HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA


Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu. Ni vigumu kuwatofautisha wenye sumu na wasio na sumu kwani wakati mwengine wanafanana sifa. Wataalamu wameweka njia kadhaa za kuweza kuwajuwa weenye sumu. Nyoka mwenye sumu ana sifa zifuatazo


1.kichwa chake kipo katika pembe tatu


2.Rangi zake zinameremeta sana


3.Mboni ya Macho yao yamefanana na macho ya paka


4.Wanapoogelea kwenye maji miili yao inaelea juu



Tmbua kuwa sifa hizi hata nyoka wasio na sumu wamaweza kuwa nazo. Kuwa makini na kaa mbali na nyoka wa aina yeyote kama huna ujuzi na utambuzi huu. Mtu aliyengatwa na nyka mwenye sumu ataonyesha dalili zifuatazo:-


1.Uchovu

2.Kizunguzungu

3.Anaweza kuzimia

4.Kichefuchefu

5.Kuharisha

6.Kutapika

7.Mapigo ya moyo kuongezeka kwa kasi

8.Misuli kukosa uweze wa kutanuka na kusinyaa

9.Kuvimba eneo alipong’atwa.



Ukiona mtu ameng’atwa na nyoka na akaonyesha dalili hizi, wahi kuomba msaada ili awahishwe ituo cha afya kwa haraka. Hakikisha unampatia huduma ya kwanza ili kupunguza athari za kusambaa kwa sumu mwilini. Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng’atwa na nyoka inaweza kuwa kwa nama zifuata zo:-




1.mtulize mgonjwa nafsi yake, mpe maneno matamu na ya kutuliza. Hii itasaidia moyo kupunguza kazi ya kusambaza damu mwilini, hivyo sumu haita sambaa kwa kasi.


2.Muweke mgonjwa chini, na katu usimtembeze, mlaze chini kwa namna ambayo sehemu alipong’atwa itakuwa chini. Kwa mfano kama ameng’atwa mguuni, unaweza kumuwekea kitu kichwani akaegemea kwa mto ili sehemu ya mguuni iwe chini.


3.Ondoa mengo ya nyoka kwa uangalifu na katu usimishe eneo alilongatwa na nyoka.


4.Kama mgonjwa ana kizunguzungu, ama baridi mfunike kwa nguo ili kumuongezea joto


5.Chukuwa maelezo kuhusu aina ya nyoka, hii itasaidia wataalamu wa afya kujuwa tiba sahihi.


6.Osha eneo kwa kupitishia maji kwa juu na katu usisugue ama kuminya jeraha.



Usifanye vitu hivi:
1.Usinyonye sumu kwa mdomo wako
2.Usimpe mgonjwa chakula wala maji
3.Usimtembeze mgojwa
4.Usitumie barafu sehemu yenye jeraha
5.Usifunge kwenye jeraha eti kuzuia mzunguo wa damu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 4554

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo, ni njia ya kuwasaidia wagonjwa waliopata madonda ya tumbo

Soma Zaidi...
Kazi ya chanjo ya Surua

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa.

Soma Zaidi...
Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.

Soma Zaidi...
Upungufu was fati

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu was fati

Soma Zaidi...
Namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi

Soma Zaidi...
Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na minyoo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo

Soma Zaidi...
Huduma kwa mgonjwa mwenye maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi huduma Kwa mgonjwa mwenye maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo,ni huduma maalumu ya kumsaidia mgonjwa aliyepata maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...