Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani.

Hasara za wivu na kutokuwa wazi.

1. Mama Lisa akiwa amepanic vibaya na wasiwasi mkubwa aliingia kwa mama lita akiwa anaita lita ,lita, yaani kwa nguvu sana na kuhamaki, ndipo mama lita akashutuka sana na kumuuliza Mama Lisa kinachoendelea, ndipo Mama Lisa akaangua kilio na kugala gala kwenye sakafu baadae mama lita aka mpoza na kumuuliza kinachoendelea ndipo akaeleza kila kitu akidai kwamba Lita anajua kila kitu kinachoendelea shule na hajatoa taarifa yoyote kwa Mama yake, ndipo lita akaitwa akaulizwa akajibu kwamba hajui kitu chochote na kudai kwamba Lisa huwa anasoma na hajui kinachoendelea.

 

 

 

 

 

2. Hapo mama Lisa akapoa akarudi kwake, kumbe Lisa alikuwa tayari yupo kwao na lita na alisikia kila kitu akamshukuru sana lita, basi mama yake Lisa alipotaka kwenda nyumbani naye Lisa akakimbia akawahi kabla mama yake hajafika nyumbani na akalala kitandani kama vile anaumwa, basi mama Lisa akaenda nyumbani akamkuta mwanae yuko kitandani analalamika kwamba akija kusoma kichwa kinauma ,na akifanikiwa kusoma kuna vitu vinakuwa vinapiga kelele kichwani mwake na akamwambia mama yake kwamba hali hii ilijitokeza mda kwa hiyo nilishindwa kukwambia kwani nilitaka usiumie mama yangu kipenzi.

 

 

 

 

3. Basi mama Lisa akafanana kama vile amechanganyikiwa na akatafuta cha kufanya ili kuweza kumwokoa mtoto wake ili aweze kusoma vizuri kabisa, kwa sababu mama Lisa alimzaa Lisa kwa mwanaume ambaye alikuwa na familia yake tayari kwa hiyo aliamua kumwambia baba yake, na baba yake alikuwa anampenda sana Lisa kwa sababu ndiye aliyekuwa msichana pekee na waliobaki walikuwa ni wavulana, kwa sababu baba yake na Lisa alikuwa hajamtambulisha Lisa kwa mke wake wa ndoa alitamani kumwambia ili aweze kumwokoa mtoto wake, lengo la baba lilikuwa na kuishi na Lisa kwa mda ili aweze kumsaidia.

 

 

 

 

 

4. Basi baba Lisa akatoa siku moja akamwambia mke wake waende mjini na watarudi jion, basi akampeleka mjini akamwambia achukue kila kitu anachokihitaji na yule mama akafurahi sana kusikia vile basi kama kawaida ya wanawake akabeba nguo,wigi na takataka zote kwa sababu baba Lisa alikuwa na hela kweli na aliweza kulipa kila kitu, na baada ya kumaliza shopping waliweka vitu kwenye gari na wakaenda kula na yule mama aliulizwa hoteli anayoipenda akapendekeza hoteli moja iliyoitwa Victoria hotel, wakaenda wakala na kusaza na yule mama alifurahi mno.

 

 

 

 

 

5. Basi walipokuwa wanakula na kunywa na kucheza, baba Lisa aliomba kitanda kusudi wapumzike kidogo ili baadae waende nyumbani basi wakapewa kitanda, na katika kupumzika baba Lisa akamwambia mkewe kwamba ana kitu cha kumwambia na anaomba akipokee na akimsaidia atampenda maisha yake yote na yule mama kwa sababu alikuwa na furaha akamwambia yuko tayari kumsaidia kwa hiyo akamwambia kwamba ana mtoto wa kike na ana matatizo anataka amlete kusudi aweze kumsaidia na baadae atarudi kwa mama yake, yule mama akasita kidogo ila kwa kuwa alikuwa ameahidi kumsaidia alikubali ila aliumia kuona mumewe ana mtoto wa kike na yeye hana na ndiyo iliyokuwa tamaa yake .

 

 

 

 

6. Basi yule mama akaanza kuhoji zaidi kama mme wake huwa anaenda kwa yule mama Lisa kwa sababu sehemu ilikuwa mbali hakuona ushaidi wowote ila baba Lisa alikuwa anaenda na kuhudumia alikuwa anamhudumia mtoto kama kawaida , ila mama yule akamwambia baba amlete yule mtoto ili wamsaidie haraka ila lengo la mama lilikuwa ni kujua mtoto yaani Lisa na mama yake wanaishi wapi, basi wanaume walivyo na akili alikwenda mwenyewe akamleta nyumbani kwake ila mama alikuwa anataka kujua wanaishi wapi, basi Lisa akaletwa pale akawa anapendwa sana na yule mama, akaanzishiwa tution akawa anasoma kama Kawaida na alipopelekwa shuleni kufanya mtihani akawa wa kwanza na baba yake akafurahi akataka kuishi naye ili atoke kwenye mazingira ya kwa mama lisa. ila yule mke wa ndoa kazi yake ni mwanasaikolojia ya watu waliohathariwa na mahusiano kwa hiyo akaanza kuhoji ili kujua tatizo ni lipi basi akapata uhakika kwamba shida ni yule mwalimu na akakaa kimya, lengo lake lilikuwa ni kuharibu kabisa maisha ya mtoto kwa hiyo akamshawishi mme wake wamrudishe mtoto kwa mama yake.

 

 

 

 

 

7. Basi yule mke wa ndoa akajifanya mwema akamsihii mmewe waende wote kwa mama Lisa badi yule mwanaume akakubali wakaenda wote wakamfungia mama Lisa zawadi nyingi pamoja na Lisa,kwa hiyo walipofika kwa mama Lisa na Lita alikuwepo alipomwona Lisa alichukia mno na kusema kwamba amerudi kuchukua nafasi yangu darasani na akasema nitamkomesha na atakuwa anafeli tu, subiri mama Lisa kusikia hivyo alichukia mno na akaanza kumchukia Lita.wale wageni walipoondoka mama yule akaomba number za simu za mama lita na mama Lisa na watu wote hapo akapewa na pia wakaondoka na mumewe na Jumatatu Lisa akarudi shule alifurahi sana kuonana na mpenzi wake na siku nzima hakwenda darasani na lita hakusema kitu nyumbani ila kumtunzia siri tu.

itaendelea baadae.

 

 

 

 

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/23/Tuesday - 08:21:04 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 638


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hadithi iliyosimuliwq na mlevi mbele ya sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi iliyosimuliwa na mlevi mbele ya sultan Soma Zaidi...

Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

HADITHI YA SIRI YA UTAJIRI WA AJABU : sehemu ya 01
huu ni ufupisho wa kisa cha utajiri wa ajabu katika kijiji fulani huko zamani za kale. Soma Zaidi...

Kukatwa mkono na kuurithi utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tano)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma. Soma Zaidi...

SAFARI YA MUUJIZA
Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama. Soma Zaidi...

Kwanini vidole gumba vilikatwa
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa y Soma Zaidi...

Siri ya wageni wale inafichuka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo no tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda,hutokea baada ya ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaitwa mucus kuharibika. Vidonda vya tumbo (peptic ulcers) imegawanyika katika ma Soma Zaidi...

Hadithi ya jini na mfanya biashara
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani. Soma Zaidi...