picha

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) Ugiriki
Tunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika. Lakini utakuta kuwa hadhi ya mwanamke katika jamii hiyo ilikuwa chini sana. Bwana E.A. Allen katika kitabu chake "History of Civilization Vol. 3" anasema mwanamke wa Kigiriki alilazimishwa kuolewa pasina idhini yake. Mumewe huyo alihesabiwa kuwa Bwana (Lord) wake. Mwanamke alihesabiwa kuwa ni kama mtoto na kwahiyo alitakiwa kumtii mumewe bila kuhoji. Wanawake huko Ugiriki waligawanyika katika makundi matatu:



(i)Makahaba (Malaya) ambao kazi yao ilikuwa ni kuwastarehesha wanaume tu.
(ii)Watumishi ambao kazi yao ilikuwa kuangalia na kutunza siha za mabwana zao.
(iii)Wake amabo kazi yao ni kuzaa na kulea watoto.



Mke alitakiwa awe mwadilifu na achunge murua wake lakini haikuwa vibaya kwa mwanamume kujamii nje ya ndoa. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwa wanawake makahaba wakawavutia watu wa ngazi zote - wanafalsafa, washairi, wanahistoria, wanafasihi na wasanii. Picha na sanamu za wanawake walio uchi zikazidi kuchochea zinaa na ufasiki. Ndoa ikaja kuonekana kuwa kero na zinaa ikawa jambo takatifu. Kuzama katika uzinifu kuliwapeleka Wagiriki kuchonga na kuabudu Aphrodite - mungu wa kike wa urembo na mahaba.


Kwa mujibu wa mafundisho ya Wagiriki ni kuwa huyo "Aphrodite" anasemekana kuwa alikuwa ni mungu wa kike aliyeolewa na mungu mwingine. Lakini hakutosheka na mume huyo mmoja. Akaanza kuzini na miungu wengine watatu na akawa pia anazini na binaadamu mmoja. Mungu huyo alipofanya jimai na binaadamu, wakazaa mungu wa kiume aliyeitwa Cupid yaani mungu wa mapenzi. Uzinifu wa "Aphrodite" na kuabudiwa kwake na Wagiriki ni kielelezo cha namna jamii hii iliwatukuza makahaba na kuupa uzinzi hadhi kubwa.


Kutokana na haya tunajifunza kuwa mwanzoni mwanamke katika jamii ya Ugiriki alidunishwa sana. Baadaye jamii ilipopiga hatua mbele katika maendeleo ya kiuchumi, hadhi duni ya mwanamke ilibadilishwa sura. Mwanamke aligeuzwa kuwa chombo cha kuwastarehesha wanaume jambo ambalo lililzidi kumdunisha na kumdhalilisha.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1518

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu

Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu

Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu

Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu

Soma Zaidi...
Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...