image

Hadithi ya Kaka wa sita wa kinyozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

HADITHI YA KAKA WA SITA WA KINYOZI

Kaka yangu wa sita amekatwa mdomo wa chini. Nitakusimulia kisa hiki kwa ufasaha na kwa ufupi. Habari ni kuwa kaka yangu wa sita hakuwa ni mtafutaji sana wa mali ila alikuwa ni mcheshi na mpenda utani sana. Alikuwa na hali ya kipato cha chini na ilitokeaga siku nyingine anakosa hata cha kukila. Kaka yangu wa sita naye ni kama wenzie hakuwa na mke wala mtoto na hakupatapo kuoa. Hakuwa na makazi ya kudumu kwamuda mrefu hivyo alizoea sana kutanga tanga. Jambo ambalo lilikuwa linampatia sifa kaka yangu huyu ni kuwa alikuwa ni kijana mwenye sura nzuri. Alikuwa akipendwa sana na wabinti na hata wake za watu. Nadhani hali hii ndiyo iliyomfanya asiwe na makazi maalumu ili kuepuka mitihani na wake za watu na watoto za watu.

 

Ilitokea siku moja kaka hakupata kula toka asubuhi mpaka mwishoni mwa mchana. Katika hali hiyo hakupatapo kutia kitu mdomoni iwe kinywaji ama chakula. Katika hali kama hiyo kaka alidhoofu sana kwa ghafla ndani ya siku moja tu. Katika kutembea kaka akafika kwenye nyumba moja pembeni kidogo na mji. Kaka alikwenda kuomba walau apate hata tunda moja la kufunguwa kinywa chake. Alikuatana na mlinzi wa geti. Kaka akaeleza shida yake kwa mlinzo aliyeonekana mwenye busara sana na mwenye huruma. Mlinzi alimueleza kuwa aingie ndani na atakutana na mwenye nyumba.

 

Kaka akaingia ndani, huko akakutana na bostani kubwa na la kifahari. Matunda yaliyowiva yalikuwa yakining’inia kama taa za fanusi zilizotengenezwa Misri. Maembe machungwa na midizi iliyopangiliwa kwa mistari kwa pamoja ilipendeza vyema. Kaka njaa ndio ilizidi baada ya kuona minanasi iliyokatika sura njema. Kaka hakujuwa ni wapi atamuona mwenye nyumba. Aliendelea mbele huku akiona vitu vizuri na vya kupendeza. Hatimaye alianza kuona kiti kizuri chenye miguu ya kumeremeta. Mzee wa makamo alikuwa akisoma kitabu kikubwa sana. “Asalaamu Alykum” “waalykumsalaam habari yako kijana” “Nzuri tuu” yalikuwa ni salamu kati ya kaka na mzee wa makamo.

 

Baada ya salamu kaka akaeleza shida yake. Mzee alionekana kufurahi sana na alionyesha tabasamu la udadisi. Mzee akamchukuwa kaka hadi kwenye baraza ya nyumba na kukete wakiwa wanaangaliana. Mzee naye akasema kuwa hata yeye ana njaa sana. Alikuwa akisubiri mtu wa kukaa na kula naye, kwani yeye hakuzoea kula akiwa pekeyake hata siku moja. Kaka alifurahi na kuona kuwa nitakula na mwenye nyumba kubwa na ya kifahari. Bila shaka aliamini kuwa leo atakula vitu vya utamu sana.

 

Mzee akaagiza vijana wake walete viliwa. Mmoja akaleta birika la kunawia maji. Cha kushangaza birika lilikuwa tupu, na katika hali hiyo akafanya kama anamnawisha mzee na mzee akafanya kama ndio ananawa. Alipomaliza kunawa alifanya kama anakung’uta mikono. Ukweli ni kuwa hakuna alichonawa ila ilikuwa tu ni utani. Mzee huyu alizijuwa vyema sifa za kaka kuwa anapenda utani. Lakini leo kaka mpenda utani ana njaa sana. Na anafanyiwa utani kwenye chakula. Leo uvumilivu wa kaka unakwenda kupimwa. Baada ya kijakazi kumnawisha mzee alienda kwa kaka naye akafanya vile vile kama anamtirizia maji. Kaka naye akafanya kama mzee vile ananawa kisha akakung’uta mikono yake. Kijakazi akaondoka.

 

Kijakazi mwingine akaja, mzee akamwambia tuwekee nyama ya kuoka na mikate pamoja na mchuzi wa kuchovyea. Kijakazi akafanya kama anatenga. Alipomaliza akaondoka. Ukweli ni kuwa alitenga hewa tu. Mzee akamwambia kaka waanze kula. Mzee akajifanya kama anakata kipande cha nyama huku anaminyana kwa taabu. Akamwambia kaka akamate kipande kile wavutiane. Kaka akafanya kama anakamata kipande kisha kikakatika na wakaendelea kula. Hapa walikuwa hawalikiuhalisia ila kila kitu kilikuwa ni hisia tu. Kaka akagunduwa kuwa stiki za kuchokole meno hazipo. Hapo akajifanya kana kwamba nyama imemkwama kwenye meno yake.

