picha

Huduma kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa, ni huduma anayopewa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa.

Huduma kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa.

1. Kwanza mtoto akigunduliwa kubwa na tatizo la Maambukizi kwenye mifupa anapaswa kupewa antibiotics ambayo inatibu ugonjwa huu ni vizuri mtoto kupewa antibiotics kwenye mfumo wa maji yaani drip kwa kufanya hivyo bakteria wanaosababisha Maambukizi wanaweza kupunguza au kuondolewa.

 

2. Jaribu kumweka mtoto kwenye mkao mzuri zaidi ili kuweza kupunguza kiwango cha maumivu, kwa sababu ya Maambukizi kuna sehemu ambazo zinakuwa na maumivu kupita sehemu nyingine kwa hiyo sehemu hizo zinabidi kugundulika na kuepuka kukaliwa au kukaliwa, kwa hiyo mtoto anapaswa kuwekwa kwenye sehemu nzuri.

 

3. Kwa kuwa mtoto anakuwa kwenye drip na anakuwa na maumivu kwa hiyo anapaswa kupimwa joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo ili kuona kama kuna mabadiliko, kama joto la mwili liko juu mtoto anapaswa kushushwa joto la mwili kwa kutumia baadhi ya Dawa na maumivu kama vile paracetamol ili kuepuka matatizo mengine ambayo usababishwa na joto la mwili kuwa juu kama vile degedege na kupungukiwa kwa damu.

 

4, Hakikisha kama kuna kidonda kidonda kwenye mfupa kilichotokana na Maambukizi kimesafishwa kwa kufanya hivyo tunaweza kupunguza maumivu na kuongeza kiwango cha kupona haraka na pia vitu vyote vya kusafishia kidonda vinapaswa kuwepo ili kukifanya kipone haraka.

 

5. Kwa mtoto hakikisha unaangalia kiasi cha kilichoingia na kiasi kilichotoka, kwa kuangalia kiasi kilichoingia angalia maji anayokunywa, chai au uji na vitu vyote vya aina ya kumiminika vilivyoungia mwilini na pia anapaswa kuangalia kiasi kilichotoka kwa kuangalia mkojo uliotolewa na jasho kama limetoka tunafanya hivi ili kuzuia kuishiwa kwa maji mwilini.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1735

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 web hosting     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia virusi vya ukimwi

Posti hii inaelezea kuhusiana na kujikinga au kuzuia virusi vya ukimwi.

Soma Zaidi...
Vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.

Soma Zaidi...
Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi.

Soma Zaidi...
Madhara ya kulala usiku sana

​Post hii inachunguza changamoto za kiafya zinazotokana na kukosa usingizi wa kutosha au kuchelewa kulala. Tutajadili athari zake kwenye mfumo wa kinga, uwezo wa kufikiri, na uzalishaji wa homoni, huku tukitoa vidokezo vya kuboresha mzunguko wako wa kulala kwa maisha bora.

Soma Zaidi...