image

Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa

Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.

Talaka Kabla ya Jimai:
Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa. Mwanamume atatoa talaka na mkewe ataachika hapo hapo bila ya kukaa eda. Kama mwanamume ameshatoa mahari hatadai chochote kama yeye ndiye aliyeamua kumuacha mkewe bali atalazimika kumpa kiliwazo (kitoka nyumba). Ikiwa hajatoa mahari atalazimika kutoa nusu ya mahari. Kama mke ndiye aliyedai talaka atalazimika kumrudishia mumewe mahari aliyompa. Hukumu ya talaka ya ama hii inabainika katika aya zifuatazo:

 

Si dhambi kwenu kama mkiwapa wanawake talaka ambao hamjawagusa au kuwabainishia mahari (yao). Lakini wapeni cha kuwaliwaza (kitoka nyumba); mwenye wasaa kadiri awezavyo, na mwenye dhiki kadiri awezavyo. Matumizi hayo (wanayopewa) yawe kama inavyosema Sharia. Ndio wajibu kwa wafanyao mema. (2:236)

 

Na kama mkiwapa talaka kabla ya kuwagusa na mmekwisha wawekea hayo mahari (basi (wapeni) nusu ya hayo mahari mliyoagana, isipokuwa wanawake wenyewe waache (wasitake kitu), au yule (mume) ambaye kifungo cha ndoa ki mikononi mwake aache (haki yake kwa kumpa mahari kamili). Na kuachiana ndiyo kunakomkurubisha mtu sana na kumcha Mungu. Wala msisahau kufanyiana ihsani baina yenu; hakika Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyafanya. (2:237)





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 944


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu
HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU. Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Fadhila za kufunga mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

haki za mwanamke za kisiasa katika uislamu
Haki ya Kushiriki Katika Siasa. Soma Zaidi...

umuhimu wa swala katika uislamu
Soma Zaidi...

Kujitwaharisha kutokana na najisi
Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu? Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke Ulaya chini ya kanisa hapo zamani
Soma Zaidi...

Nini maana ya twahara katika uislamu, na ni zipi njia za kujitwharisha
1. Soma Zaidi...

Hili ndilo hasa lengo la kuamrishwa kufunga
Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu
3. Soma Zaidi...