picha

Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.

Hatua tatu anazozipitia Mgonjwa wa tauni.

1.Hatua ya kwanza ni pale kiroboto mwenye Maambukizi ambaye ameyapata kutoka kwa panya anamngata mtu na kuingiza wadudu ambao kwa kitaalamu huitwa yersinia pestis, wadudu hao hawapiti kwenye mfumo wa mzunguko wa damu bali upitia kwenye lymphatic na kushambulia limfu node za kwenye kwapa, kwenye shingo na sehemu mbalimbali ambazo zina limfu.

 

2.Pia hizo limfu zinakuwa na Maambukizi hali ambayo ufanya hizo limfu kubwa na ma upele na na upele hayo utoa usaha ambapo Usababisha maumivu makali kwa mgonjwa kwa hiyo Dalili hii kwa watu wengine ushindwa kutambuliwa mapema kama ni tauni au nini kwa hiyo matibabu ulenga zaidi Dalili hali ambayo Usababisha kushindwa kupona na kusababisha hatua nyingine kama tutakavyoona hapo chini.

 

3.Baada ya Maambukizi kuingia kwenye node uingiliana na mzunguko wa damu hii hatua ya wadudu kuingia kwenye mzunguko wa damu kwa kitaalamu huitwa septicaemia, kwa hiyo kwenye damu wadudu ushambulia mishipa ya damu na kufanya mzunguko wa damu kuwa wa shida hali ambayo Usababisha kupasuka kwa mishipa ya damu na kusababisha kuvuja damu kila mahali.

 

4.Ugonjwa ukifikia kwenye hali hii wengine udhani kwamba ni ebola na kuanza kuwa tenga na kuwakimbia wagonjwa kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa dalili za Ugonjwa huu zinatambulika mapema na katika hatua hii matibabu yanaweza kufanya kazi.

 

5.hatua ya tatu ni pale ambapo wadudu wanasambaa kwenye mapafu ambapo kwa kitaalamu huitwa pneumonic, kwa hiyo wadudu wakizidi kwenye damu uhamia kwenye mapafu na kuweza kuyashambulia, na katika hatua hii mgonjwa anapumua vibaya vibaya na kwa hatua hii mgonjwa anaweza kuambukiza kwa hiyo ni vizuri mgonjwa akifikia hatua hii akaweza kutunzwa vizuri na sehemu yenye hewa.

 

6 . Kwatika hatua hii ni vigumu kwa mgonjwa kupona kwa sababu Maambukizi yanakuwa yamesambaa sehemu mbalimbali kwenye mwili, kwenye damu na mapafu pia na sehemu nyingine pia ushambulia kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili hizi ili kuweza kupambana na ugonjwa huu.

 

7.pia jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu Dalili za Ugonjwa huu na kuweza kutambua Dalili zake mapema ili kuweza kupata matibabu ipasavyo kwa sababu kuna dawa ambazo zinatumika dawa zenyewe ni kama ifuatavyo, dawa za antibiotics kama vile streptomycin, Tetracycline, doxycycline ambazo utumika na kuponyesha Ugonjwa huu.

 

8.Dawa hizi utumika kama ifuatavyo, kwa kuanza na streptomycin tumia milligram 30, vidonge viwili kwa siku tatu, Tetracycline tumia milligram kuanzia mia mbili hamsini mpaka mia tano mara nne kwa siku kumi, na doxycycline vinatumika kwa siku saba hizi dawa zinapaswa kutumika kwa maagizo ya wataalamu wa afya sio kutumia kiholela tu.

 

9.pia tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo na unatibika kwa hiyo mila na desturi zisizofaa tuziache ili kuweza kuokoa maisha ya watu

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1998

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Yajue maambukizi kwenye epididimisi kwa kitaalamu huitwa (Epididymitis)

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.

Soma Zaidi...
Njia za maambukizi ya Homa ya inni

Posti hii inahusu zaidi njia za maambukizi ya Homa ya inni, Homa ya inni usababishwa na virusi viitwavyo Hepatitis B, huwapata watu wote hasa wale wenye umri chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...
Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.

Post hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.

Soma Zaidi...
Kupoteza matumaini ya maisha: Jinsi ya kupata msaada.

Kupoteza matumaini ya maisha ni hali ya kihisia inayoweza kumpata mtu yeyote, ikijidhihirisha kama hali ya kukata tamaa, uchovu wa kiroho, na kuona kama hakuna njia ya kutokea katika changamoto za maisha. Makala hii inachunguza kwa kina kiini cha hali hii, hatua za vitendo za kupata msaada, na umuhimu wa kutafuta msaada wa kitaalamu. Lengo kuu ni kutoa mwanga wa matumaini kwa wale wanaopitia kipindi kigumu, ikisisitiza kuwa kupata msaada ni ishara ya ujasiri na hatua ya kwanza kuelekea kupona.

Soma Zaidi...
Dalili za macho kuwa makavu

posti hii inaelezea kuhusiana na dalilili na Mambo ya hatari ya Macho makavu  hutokea wakati machozi yako hayawezi kutoa unyevu wa kutosha kwa macho yako. Machozi yanaweza kuwa duni kwa sababu nyingi. Kwa mfano, Macho makavu  yanaweza ku

Soma Zaidi...