HADITHI ILIYOSIMULIWQ NA MLEVI MBELE YA SULTANI


image


Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi iliyosimuliwa na mlevi mbele ya sultan


HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MLEVI MBELE YA SULTANI

Tambua ewe Sultani muadilifu wa Baghdad mwa na wa Rashidi utambulikae kwa Harun, tambua kuwa mimi ni mzaliwa wa Misri na huku nimefika tu kwa sababu za utafutaji wa riziki. Baba yangu alikuwa ni mfanyabishara mzkubwa sana huko misri. Alijulikana sana katika miji na hata viji na nchi za majirani ya misri. Nilikuwa nikishiriki biashara na baba yangu toka nilipokuwa mdogo.

 

Hatimaye Mwenyezi Mungu akamchukuwa baba yangu na hapo mimi nikarithi kazi ya baba. Katika familia nipo peke yangu na mama yangu alishafariki zamani sana nikiwa mdogo. Nilifanyabiashara misri. Biashara yangu kuu ilikuwa ni kuuza kanzu. Nilikuwa nikizipaka manukato mazuri hata zikawa zikinukia sana na kumvutia mpita njia.

 

Watu walipenda sana biashara yangu na jina langu lilikuwa hata kumzidi baba yangu. Ila katu sikuweza kusafiri kibiashara kama alivyokuwa akifanya baba yangu. Niliweza kutengeneza chaneli za kibiashara wakawa wafanyabiashara wadogowadogo wanachukuwa mzugo kutoka kwangu. Kwa hakika biashara ya kanzu ilikuwa ikinilipa vyema. Kipindi chote hiki sikuwa mwenye kuoa.

 

Ilitokea siku moja akaja mtu mmoja na kuulizia bei ya kanzu. Badala ya kumtajia akanipatia kiasi kikubwa cha fedha na kunieleza nimpelekee mzigo wake sehemu ambayo alinitajia. Haikuwa ni kazi nzito kwani ni katika majukumu ya kazi yangu. Nilipomaliza maandalizi nikampelekea mzigo wake. Alipouona akanieleza kuwa nimuuzie mzigo ule pale kwake na faida yeyote nitakayoipata tutagawana.

 

Kwa uchu wangu wa pesa nikakubali. Yule bwana akaniaga safari ila akanieleza nimtunzie pesa yake mpaka atakapo rejea. Mambo yakawa hivyo nilimaliza kuuza mzigo na nilipata faida kubwa sana. Yule bwana baada ya mwezi akaja na kuniulizia pesa yake. Nikamueleza kuwa ipo salama. Basi akanieleza nimtunzie hadi atakaporudi tena.

 

Baada ya mwezi akarejea, na kuniambia kuwa ana shughuli nyingi, baada ya kumaliza atakuja kuchuuwa pesa yake. Alipoondoka akakaa kiasi cha mwezi. Hata aliporudi alikuwa mapendeza sana. Alifaa nguo nadhifu na za kupendeza.. alipokuja akanieleza ataondoka tena ila akirudi atachukuwa pesa yake. Mimi nikajiapiza kuwa pindi akija nitamkirimu kama mgeni wa heshma.

 

Safari hii alikaa kama mwaka hivi na aliporudi akaulizia pesa yake nikamueleza kuwa ipo salama. Basi nikamuomba awe mgeni wangu kwa siku ile na akakubali kwa sharti kuwa matumizi nitakayotumia yasiwe katika ile pesa yake. Nikakubali, baada ya muda kikaletwa chakula safi sana. Nikamnawisha kisha akanawa mgono wa kushoto. Nilistaajabu sana. Apilpoanza kula akala kwa mkono wa kushoto.

 

Nilistaajabu sana kwa mtu mtanashati na msafi kama huyu alafua anakula kwa shoto. Tulipomaliza kula akanywa maji kw ashoto. Basi baada ya chakula tukaanza kuzimulia za hapa na pale. Ndipo nikamuulza anitoe mashaka kuhusu kula kwake kwa shoto. Huenda ana ugonjwa ama ameumia ama anafanya masifa. Ndipo akatoa mkono wake. Looo! Mkoni wake ni kugupu aani ni kiwete ana mkono lakini kiganja kimekatwa.

 

Baada ya hapo akanieleza kuwa si kama ametaka kula na kushoto ila kuna sababu ilopelekea hali hiyo. Basi kwa udadisi niauiza kuhusu chanzo bila kusita ndipo akaanza kuzimulia hadithi yake na kukatwa kwa mkono wae:-



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    6 Maktaba ya vitabu    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hatma ya kinyozi maishani mwangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hadithi iliyosimuliwa na tabibu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Historia ya zamani
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image WAKATI WA KUFUMBUKA
Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha. Soma Zaidi...

image Nani muuaji?
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu muuaji wa mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

image Safari ya kwanza ya sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Hadithi ya mvuvi na jini
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu. Soma Zaidi...