Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.
Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kumfariji mgonjwa na kumpa pole tukijua kuwa sio yeye pekee yake ambaye amepatwa na ugonjwa huu bali ni tatizo la walio wengi na ni la mda maana utokea kwa siku chache na utoweka na kumhakikishia kuwa akibeba mimba hatapata tena tatizo hili
2. Chukua maji ya moto weka kwenye chupa na weka kwenye tumbo lake na maumivu yatapungua na pengine utoweka kabisa na pengine kama hauna chupa chukua kitambaa chochote na weka kwenye maji ya moto ila sio sana kamua na weka kwenye tumbo hasa hasa sehemu ya maumivu na maumivu yatapungua au yataisha kabisa kwa kufanya hivyo mara kwa mara mgonjwa atapata nafuu.
3. Mpatie mgonjwa dawa za kupunguza maumivu kama vile asprin, panadol na dawa hizi zisitumike mara kwa mara zinaweza kusababisha vidonda vya tumbo kwa hiyo wanaovitumia kila mara wawe na tahadhari kubwa kwa sababu matumizi ya mara kwa mara uweza kuleta matatizo makubwa
4. pia mgonjwa anaweza kupatiwa vidonge vya njia za uzazi wa mpango navyo usaidia kupunguza tatizo aina ya vidonge hivi uwa vina homoni ambavyo kwa kitaalamu huitwa combine contraceptive pill, huwa vina homoni zilizochanganywa kwa hiyo msiogope kwamba vina madhara ila upunguza maumivu ya tumbo.
5. Kwa sababu maumivu ya tumbo kama tulivyotangulia kusema kwamba uweza kusababishwa na kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi kwa hiyo ikiwa uvimbe huo umeonekana ni vizuri kumwandaa mgonjwa kwa ajili ya upasuaji ili kuweza kuondoa uvimbe huo ambao unaweza kuleta madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Dalili za Maambukizi na Uvimbe katika mirija ya uzazi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi
Soma Zaidi...Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?
Soma Zaidi...Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Zifahamu sifa za mtoto mchanga.
Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy
Soma Zaidi...Jinsi ya kupata mtoto wa kiume
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.
Soma Zaidi...