Hadithi ya Kaka wa tatu wa kinyozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

HADITHI YA KAKA WA TATU WA KINYOZI

Kaka yangu wa pili alikuwa ni kipofu. Alipata upofu badala ya kupata ajali katika shughuli zake za kutafuta mali. Baada ya kupata upofu alikuwa akijipatia pesa kwa kuombaomba kutoka kwa watu. Kaka hakuwa na mke wala watotot. Ilitokea siku moja katika kuombaomba kwake alifika kwenye nyumba moja. Akagonga mwenyenyumba alipouliza kaka hakujibu kitu. Lengo lake ilikuwa mpaka ajemwenyeyumba ili atakapomuona ataweza kumsaidia. Kwa mara ya pili mwenyenyumba akauliza “wewe nani na unataka nini?”/ kaka hakujibu kitu hata akauliza kwa mara ya tatu bila ya majibu tena.

 

Mwenyenyumba alikasirika na akatoka kuja mlangoni. Alipofika mlangoni akamkuta kaka. Kaka akamweleza kuwa anahitaji msaada japo wa chakula ama pesa. Kwa hasira mwenyenyumba akamwambia nifate. Kaka akamfuata kwa kumshika kipande cha kanzu yake. Wakiwa wanapanda ngazi za gorofa kaka aligundua kuwa walikufika hadi gorofa la nne. Juu kileleni mwenyenyumba akamwambia kaka “umesema unahitaji nini” kaka akajibu “msaada, wa kifedha ama chakula”. mwenyenyumbq akajibu “ruka chini hapo msaada upo huko mbele” kaka akagunduwa kuwa endapo ataongeza hatua mbili mbele ataangukia chini. “kama hutaki kunisaidia si ungenieleza tu toka mwanzo” “nilipouliza nani aliyekuwepo mlangoni na nini unataka haukunijibu” yalikuwa ni maneno ya kaka na mwenyenyumba.

 

Kaka akagunduwa kuwa endapo ataendelea kupoteza muda anaweza kuuwawa ama kupata madhara zaidi. Kaka akashuka kwa haraka huku anahisabu vingazi alipokazibia chini kwa bahati mbaya alianguka na kuumia vibaya. Kaka akaelekea asikokujuwa akiwa anaugumia maumivu ya mguu. Katika kutembea huku na kule alikutana na vipofu wengine wawili. Kwa kuwa nao walikuwa hawakujui wendako wakaungana na kutengeneza mstari mmoja wa vipofu. Wakiwa wanatembetembea wakafika kwenye kajumba kamoja wakakaa. Wakiwa wamepumzika ghafla wakasikia sauti za watu zinawakaribia.

 

Kaka akashauri wenzie wazunguke nyuma ya nyumba wajifiche wasije onekana. Wakazunguka nyuma kimyamkimya, na baada ya muda wale watu wakaingia kwenye kijumba kile na kuakuzungumza. Katika mazungumzo ya watu wale kaka aligunduwa kuwa walikuwa ni wezi na pale walikuja kuficha pesa walizoiba. Walipatana warudi pale baada ya wiki moja huku wakisubiria mtaani kutulitulia. Waliziweka pesa zao kwenye moja ya sanduku la mbao lililopo pale ndani. Kisha wakaondoka zao.

 

Kaka na wenzie walikaa kule nyuma ya kijumba kile, kisha walipojiridhisha kuwa wale watu hawapo tena walirudi walipokuwa mwanzo. Wakajadiliana na kukubaliana kuwa wazitfute zile pesa na wagawane. Wakaingia ndani na kuzitafuta. Baada ya muda wakafanikiwa kuzipata. Loo ilikuwa ni viande 3000 vya dhahabu na 200 vya silva. Wakakubaliana kugawana kiasi kile cha pesa. Wakati wapo katika harakati za kugawana kaka aligunduwa kuwa kuna mgeni kati yao. Kaka akawaambia wenzake “mbona kuna mtu mwingine kati yetu”. Wakaanza kuchunguza wakamgundua mtu wa nne.

 

Wakamkamata na kuanza kumshambulia kwa kumpiga. Kaka akachukuwa zile pesa na kuzificha tena. Kakana wenzake wakamburuza yule mwingine hadi mbali kidogo na lile eneo a kuanza kumshambulia tena. Haukupita muda watu wakaanza kujaa. Yule mtu mwingine akajichokowa kwenye macho na kuwa kama kipofu. Kisha akaanza kuguta kelele “jamani naombeni msaada, hawa wenzangu wananionea na kunidhulumu, naombeni msaada”. watu wakaona wawapeleke wote kwa kadhi apate kutoa hukumu kati yao.

 

Kadhi alipouliza hasa kilichotokea yue mtu akasema “kadhi niadhibu kwanza kisha nitakueleza kila kitu” basi kadha akaamrisha apingwe viboko 25. kisha akaanza kueleza “sisi unaotuona hapa wote si vipofu. Tumeigiza kuwa vipofu ili tupate kuwaibia watu na kuapata msaada wa bure kifedaha. Na kwa kutumia njia hii tumenufaika vyema” kisha akafumbuwa macho yake Loo!! hakuwa kipofu hata kidogo kisha akaendelea kusema “leo tulipata pesa vipande 300 vya dhahabu na 200 vya silva. Lakini tulipokuwa tunagawana wenzangu wakanidhulumu wakati mimi ndiye niliyepata pesa hiyo. Ninakuomba uwaadhibu vikali ili wafunguwe macho yao, na waseme ukweli”.

 

Basi kaka na wenzake wakaanza kuadthibiwa kwa mijeledi . walichapwa viboko 25, waliposhindwa kufungua macho yao wakaongezwa viboko 25 hata wakashindwa kukaa wala kuzungumza. Kisha wakamuelekea yule mtu wakambana vyema aeleze ukweli vinginevyo ataadhibiwa tena. Ndipo akaanza kutaja kuwa pesa zimefichwa sehem flani, na kama kadhi ataahidi kuwa naye atapewa shea atawaonyesha mahali pesa ilipofichwa. Pia aliongezea kwa kusema “hawa hawatafumbua macho kwa hofu, hivyo kuthibitisha utapeli wetu na wao na kutaka kunidhulumu kwao nitakwenda kuonyesha mahali esa ilipo”.

 

Kadhi akachaguwa kundi la askari limfate. Akaenda nao mpaka kwenye kale kajumba na kuzitowa zile pesa. Kadhi akampatia yule mtu fungu lake na zilizobakia zikawekwa kwenye hazina ya nchi. Kaka na wenzake wakafukuzwa mjini na hawakutakiwa kuonekana tena. Mimi nilipopata habari hizi nikaenda kumchukuwa kaka kwa siri. Mpaka kufikia hapa kinyozi akamaliza stori ya kaka wake wa tatu. Kisha akaendelea kuhadithia kilichompata kaka wa nne kama ifuatavyo:-



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-08     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1219


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya tunda la tufaha (epo)
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kwanini vidole gumba vilikatwa
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa y Soma Zaidi...

Safari ya tano ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Deni la mapenzi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Kiapo cha sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Safari saba za sinbad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hatma ya kinyozi maishani mwangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma. Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Matibabu ya vidonda sugu
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya vidonda vya tumbo sugu Soma Zaidi...

Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini. Soma Zaidi...