picha

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) Warumi
Jamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu. Je jamii hii ilimpa mwanamke heshima na hadhi anayostahiki? Katika historia ya Urumi tunajifunza kuwa Warumi walimwona mwanamke kama mtoto anayetakiwa kuangaliwa na kukemewa. Akiolewa yeye na mali yake ni mali ya mume. Akikosea, mume alikuwa na mamlaka ya kupitisha hukumu yoyote.aliyoweza hata ya kutoa adhabu ya kifo.



Mwanamke alikatazwa kushiriki katika jambo lolote. Hakuruhusiwa kutoa ushahidi wala kumuwekea mtu dhamana. Mumewe akifariki, Shemeji zake walikuwa na haki ya kumrithi.



Hapo awali katika historia ya Urumi, wanawake walibakia nyumbani na ukahaba (umalaya) haukujulikana. Mtu kufanya kitendo cha mapenzi na mkewe kama vile kumbusu mkewe hadharani ilionekana ni kitendo kiovu na utovu wa adabu na heshima. Kiongozi mmoja wa Kirumi alishutumiwa vibaya na raia wake kwa kitendo cha kumbusu mkewe mbele ya binti yake.



Warumi waliposongambele katika maendeleo ya kijamii, waliona wamkomboe mwanamke kwa kulegeza sharia ya ndoa kiasi cha kuifanya kama mkataba wa wawili wanaopendana. Wanawake walipewa haki ya kurithi na walikuwa huru na mamlaka ya baba au mume. Katika wakati huu sio tu kuwa wanawake wa Kirumi walijitegemea kiuchumi bali walikuwa wakiwakopesha waume zao kwa nba kubwa kwa kiasi kwamba Wanaume ambao wake zao walikuwa matajiri walijikuta wamekuwa watumwa wao.
Kutaliki kulikuwa jambo jepesi na ndoa zilikatika bila ya sababu za msingi.


Kwa mfano Seneca (4B.C - 65 A.D), Mwanfalsafa Mashuhuri wa Kirumi alitoa shutuma kwa watu wake kutokana na kiwango cha talaka kilicho kithini katika jamii yake kwa kusema: "Now divorce is not regarded as something shameful in Rome. Woman calculate their age by the number of husbands they have taken."



Tafsiri:
"Talaka sasa hainonekani kuwa nijambo la aibu hapa Urumi. Wanawake wanahesabu umri wao kwa idadi ya Wanaume waliofunga nao ndoa."



Yaani, wanawake wa Kirumi katika wakati huo wa historia, kwa uhuru waliopewa na jamii waliweza kuolewa na wanaume wengi kwa muda mfupi. Kwa mfano Martial (43 A.D - 104 A.D) ameeleza juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume kumi. Juvenal (60 A.D - 130 A.D) ameandika juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume wanane, mmoja baada ya mwingine, katika kipindi cha miaka 8. St. Jerome (340 A.D - 420 A.D) ameeleza juu ya mwanamke wa ajabu ambaye mume wake wa mwisho alikuwa wa 23, mmoja baada ya mwingine. Yeye mwenyewe kwa mumewe huyo wa mwisho alikuwa ni mke wake wa 21. ni katika wakati huu uzinifu ulianza kustawi na wazinifu hawakuhesabiwa kuwa ni wakosaji wanaostahiki kuadhibiwa.



Katika historia hii fupi, tunajifunza jisni mwanamke alivyokandamizwa na jamii hapo awali na tumeona hali ya mwanamke ilivyokuwa baada ya kukombolewa. Je, ukombozi huu ulimpa mwanamke hadhi yake anayostahiki?




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1540

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 ai web app    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii

Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?

Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Sunnah za udhu

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu sunah za udhu

Soma Zaidi...
Hijja na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya sadaqat

Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Maana ya elimuElimu ni ujuzi ulioambatanishwa na utendaji.

Soma Zaidi...
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa

Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.

Soma Zaidi...