picha

Faida za vitamin C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vitamini C mwilini

FAIDA ZA VITAMINI C MWILINI

 

Kama tulivyokwisha kuona vyakula vya vitamini C kama vile papai, machungwa, mananasi, maembe, malimao na ndimu. Pia tuliona baadhi ya kazi za vitamini C ambazo ni kusaidia katika kuuwa kemikali mbaya mwilini, kuipa nguvu miili yetu ya kupambana na maradhi. Katika makala hii nitakwenda kukujuza umuhimu wa vitamin C katuka mwili wa kila kiumbe akiwemo binadamu.

 

Faida na umuhimu wa vitamini C

1.Hulinda mwili dhidi ya maradhi ya kiseyeye (scurvy): Haya ni maradhi ambayo hufanya mwili uweze kutoa damu kwenye mafinzi, mwili kuchubuka kwa urahisi, kuchelewa kupona kwa majeraha. Kusoma zaidi kuhusu ugonjwa huu pitia zaidi makala zetu.

 

2.Kulinda mwili zidi ya maambukizi na mashambulizi:

Tafiti mbalimbali zilizofanya zinaonesha kuwa vitamini C inaweza kusaidia kupunguza nguvu za virusi waletao mafua na homa ya mafua. Baadhi ya tafiti zinadiriki kusema kuwa vitamini hivi kuponyesha mafua yaa kwa haraka, lakini ambalo halina shaka ni kuwa vitamini c vinaweza kupunguza kupata mafua ya mara kwa mara au kufanya mafua yaondoke kwa haraka.

 

3.Vitamini C ni muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini. Kwani vitamini C husaidia katika Antimicrobial yaani katika kuzuia vijidudu shambulizi mwilini kama bakteria na virusi, pia vitamini C husaidia katika Natural killer cell yaani katika kuuwa vijidudu shambulizi ama kuvizuia visiendelee kukua mwilini, pia vitamini C husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga kwa kuimarisha seli hai nyeupe ziitwazo lymphocyte hizi ndizo seli ambazo askari mkuu wa mwili dhidi ya vimelea vya maradhi kama virisi, fangasi, protozoa na bakteria.

 

4.Kulinda miili yetu dhidi ya saratani (cancer):

Tafiti mbalimbali zimefanywa kuhusu aina ya saratani na zinavyohusiana na vitamini C kama saratani ya matiti na mapafu. Ijapokuwa tafiti hizi hazikuweza kuthibitisha moja kwa moja kuwa vitamini C vinasaidia kuondoa saratani hizi kalaki kuna mambo ambayo tafiti hizi yametufungua mawazo:

A. Vitamini C husaidia kuborsha afya na kuishi vyema kwa wagonjwa wa saratani

B. Vitamini C inaweza kuuwa seli zinazotengeneza uvimbe wa saratani

 

5.Husaidia kulind miili yetu dhidi ya maradhi yanayohusu mishipa ya damu na moyo (cardiovascular)

 

6.Husaidia kulinda miili yetu dhidi ya maradhi ya ubongo na kusahasahau

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-11-03 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 8569

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 ai web app    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 web hosting    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula spinach

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula spinach

Soma Zaidi...
Karoti

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula karoti

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za peaz/ peas

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula peazi/peas

Soma Zaidi...
Orodha ya madini, chanzo chake na faida zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu orodha ya madini chanzo chake na faida zake

Soma Zaidi...
Vyakula vinavyopendekezwa kwa mtu mwenye kisukari.

Tutazungumzia: Makundi ya vyakula rafiki kwa mgonjwa wa kisukari. Namna ya kuchagua chakula chenye sukari ndogo kwa mwili. Mifano ya vyakula vya kula na vile vya kupunguza.

Soma Zaidi...
Faida za kula papai

Posti hii inaonyesha Faida za kula papai.papai Ni tunda na Lina leta afya,nguvu na kuujenga mwili.

Soma Zaidi...
Faida za kula ukwaju

Uchachu wa ukwaju, ndio ubora wake, kuna virutubisho vingi kwa kula ukwaju, soma makala hii

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya kula

Zijuwe sababu kuu za kuwepo kwa maumivu ya tumbo baada ya kula chakula

Soma Zaidi...