picha

Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.

Hatua tatu anazozipitia Mgonjwa wa tauni.

1.Hatua ya kwanza ni pale kiroboto mwenye Maambukizi ambaye ameyapata kutoka kwa panya anamngata mtu na kuingiza wadudu ambao kwa kitaalamu huitwa yersinia pestis, wadudu hao hawapiti kwenye mfumo wa mzunguko wa damu bali upitia kwenye lymphatic na kushambulia limfu node za kwenye kwapa, kwenye shingo na sehemu mbalimbali ambazo zina limfu.

 

2.Pia hizo limfu zinakuwa na Maambukizi hali ambayo ufanya hizo limfu kubwa na ma upele na na upele hayo utoa usaha ambapo Usababisha maumivu makali kwa mgonjwa kwa hiyo Dalili hii kwa watu wengine ushindwa kutambuliwa mapema kama ni tauni au nini kwa hiyo matibabu ulenga zaidi Dalili hali ambayo Usababisha kushindwa kupona na kusababisha hatua nyingine kama tutakavyoona hapo chini.

 

3.Baada ya Maambukizi kuingia kwenye node uingiliana na mzunguko wa damu hii hatua ya wadudu kuingia kwenye mzunguko wa damu kwa kitaalamu huitwa septicaemia, kwa hiyo kwenye damu wadudu ushambulia mishipa ya damu na kufanya mzunguko wa damu kuwa wa shida hali ambayo Usababisha kupasuka kwa mishipa ya damu na kusababisha kuvuja damu kila mahali.

 

4.Ugonjwa ukifikia kwenye hali hii wengine udhani kwamba ni ebola na kuanza kuwa tenga na kuwakimbia wagonjwa kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa dalili za Ugonjwa huu zinatambulika mapema na katika hatua hii matibabu yanaweza kufanya kazi.

 

5.hatua ya tatu ni pale ambapo wadudu wanasambaa kwenye mapafu ambapo kwa kitaalamu huitwa pneumonic, kwa hiyo wadudu wakizidi kwenye damu uhamia kwenye mapafu na kuweza kuyashambulia, na katika hatua hii mgonjwa anapumua vibaya vibaya na kwa hatua hii mgonjwa anaweza kuambukiza kwa hiyo ni vizuri mgonjwa akifikia hatua hii akaweza kutunzwa vizuri na sehemu yenye hewa.

 

6 . Kwatika hatua hii ni vigumu kwa mgonjwa kupona kwa sababu Maambukizi yanakuwa yamesambaa sehemu mbalimbali kwenye mwili, kwenye damu na mapafu pia na sehemu nyingine pia ushambulia kwa hiyo tunapaswa kujua Dalili hizi ili kuweza kupambana na ugonjwa huu.

 

7.pia jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu Dalili za Ugonjwa huu na kuweza kutambua Dalili zake mapema ili kuweza kupata matibabu ipasavyo kwa sababu kuna dawa ambazo zinatumika dawa zenyewe ni kama ifuatavyo, dawa za antibiotics kama vile streptomycin, Tetracycline, doxycycline ambazo utumika na kuponyesha Ugonjwa huu.

 

8.Dawa hizi utumika kama ifuatavyo, kwa kuanza na streptomycin tumia milligram 30, vidonge viwili kwa siku tatu, Tetracycline tumia milligram kuanzia mia mbili hamsini mpaka mia tano mara nne kwa siku kumi, na doxycycline vinatumika kwa siku saba hizi dawa zinapaswa kutumika kwa maagizo ya wataalamu wa afya sio kutumia kiholela tu.

 

9.pia tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu upo na unatibika kwa hiyo mila na desturi zisizofaa tuziache ili kuweza kuokoa maisha ya watu

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1973

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo.

Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo.

Soma Zaidi...
Dalili za mtoto Mwenye UTI

Posti hii inahusu zaidi dalili za mtoto Mwenye UTI,ni dalili ambazo uwapata watoto wadogo chini ya umri wa miaka mitano.

Soma Zaidi...
Sababu za mdomo kuwa mchungu

Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.

Soma Zaidi...
NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE

Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .pia  tutangalia  njia za kujikinga na  ugonjwa wa UKIMWI

Soma Zaidi...
​Kupima HIV Nyumbani

Posthii inatoa mwongozo kamili kuhusu upimaji wa HIV nyumbani. Tutachunguza umuhimu wake, jinsi ya kutumia vifaa hivyo, faida zake, na hatua za kuchukua baada ya kupata majibu, ili kukuwezesha kufanya maamuzi sahihi kuhusu afya yako kwa usiri na utulivu.

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...