Haki na wajibu kwa mayatima

Haki na wajibu kwa mayatima

Wajibu kwa Mayatima



Yatima ni mtoto aliyefiwa na wazazi wake, hasa baba, kabla ya kufikia baleghe. Uislamu unatuhimiza kuwatendea wema yatima na kuwatunzia urithi wao kwa uadilifu mpaka wafikie baleghe yao na kuwa na akili ya kutunza mali.


"... Na wanakuulizajuu ya mayatima: Sema: Kuwatendea mema ndivyo vizuri. Na kama mkichanganyika nao (ndivyo vyema vile vile) ,kwani ni ndugu zenu..." (2:220)
Tunajifunza kutokana na aya hii kuwa tunatakiwa tuwatendee wema mayatima na tuishi nao katika familia kama tunavyoishi na watoto wetu. Kukaa nao pamoja kwa huruma na mapenzi kutawafariji na kuziba pengo Ia kufiwa na mzazi au wazazi wao. Si katika mwenendo wa Kiislamu kuwatenga mayatima kwenye makazi maalumu. Tuishi nao katika familia zetu na tuwasomeshe katika shule wanazosoma watoto wetu.



Kuwanyanyasa mayatima ni katika madhambi makubwa mbele ya Allah (s.w). Si muumini wa kweli yule anayemnyanyasa yatima kama tunavyojifunza katika Qur-an:


".Je, umemuona yule anayekadhibisha dini (asiyeamini malipo ya akhera)? Huyo ni yule anayemsukuma (anayemnyanyasa) yatima." (107:1-2)



Msisitizo wa kuwatendea wema mayatima pia tunaupata katika hadith zifuatazo:
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Kaya (familia) bora kuliko zote ni ile ambamo anatendewa wema yatima; na kaya mbovu kuliko zote ni ile ambamo ananyanyaswa yatima." (Ibn Majah)



Sahl bin Sa 'ad (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 'Mimi na yule anayemlea yatima (kwa wema), akiwa wa kwake au kwa wengine, tutakuwa naye peponi kama hivi - akionyesha kidole cha mwanzo (cha shahada) na kinachofuatia (cha kati) huku vikiwa vimeshikamana bila ya kuachana mwanya wowote ". (Bukhari)
Kuwatendea wema mayatima ni pamoja na kuwatunzia mali zao za urithi kwa uadilifu kama inavyosisitizwa katika Qur-an:


"Na wapeni mayatima mali zao. Wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika (yote) hayo nijukumu kubwa." (4:2)



Na wajaribuni mayatima (wanapokuwa karibu ya kubaleghe kama wataweza kutumia fedha zao vizuri wakati watakapobaleghe. Wajaribuni kidogo kidogo) mpaka wafike wakati wa kuoa (kubaleghe). Kama mkiwaona wana akili njema, wapeni mali zao. Wala msizile kwa fujo na kwa haraka ya kwamba watakua (wazitake; hebu tuzile upesi). Na mwenye kuwa tajiri basi ajiepushe (na kuchukua ujira katika kuwafanyia kazi zao). Na atakayekuwa mhitaji basi ale kwa namna inayokubaliwa na Sharia. Na mtakapowapa mali zao, basi wawekeeni mashahidi (/uu ya kuwa Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi. (4:6)


Hakika wale ambao wanakula mali ya mayatima kwa dhuluma, bila shaka wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika huo Moto (wa Jahannam) uwakao. (4:10)
Kutokana na aya hizi tunahimizwa kutunza mali za mayatima mpaka watakapofikia umri stahiki ndio tuwakabidhi. Kama tuna uwezo tusitumie chochote kutokana na mali hiyo katika kuwalea. Kama hatuna uwezo tunaruhusiwa tuitumie katika kuwapa mahitaji ya lazima kama vile Elimu, mavazi, n.k; lakini vile vile kwa tahadhari na ungalifu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1340

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sunnah za swaumu, sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani

Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.

Soma Zaidi...
Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.

Soma Zaidi...
Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu

Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia na kupunguza zinaa katika jamii

(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.

Soma Zaidi...