picha

Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi

Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.

Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kumfariji mgonjwa na kumpa pole tukijua kuwa sio yeye pekee yake ambaye amepatwa na ugonjwa huu bali ni tatizo la walio wengi na ni la mda maana utokea kwa siku chache na utoweka na kumhakikishia kuwa akibeba mimba hatapata tena tatizo hili 

 

2. Chukua maji ya moto weka kwenye chupa na weka kwenye tumbo lake na maumivu yatapungua na pengine utoweka kabisa na pengine kama hauna chupa chukua kitambaa chochote na weka kwenye maji ya moto ila sio sana kamua na weka kwenye tumbo hasa hasa sehemu ya maumivu na maumivu yatapungua au yataisha kabisa kwa kufanya hivyo mara kwa mara mgonjwa atapata nafuu.

 

3. Mpatie mgonjwa dawa za kupunguza maumivu kama vile asprin, panadol na dawa hizi zisitumike mara kwa mara zinaweza kusababisha vidonda vya tumbo kwa hiyo wanaovitumia kila mara wawe na tahadhari kubwa kwa sababu matumizi ya mara kwa mara uweza kuleta matatizo makubwa 

 

4. pia mgonjwa anaweza kupatiwa vidonge vya njia za uzazi wa mpango navyo usaidia kupunguza tatizo aina ya vidonge hivi uwa vina homoni ambavyo kwa kitaalamu huitwa combine contraceptive pill, huwa vina homoni zilizochanganywa kwa hiyo msiogope kwamba vina madhara ila upunguza maumivu ya tumbo.

 

5. Kwa sababu maumivu ya tumbo kama tulivyotangulia kusema kwamba uweza kusababishwa na kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi kwa hiyo ikiwa uvimbe huo umeonekana ni vizuri kumwandaa mgonjwa kwa ajili ya upasuaji ili kuweza kuondoa uvimbe huo ambao unaweza kuleta madhara makubwa zaidi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2447

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea ugumba.

Post huu inahusu zaidi mambo yanayopelekea ugumba kwa wanaume, ni mambo ambayo uchangia au upelekea mwanaume kukosa uzazi.

Soma Zaidi...
Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto mchanga kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, ni tatizo ambalo utokea kwa baadhi ya wajawazito kupata mtoto mwenye Uzito mkubwa, wengine uona kama ni sifa ila Kuna madhara yanaweza kujitokeza kwa Mama hasa wakati wa kujif

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Soma Zaidi...
faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito

Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba

Soma Zaidi...
Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia

Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?

Soma Zaidi...