image

Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu

Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha

Khutuba ya Ndoa

Kabla ya kuozesha (kufungisha ndoa), ni Sunnah kwanza kuleta khutuba ya ndoa (mawaidha ya ndoa) kwa ufupi iii kuwakumbusha wanaooana na Waislamu wengine wachunge ahadi waliyoichukua mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa watakaa kwa wema katika maisha ya ndoa na ikibidi kuachana, wataachana kwa wema vile vile.

 

Ni vyema katika mawaidha haya kuwafahamisha hawa wenye kuoana na kuwakumbusha Waislamu wote waliohudhuria kuwa maisha ya ndoa yatakuwa ya furaha na upendo endapo kila mmoja, mume na mke, atajua wajibu wake kwa mwenziwe na akawajibika kwake ipasavyo. Ndoa iliyofanikishwa kulingana na ahadi ya ndoa ni msingi wa furaha, ushirikiano, utulivu na amani katika familia na jamii kwa ujumla. Ndoa pia imekusudiwa iwaokoe wenye kuoana na adui Shetani na iwasalimishe kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa ujumla, katika khutuba hii, ni vyema umuhimu wa ndoa uelezwe kwa muhtasari.

 


Msisitizo wa Khutuba unaonekana katika hadithi zifuatazo:

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema; Ndoa yoyote ambayo ndani yake hamna Tashahhud (Maamkizi ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni kama kata isiyo na mkono. (Tirmidh).

 


Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Jambo lolote muhimu lililofanyika bila ya kumtukuza (Kumhimidi) Mwenyezi Mungu (s.w) kwa utukufu wake, limekosa baraka. (Ibn Majah).

 


Kutckana na hadithi ilisimuliwa naAbdullah bin Mas'ud (r.a), Mtume (s.a.w) amelündisha tashahud mbili, ya kwanza ni ile ya swala (Tahiyyatu) na ya li ni ile inayopalikana katika khutuba ya kukidhiwa haja, kama vile khutuba ya ndoa, ambayo inaanza na kuendelea kama iluatavyo:

 

Sfa zote anastahiki Mwenyezi Mungu (s.w). tunamtukuza kwa Utukufu wake, Tunataka msaada wake, na msamaha Wake, na tunajikinga kwake na shari ya nafsi zenu na shari ya vitendo vyetu viovu. Ambaye Mwenyezi Mungu amemuongoa, hakuna awezaye kumpoteza, na ambaye amempoteza hatakuwa na wa kumwongoa. Na ninashuhudia kuwa hapana mola ila Mwenyezi Mungu (s.w), na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtumwa wake na Mjumbe Wake.

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha wala msfe ispokuwa mmekwisha kuwa Waislamu kamili. (3:102).

 

Enyi Watu! Mcheni Mola wenu ambaye amekuumbeni katika nafsi (asili) moja. Na akamuumba mkewe katika nafsi ile ile. Na akaeneza wanaume wengi na wanawake kutoka wawili hao. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana.Na (muwatazame) jamaa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mlinzi juu yenu. (4:1).

 

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya Haki Atakutengenezeeni vizuri vitendo vyenu na Atakusameheni madhambi yenu; Na anayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake bila shaka amefuzu kufuzu kukubwa. (33:70-71).

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1355


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la Hija halifikiwi?
Soma Zaidi...

Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake
Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii Soma Zaidi...

Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq
Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

Funga za kafara, aina zake na sababu za funga hizi za kafara na hukumu zake
Soma Zaidi...

Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika. Soma Zaidi...

Zijuwe Suna zinazofungamana na swaumu na funga ya ramadhani
Soma Zaidi...

Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki. Soma Zaidi...

Kusimamisha Swala
Kusimamisha Swala. Soma Zaidi...

Maana ya uadilifu na usawa na tofauti zao
Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa Soma Zaidi...