image

Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi

Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Tofauti na Qur-an, ambayo iliandikwa mara tu baada ya kushushwa chini ya malekezo na usimamizi wa Mtume (s.a.w) mwenyewe, Hadith za Mtume (s.a.w) ambamo ndani yake ndio tunapata sunnah yake, zimeandikwa na watu kulingana na walivyomuona, au walivyomsikia. Historia ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w) katika vitabu vya Hadith , imechukua takriban muda wa karne tatu. Kwa kurahisisha tutaigawa historia ya kuhifadhiwa Hadith katika maandishi katika hatua nne zifuatazo:  - Wakati wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Maswahaba wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Tabi'iina.
- Wakati wa Tabii Tabi'iina.

Wakati wa Mtume (s.a.w)
Wakati wa Mtume (s.a.w), hapakuwa na uandishi mkubwa wa Hadith kwa sababu:

Kwanza, Mtume mwenyewe alikuwepo, hivyo kilichokuwa muhimu kwa Masahaba ni kufuata mafundisho ya Mtume(s.a.w) na kuigiza mwenendo wake,kila walipokwama katika utendaji au kila walipotatizwa na tatizo lolote, walimwendea Mtume(s.a.w) na aliwakwamua au kuwatatulia tatizo lolote walilokuwa nalo.

Pili, Masahaba katika kipindi hiki walijishughulisha sana na kuandika, kusoma na kuhifadhi Qur-an moyoni na kuitekeleza katika maisha yao ya kila siku.

Tatu, kwa kuwa mwanzoni Mtume (s.a.w) aliwakataza Masahaba wake kuandika Hadith, walizoea kutoandika Hadith hata wakati waliporuhusiwa kuandika na walipendelea kutoandika kuliko kuandika Hadith.

Nne, katika wakati huu wa Mtume (s.a.w) Masahaba walishughulika sana katika harakati za kuuhami Uislamu ambao ulikuwa umesongwa sana na maadui wake ambao walipania sana kumuua Mtume, Uislamu na Waislamu.

Kutokana na sababu hizi nne na nyinginezo, uandishi wa Hadith haukupewa nafasi nzito katika kipindi hiki cha Mtume (s.a.w). Hivyo, Hadith nyingi zilibakia katika matendo na vifua vya Masahaba. Masahaba waliokuwa karibu sana na Mtume (s.a.w) kwa muda mrefu wa maisha yao, walihifadhi Hadith nyingi zaidi kuliko wale waliokaa mbali na Mtume (s.a.w). 

Miongoni mwa Masahaba waliofahamika kuwa mashuhuri kwa kuhifadhi Hadith nyingi ni Abu Hurairah, bibi Aysha (mkewe Mtume (s.a.w)) 'Abdullah bin 'Umar, 'Abdullah bin 'Abbas, na Abdullah bin 'Amr na Abdallah bin Masu'ud (r.a)


 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 683


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi
Soma Zaidi...

DUA 120
Soma Zaidi...

DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...

DUA ZA WAKATI WA HASIRA
DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA. Soma Zaidi...

Mzazi na msafiri na mwenye kudhulumiwa dua zao hujibiwa kwa haraka
Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri. Soma Zaidi...

NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA. Soma Zaidi...

ADABU ZA KUOMBA DUA
ADABU ZA KUOMBA DUA. Soma Zaidi...

Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 3: Nguzo za uislamu
Katika hadithi hii utakwenda kujifunza nguzo za uislamu Soma Zaidi...

DUA 11 - 20
11. Soma Zaidi...

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii
11. Soma Zaidi...

DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...

DUA 32 - 40
32. Soma Zaidi...