Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

HAKI 5 ZA MUISLAMU ANAZOPASA KUPEWA: 

 
وعن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال‏:‏ ‏"‏حق المسلم علي المسلم خمس‏:‏ رد السلام، وعيادة المريض، واتباع الجنائز، وإجابة الدعوة، وتشميت العاطس” ‏(‏‏(‏متفق عليه‏)‏‏)
 
 
 
Imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurairah kuwa Mtume s.a.w amesema : "Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe ni tano: kurudisha salamu, kumuangalia anapoumwa, kuifuata jeneza lake, kuitikia wito anapokuita, na kumuombea dua anapopiga chafya". 
 
 
Maelezo
Kwa mujibu wa hadithi haki hizo ni; -
1. Kujibu salamu ya Muislamu anapokusalimia. Hii inamaana kujibu salamu ni jambo la lazima. Endapo hutajibu salamu baada ya kusalimiana utakuwa umevunja haki hivyo utaingia kwenye makosa. 
 
 
2. Kwenda kumangalia anapoumwa. Nibsunnah kumuombea dua mgonjwa. Unapomuangalia mgonjwa unafaidika wewe na yeye kiroho na kiafya pia. 
 
 
3. Endapo atafariki ni haki yake kumsindikiza kwa kilifuata jeneza lake hadi kwenda kumzika. Hii inaambatana na kumswalia. Hata hivyo sio lazima kwako endapo wapo walioshiriki kumswalia. Hata hivyo kama huna uhuru ni haki yake umshindikize mpaka atakapozikwa. 
 
4. Endapo muislamu mwenzio atakuita ni haki yake kuitikie wito huo. Nenda kwanza kasikilize anakuitia nini,  kisha kukubali na kukataa hupatikana baada ya kujuwa wito ulikuwa na sababu gani. 
 
Hata hivyo haki hii inatakiwa ifanyike kwenye misingi ya sheria. Sio sawa kumuita mwanamke katika mazingiravtatnishi.  Ama hata mwanaume kumuita mwanaume kwenye mazingira hatari. Hivyo kwa kuangalia usalama wako pia haki hii inapaswa kutekelezwa katika misingi salama. 
 
 
5. Kumuombea dua anapopiga chafya. Endapo atapiga chafya na akasema alhamdu lillah wewe unatakiwa umwambie yarhamuka llahu. Kisha yeye anatakiwa ajibu yahdikumullahu wayuswlih baalakum. 
 
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1335

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Matendo ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu

Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...
NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa zakat al fitiri na umuhimu wa zakat al fitri kwa waislamu

Hapa utajifunza kuhusu zakat al fitiri, kiwango chake, watu wanaostahili kupewa na kutoa, pia umuhimu wake katika jamii.

Soma Zaidi...
Kutoa kati kwa kati

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa swala

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...