HUKUMU YA KUFINGA KWA KIFUATA KUANDAMA KWA MWEZI


image


Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.


Kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani

Swaumu ya Ramadhani inaanza kwa kuona mwezi baada ya siku ya 29 Shaaban au 30 Shaaban kama tunavyofahamshwa katika hadithi zifu atazo:
“Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Msifunge mpaka muuone mwezi umeandama na msiache kufunga mpaka muone mwezi (wa Shawwal) umeandama. Kama kuna mawingu (hukuuona) hesabu kamili (siku 30). Katika simulizi nyingine amesema: Mwezi una masiku 29, kwa hiyo usifunge mpaka uone mwezi umeandama kama kuna mawingu subiri na kamilisha idadi ya siku 30.”
(Bukhari na Muslim)

 


Kutokana na Hadithi hii ni wazi kuwa watu hawaruhusiwi kufunga kwa kufuata kalenda. Inabidi juhudi za kuuangalia mwezi ziwepo kwa umma wa Waislamu tangu mwanandamo wa Shaaban.

 


“Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah ameagiza: Hesabu mwandamo wa Shaaban kwa ajili ya Ramadhani”. (Tirmidh).

 


Kwanini kufuata mwandamo wa mwezi?

 


Tunafunga kwa kuona mwezi kwa sababu ndivyo alivyotuamrisha Mtume wa Allah (s.w) kama tulivyojifunza kutokana na hadithi zilizonukuliwa hapo juu. Kumtii Mtume (s.a.w) ndio Uislamu. Rejea Qur-an katika aya zifuatazo:

 

“Sema: “Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkikengeuka (Allah atakuadhibuni) kwani Allah hawapendi makafiri.” (3:32)

 

“… Na anachokuleteeni Mtume, kipokeeni, na anachowakataza
kiacheni…” (59:7).

 

“Anayemtii Mtume, kwa yakini amemtii Mw enyezi Mungu…” (4:80)

 

Pia amri hii ina hekima yake. Mwaka unaohesabiwa kwa mwandamo wa mwezi una siku 354 kwani kwa wastani mwezi mmoja una siku 29?. Mwaka unaohesabiwa kwa kufuata jua, muda ambao dunia huchukua kulizunguka jua una siku 365, saa 5, dakika 48 na nukta 46. Kwa hiyo ukilinganisha mwaka wa hesabu ya mwezi na mwaka wa hesabu ya jua, utaona kuwa mwaka wa mwezi ni mfupi kwa siku10 hivi. Hivyo mwezi wa Ramadhani hurudi nyuma siku kumi katika kila mwaka ukilinganisha na mwaka wa jua. Hivyo basi, mtu yeyote atakayejaaliwa kufunga muda wa miaka 36 hatakuwa na siku au msimu katika mwaka ambao hakuufunga. Yaani atawahi kufunga siku zote za jua, za mvua, za upepo, za shwari, za kusi, za kaskazi na kadhalika. Kama ingelikuwa inafuatwa kalenda ya mwaka wa jua, wengine daima wangalifunga nyakati za joto tu, wengine nyakati za baridi tu, wengine nyakati za njaa tu, wengine nyakati za mavuno na kadhalika ilimuradi pasingalikuwa na mabadiliko.

 

Ni lazima kila mfungaji aone mwezi?

 


Mwezi wa Ramadhani akiona mtu mmoja muadilifu inatosha na wengine waliobaki itawabidi wafunge. Hivi ndivyo alivyoamrisha Mtume (s.a.w) kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:

 


“Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mwarabu wa Jangwani alikuja kwa Mtume (s.a.w) akasema: Hakika nimeuona mwezi wa Ramadhani umeandama. Mtume (s.a.w) akamuuliza: Unashuhudia kuw a hapana Mola ila Allah? “Ndio” alijibu. Akamuuliza tena: Unashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume w a Allah? Akajibu “Ndio ”. Akasema (Mtume): Ee Bilal! Watangazie w atu kuw a haw ana budi kufunga kesho”. (Abu Daud, Tirm idh, Nisa i, Ibn Majah).

 


“Ibn Omar (r.a) ameeleza: Watu waliuona mwezi. Kisha nikamfahamisha Mtume (s.a.w): Hakika nimeuona. Kwa hiyo alifunga na aliwaamrisha watu wafunge”. (Abu Daud, Darimi).

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    4 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    5 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Swala ya jamaa na taratibu zake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake. Soma Zaidi...

image mambo yanayofungua swaumu
post hii ijakwenda kukufundisha mambo yanayoharibu funga Soma Zaidi...

image Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...

image Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala. Soma Zaidi...

image Kugungisha ndoa ya kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Hapa utajifunza jinsi ya kuozesha hatuwa kwa hatuwa. Pia utajifunza masharti ya kuoa na masharti ya kuolewa. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa
Kutawadha ni katika ibada muhimu za mwanzo kutakiwa kuzijuwa na ni lazima. Swala yako haitaweza kutimia bila ya kujuwa udhu. Inakupasa kujuwa nguzo za udhu, yanayoharibu udhu na namna ya kutawadha kifasaha. Hapa utajifunza hatuwa za kutawadha Soma Zaidi...

image Taratibu za kufanya kazi na kuajiri katika uislamu
Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake. Soma Zaidi...

image Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali. Soma Zaidi...

image Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii. Soma Zaidi...