 

Mzee akamuita kijakazi alete stiki, punde ikaletwa na kaka akaanza kuchokowa meno. Kisha akaendele akula kawaida. Nmzee alikuwa akionyesha tabasamu la udadisi muda wote. Kaka akajifanya anakula kwa pupa maana ana njaa sana. Haukupita muda kaka ndipo akapaliwa na kipande cha mkate. Mzee kwa shauku akamkamata kaka na kuktia ngumi mgongoni, ngumu iliyoingia vyema mgomgoni mwa kaka aliyekuwa ana njaa kali sana. Kaka alikasirika sana na alitamani amrudishie ila alivumilia. Kaka akasema kimoyoni huyu mzee nitamlipa masikhara yake leoleo hii na atajuta kufanya utani na mimi.

 

Mzee akajifanya ameshiba hivyo akaagiza vinywaji viletwe. Kaka alitaka aletewe mvinyo uliotemgenezwa kutoka nchi ya uhabeshi. Mzee akaagiza mvinjo wa tende na zabibu. Wote kwa pamoja waliagiza kwa sauti. Punde kijakazi akafanya kama anatenge bilauri na birika mbili akaweka mbele yao ili waweze kujitilia wenyewe. Ukweli ni kuwa kaka alikuwa na njaa sana lakini alijitahidi kuvumulia yote haya huku akitafuta nafasi ya kulipa huu utani. Nafasi aliyoitafuta kaka sasa ndipo imepatikana maana sasa ameanza kujifanya amelewa.

 

Katika hali kama hiyo mvinyo wa kihabeshi ulionekana mkali sana. Sasa kaka amelewa na ameanza kutapika. Akajifanya amemtapikia mzee. Na mzee akajifanya kama anafuta matapishi kwenye kanzu yake. Haukupita muda kaka akamtandika kofi kubwa mzee kwenye shingo. Akamuongeza tena kwenye uso, hadi mzee akaona nyotanyota. Mzee tabasamu likaondoka na akahamaki na kuuliza mbna unaniadhibu? Kaka alifurahi baada ya kuvunja utani wa mzee. Kaka ndipo akajifanya anaongea kwa kulewa, na kumwambia mzee “unataka lingine, wanasema kofi na mlevi zito, na kulewa huku niliko nako nataka nikuongeze lingine”. hapo mzee akacheka sana na kutamka “umeshinda kijana”.

 

Kumbe muda wote mzee alikuwa anamjaribu kaka na sasa kaka ameshinda majaribu. Mzee akajitambulisha vyema kwa kaka, na kaka akjitambulisha. Japo mzee alikuw akimfahamu kaka, maana mzee alikuwa ni rafiki na baba. Baada ya hapo mzee akaagiza chakula cha ukweli kiletwe, na hapo ilikuwa ni kula na kunywa kiukweli. Baada ya hapo mzee alimtaka kaka waishi pale kwa pamoja. Waliishi pamoja kwa muda wa miaka 20, kisha mzee akafariki. Ndugu za mzee wakazichukuwa mali zote na kaka wakamuhisabu kuwa ni mtumwa wa mzee na wakamuuza kwenye biashara za utumwa.

 

Kaka alinunuliwa na mzee mmoja hivi. Kwa kuwa kaka alikuwa na sura nzuri, mke wa mzee alikuwa akimtamani kaka. Siku moja walikutwa wakiwa wamekee kwa pamoja kwa ukaribu sana. Mzee alikasirika na kumkata kaka mdomo, akamtandika na kwenda kumtupa mbali maeneo ya milimani. Wapitanjia walimuokota kaka na kumtibu kumpatia mavazi na chakula. Nilipozipata habari hizi nilikwenda kumtafuta kaka na kumchukuwa.

 

Baada ya kumaliza masimulizi haya haya ya kaka sita pamoja na yeye mwenyewe mkinyozi akamueleza kadhi je umeamini kuwa mimi si mtu wa maneno mengi, bali nazungumza ukweli?. kadhi alifurahi sana na kuniruhusu niondoke pale. Kisha kinyozi akaendelea kusema kuwa katika pirika pirika ndipo nikakutana na baba wa huyu kijana wakati huo kijana huyu akiwa ni mdogo. Niliweza kuishi na baba wa huyu kijana kwa muda mrefu, na kabla ya kufariki alinitaka niendelee kumlinda kijana wake. Niliendelea kufanya hivi kwa siri kwa muda mrefu. Hivyo sikuwa nikimtakia maomvu huyu kijana kama yeye alivyofikiria.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1188


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kukatwa mkono na kuurithi utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Utajiri wa baba na kifo chake
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Upendo uliotafsiriwa kwa michoro
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Hadithi ya aliyekatwa vidole gumba
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa tano wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

HADITHI YA ALADINI NA TAA YA MSHUMAA WA AJABU
Soma Zaidi...

Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Nani muuaji?
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu muuaji wa mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

Hatma ya kijana mchonganishi
Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi mwenyewe
Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa sita wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Mshenga wa aladini mbele ya mfalme
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...