hajapima. Kwa kawaida mtu akiwa na maambukizi na kinga ya mwili inashuka kwa hiyo ni rahisi kabisa kupata maambukizi ya kaswende, kwa hiyo akina mama pindi wanapopata mimba ni vizuri kabisa kwenda kupima magonjwa hatarishi kwa mtoto na pia wasiende wenyewe ila waende na waume zao,na wakigundulika kwamba wana maambukizi ni vizuri kabisa kuanza matibabu mara moja ili kulinda afya ya mtoto.

 

6.Wanawake wenye wapenzi zaidi ya mmoja.

Pia na hili ni tatizo unaweza kukuta mwanamkea ana familia yake ana mme wake na pia ana wapenzi wengi nje na pia anajamiiana nao bila kinga ,na kuna wakati mwingine mama anakuwa ameshatoka kliniki kupima pamoja na mme wake na kukutwa hawana maambukizi ila mama anaendelea kutembea na wanaume wengi na bila mpangilio, kwa hiyo tunawasihi akina Mama wote wakishabeba mimba watulie na mme mmoja na hata kama labda mimba hiyo imepatikana bila matarajio au mama hana matunzo anapata matunzo kutoka kwa wanaume mbalimbali ila kwa usalama wa mtoto na kuepuka kupata mtoto wa ajabu atakayekutesa maisha yako yote ni vizuri kabisa kumlinda mtoto akiwa tumboni kwa kuachana nakutembea na wanaume wengi wakati wa ujauzito na kusababisha maambukizi ya kaswende kwa mtoto.

 

7. Napenda kuwashauri akina Mama na baba pia kwamba kaswende inatibika pindi ukipata ugonjwa huu ni vizuri kwenda hospitali kwa ajili ya matibabu na pia wazazi wanapaswa kuja madhara ya kaswende kwa mtoto ambapo mtoto anaweza kuzaliwa akiwa kipofu au na ulemavu wowote au pengine anaweza kuzaliwa akiwa mfu, na pia ugonjwa huu unaweza kukaa kwenye mwili wa mtu kwa mda mrefu kwa hiyo ni vizuri kabisa kupima afya mara kwa mara, na kwa upande wa vijana wanapaswa kulinda maisha yao kwa kuepuka maambukizi haya ambayo yanasababisha kuwepo kwa watoto wasiohitajika kwenye jamii pia kuacha ngono zembe na pia kuwa waaminifu kwenye mahusiano maana vijana ndilo taifa la kesho.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/11/16/Wednesday - 01:03:04 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 631

Post zifazofanana:-

Njia ambazo VVU huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa Soma Zaidi...

Uyoga (mushrooms)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga Soma Zaidi...

Faida za vidonge vya zamiconal
Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi. Soma Zaidi...

Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa wanawake.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kufunga kizazi kwa wanawake. Soma Zaidi...

Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe
Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao. Soma Zaidi...

Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake. Soma Zaidi...

Njia za kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuongeza nguvu za kiume Soma Zaidi...

ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan
Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya. Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo, ni hatari inayotokea kwa mtu ambaye haujatibiwa vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Je bado unasumbuliwa na nguvu za kiume?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume Soma Zaidi...

What is Bongoclass
What is Bongoclass and what does it do to the individuals and whole community. Soma Zaidi...