HADITHI YA MJI ULIOGEUZWA MAWE


image


Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela


HDITHI YA MJI ULOGEUZWA MAWE.

Mimi ni mtoto wa mfalme wa nchi hii ambayo umemuona amegeuzwa jiwe kama watu wengine. Nilipokuwa mdogo nilikuwa nikilelewa na bibi mmoja laiyekuwa ni muiislamu. Watu wa mji huu walikuwa wanaabudu masanamu hivyo bib i yule alifanya siri imani yake. Na kwa usiri huo akanifundisha imani ya uislamu juu ya mungu mmoja na akanifundisha kusoma Qurani. Katika muda wote niloishi nae yapata miaka 10 alikuwa akinisisitiza kufanya siri imani ile na mambo yakawa hivyo mpaka bibi yule alipofariki.

 

Mwaka juzi alikuja mtu mmoja hapa nchini kwetu, mtu huyu ulikuwa ikilingania watu kuhusu kumuabudu mola mmoja tofauti na watu walivyozoea. Mfalme aliongea maneno ya ajabu na ya kipuuzi kuhusu sauti ile. Mtu yule aliondoka na akarudi tena mwaka jana na maneno yalikuwa ni yalelyale. Na mfalme yaani baba yangu alirudia maneno yaleyale. Na mara ya tatu mwaka huu alirudi tena Mtu yule na mambo yakawa vile vile.

 

Wiki mbili baada ya kuondoka kwa Mtu yule ikatokea sauti ikionya na kulingania juu ya imani ya munngu mmoja. Hali ikawa kama mwanzo Mfalme wetu akatoa kejeli na maneno machafu sana. Kwa hakika niliumia na nikataka kwenda kumtia adabu baba yangu mwenyewe lakini nilishindwa kufanya hivyo. Machozi yalinitoka na nisijuwe jambo la kufanya na hakina wa kunishauri. Basi haikupita muda mrefu ile sauti ikatoweka na hapo anga ikafunga kuwa nyeusi kutokana na wingu lisilojuliukana kama la mvua au upepo mkali.

 

Wingu lile liliendelea kusogea chini hata likakaribia kufunika nyumba. Ulikuwa ni wakati wa muda wa swala ya adhuhuri na watu wamechanganyika katika utaftaji. Wengine wapo masokoni na wengine mashambani na hali kadhalika. Wingu lile likaambatana na upepo mlaini ambao haukuweza kuharibu hata kipande cha nguo kilichokuwa kinaning’inia. Upepo ule uliingia masikion, puani na kila sehemu yenye tundu na kutokea upande mwingine.

 

Haukupita muda wat wote wakawa katika hali uloiona kuwa mawe. Na kia mtu vile alivyo ndivyo alivyobaki. Hata walokuwa wamelalaq wamebakia mawe kwenye vitanda. Nilitoka kuchunguza zaidi sikuona hata mnyama ambaye aligeuzwa jiwe. Kwa hakika msiba huu uliwapata wanadamu tuu. Basi nikawa sina pa kwenda hiyo nikabakia kisiwani hapa peke yangu kama unavyonioa. Na hii ndiyo historia ya kisiwa hiki kilichogeuzwa mawe.

 

Wakati kijana anamaliza kusimulia hadithi ile Zubeida akawa analia na machozi yanamtiririka kama chemchem iliyoanzia mlimani. Basi kijana kwa huruma akawa anamfuta machozzi Zubeida. Baada ya muda Zubeida akauliza “sasa wanyama walikwenda wapi?” kijana akamjibu baada ya kutokea yaliyokwisha tokea ilikuja tena ile sauti na kuniambia kuhusu hatima ya wanyama. “ama kuhusu wanyama amri yao ipo kwako, eidha utawatumia kama chakula chako mpaka Allah atakapoleta nusra , ama awahamishe awapeleke anakotaka ama wageuzwe kuwa vitu vya thamani na iwe kama zawadi ya Zubeida mwenye kupotea njia mwana wa tairi na msalitiwa na ndugu zake.

 

Basi nikachaguwa jambo la tatu, na pindi ulivyokuja nilifahamu hakika ni wewe Zubeidah. Zubeida akamuuliza “ni kitu gani kilichokufahamisha” akaendelea ile sauti niliiulisa sasa ni kwa namna gani nitamfahamu Zubeidah ikajibu siku moja kabla ya kuja kwa Zubeiday bahari itakuwa chafu sana na upepo maini utaingia kisiwani hapa na kusafisha nyia ya Zubeida mwana wa tajiri, msalitiwa. Hivyo Zubeida atakuwa hana jinsi ila atakufikia tu popote utakapokuwepo muda huo. Basi nilipoziona ishara hizo nilifahamu ujio wako hivyo ili kukurahisishia kunipata nikawa nasoma Qurani kwa sauti ya juu ndivyo ukanisikia.

 

Ama kuhusu kusalitiwa kwa Zubeida na ndugu zake nilishindwa kujuwa mengi zaidi maana sauti ile ikanambia hainipasi kujuwa siri za mambo yajayo. Halikadhalika ninachofahamu zaidi kuhusu huo usaliti ni kuwa maisha yangu ama yako yatakuwa hatarini. Basi Zubeida na yule kijana wakatoka pale na Zubeidah akashauri waoane na wakakubaliana kufunga ndoa punde watakapofika nyumbani.

 

Basi kijana akampeleka Zubeidah kwenye zawadi yake na akakuta mali nyingi sana na tayari imeshafungwa vizuri kwenye mkokoteni. Basi wakaburuza mkokoteni wao mpaka kwenye chombo chao na kuuingiza ndani. Wakawa wanapunga upepo ufukweni na kubadilishana mawazo na kuchat. Wakiwa katika hali hiyo ghafla akatokea nge anakimbizwa na kunguru Zubeidah akachukuwa kijiwe na kumpiga kunguru na ukawa ndio mwisho wa maisha ya kunguru yule na nge akatokomea kwenye mawe. Na wawili hawa wakaendelea kuzungumza. Wakati yote haya yanafanyika dada zake na Zubeidah walikuwa wakiona wivu na kijicho kwa mafanikio ya ndugu yao.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    4 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    5 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    6 Madrasa kiganjani    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sita
Post hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sehemu ya sita.sehemu hii inaonyesha jinsi bibi alivyo ndumila kuwili na hapendi kuonekana mbaya. Soma Zaidi...

image SAFARI YA MUUJIZA
Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama. Soma Zaidi...

image Hadithi ya jini na mfanya biashara
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Utajiri wa baba na kifo chake
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi ya binti wa kwanza na mbwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image NIMLAUMU NANI (sehemu ya sita)
Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank Soma Zaidi...

image Kwanini dirisha moja?
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Kila kitu ambacho wanaume wanatakiwa kufahamu kuhusu wanawake.
Hii ni siri kubwa kuhusu wanawake. Hapa utajifunza jinsi ya kumfanya mwanamke asikuache. Soma Zaidi...