Menu



Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango

Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana

Mtazamo juu ya matumizi ya kondonu umekuwa ukikabiliwa na imani za kidini. Zipo dini ambazo zinakataza kabisa, lakini zipo ambazo zinakubali endapo kutakuwa na haja ya kiulazima za kiafya. Kwa vyovyote itakavyokuwa haja ya kutumia kondomu ipo kulingana na sababu mbalimbali. Sababu nyingine zinakubaliwa na dini zote kwa mfano kuzuia kizazi endapo itaonekana ni hatari kwa mwanamke huwenda akapoteza maisha pindi akipata ujauzito, ama kulinda ndoa ambazo mmoja wao ameathirika. Zipo sababu nyingine ambazo zinaweza kukubalika katika dini zote.

 

Sasa kwa kuwa hali ya matumizi ya kondomu yapo kama hivyo basi ipo haja ya watu kuelezwa faida na hasara ambazo unaweza kuzipata kama utaamuwa kutumia kondomu. Faida hizi na hasara zitasaidia kukukumbusha kuendelea kuwa makini hata ukiwa unatumia kondomu.

 

Aina za kondomu

1. Kondomu ya kike ambayo huvaliwa na mwanamke wakati wa kujamiiana

2. Kondomu ya kiume, hii ni Aina ya kondomu inayovaliwa na mwanaume wakati wa kujamiiana

 

Faida za kutumia kondomu

1. Kuzuia kuongezeka kwa mimba zisizotarajiwa

2. Kuzuia magonjwa ya ngono

3. Kuzuia kuambukizwa kwa ugonjwa wa Ukimwi

Kati ya njia za uzazi wa mpango kondomu ndiyo njia pekee inayosaidia kupunguza kusambaa kwa magonjwa ya ngono na Ukimwi

 

Hasara za kutumia kondomu

1. Kondomu hukinga maambukizi ya magonjwa ya ngono, yanayoingia kwa njia ya ngono, lakini upo uwezekano wa kupata endapo kindomu itapasuka, ama itavuka wakati wa tendo. Pia kama kuna mikato iliyosababishwa na kunyoa na ikawa ipo wazi kuruhusu vijidudu kupendya kwa wawili hawa upo uwezekano wa kupata magonjwa. Ama kuvuka kwa kondomu au kupasuka upo uwezekano wa kupata ujauzito. Ijapokuwa hali hizi ni mara chache sana kutokea. hii inakuwa hasara endapo mtu atajiamini kwa asilimoa 100 kuwa yupo salama anapotumia kondomu bila ya kuchukuwa tahadhari nyingine.

 

2. kondomu kwa baadhi ya watu inawaletea allegi kama miwasho na mapele. Hii inatokana na mafuta yanayowekwa. Kwa baadhi ya watu miili yao haiendani na mafuta hayohivyo kuwasababishia aleji kila wanapotumia. Zungumza na daktari endapo una tatizo hili la aleji unapotumia kondomu.

 

3. kuna baadhi ya kondomu zinawekwa vilainishi vya Nonoxynol-9 kwa ajili ya kuuwa mbegu za kiume. Vilainishi hivi vinaweza kusababisha madhara kwenye uke kama kuwashwa hivyo kupelekea kuongezeka kwa hatari ya kupata maradhi ya ngono.

 

Kuwepo kwa hasara hizi inamaanisha kuwa watumiaji wa kondomu wawe makini wasijipe matumaini ya kuwa salama kwa asilimia 100, kwani chochote kinaweza kutokea.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 8100

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Mabadiliko ya uzito kwa mjamzito

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya uzito kwa mjamzito, hii ni hali ya kubadilika kwa uzito kwa Mama akiwa na Mimba

Soma Zaidi...
Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima

Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasip

Soma Zaidi...
Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia vidonge kwa akina dada vya uzazi wa mpango

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia vidonge vya uzazi wa mpango kwa akina dada.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa Wanaume

Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Posti hii inaelezea kiufupi kabisa kuhusiana na Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba

Soma Zaidi...
Mwanaune anapataje fangasi kwenye uume

Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.

Soma Zaidi...