Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.
Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kumfariji mgonjwa na kumpa pole tukijua kuwa sio yeye pekee yake ambaye amepatwa na ugonjwa huu bali ni tatizo la walio wengi na ni la mda maana utokea kwa siku chache na utoweka na kumhakikishia kuwa akibeba mimba hatapata tena tatizo hili
2. Chukua maji ya moto weka kwenye chupa na weka kwenye tumbo lake na maumivu yatapungua na pengine utoweka kabisa na pengine kama hauna chupa chukua kitambaa chochote na weka kwenye maji ya moto ila sio sana kamua na weka kwenye tumbo hasa hasa sehemu ya maumivu na maumivu yatapungua au yataisha kabisa kwa kufanya hivyo mara kwa mara mgonjwa atapata nafuu.
3. Mpatie mgonjwa dawa za kupunguza maumivu kama vile asprin, panadol na dawa hizi zisitumike mara kwa mara zinaweza kusababisha vidonda vya tumbo kwa hiyo wanaovitumia kila mara wawe na tahadhari kubwa kwa sababu matumizi ya mara kwa mara uweza kuleta matatizo makubwa
4. pia mgonjwa anaweza kupatiwa vidonge vya njia za uzazi wa mpango navyo usaidia kupunguza tatizo aina ya vidonge hivi uwa vina homoni ambavyo kwa kitaalamu huitwa combine contraceptive pill, huwa vina homoni zilizochanganywa kwa hiyo msiogope kwamba vina madhara ila upunguza maumivu ya tumbo.
5. Kwa sababu maumivu ya tumbo kama tulivyotangulia kusema kwamba uweza kusababishwa na kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi kwa hiyo ikiwa uvimbe huo umeonekana ni vizuri kumwandaa mgonjwa kwa ajili ya upasuaji ili kuweza kuondoa uvimbe huo ambao unaweza kuleta madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.
Soma Zaidi...Dalili ya mimba ya wiki moja(1)
Mwanaume na mwanamke wanapo kutana na kujamiina kama mwanamke yupo kwenye ferlile process ni rahisi kupata mbimba. Sparm Zaid ya million moja huingia kwenye mfuko wa lakin sparm moja ndio huweza kuingia kwenye ovum(yai)lakin nyingine hubaki kwenye follopi
Soma Zaidi...Dalili za upungufu wa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.
Soma Zaidi...Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu
Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.
Soma Zaidi...