IJUE DAWA YA KUTIBU UGONJWA WA UKOMA


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu ukoma,na dawa hiyo ni dawa ya Dapsoni, hii dawa usaidia kuzuia nerve zisiendelee kupoteza kazi yake pia na ngozi iendelee kuwa kawaida


Ijue dawa ya kutibu ugonjwa wa ukoma .

1. Ukoma ni mojawapo ya ugonjwa ambao uharibu nerve na mfumo mzima wa fahamu ambapo mgonjwa mara nyingi ushindwa kuhisi vitu vya hatari kama moto kwa sababu ya kuharibika kwa mfumo wa fahamu, pia na viungo kama vidole uweza kukatika yeye bila kuwa na taarifa yoyote Ile hali ambayo upelekea na ngozi ya mwili kutonawili ,kwa hiyo hata jamii uwatenga wagonjwa hawa, kwa matumizi ya dawa ya dapsoni utibu uaribifu wa nerve na kuzuia uaribifu wa ngozi na kumweka mgonjwa kwenye hali nzuri na akakubarika katika jamii.

 

2. Dawa hii kwa kawaida IPO kwenye mfumo wa vidonge na utumiwa kila kila siku kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, matibabu ya ugonjwa huu dawa uanza kutumika kidogo kidogo na baadae dozi uongezeka kuanzia mwezi wa kwanza mpaka wa pili, na matibabu yake ni marefu kidogo kwa sababu utumia takribani miezi kumi na minane na matibabu yanaweza kuendelea kwa kutegemea hali ya mgonjwa kwa sababu kuna wagonjwa ambao uanza matibabu mwanzoni mara tu wanapoona dalili Ila Kuna wale wanaoanza kwa kuchelewa na Kuna wale wanaofuatwa kutoka majumbani kwao kwa kulazimishwa Ili kuzuia kuendelea kuongezeka kwa ugonjwa.

 

3. Kwa sababu tofauti tofauti na matibabu utofautiana kwa sababu Kuna wanaopenda kupona haraka, Kuna ambao hawajali na Kuna wanaolazimishwa kutumia dawa, kwa hiyo kupona utegemea bidii ya mgonjwa kuanza matibabu na uaminifu katika matumizi ya dawa, dawa hii ikitumiwa uweza kukaa mwilini kuanzia masaa mawili mpaka masaa nane baada ya kuitumia, kwa hiyo ikitumiwa tu uenda kufanya kazi kwenye ngozi,nyama za mwili kwa kitaamu muscle na pia dawa hii inaenda kwenye ini na kweye Figo ambapo inawezekana kukaa kwa mda wa wiki tatu hivi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kunywa sana maji Ili kuweza kuondoa sumu ya dawa inayokaa kwenye ini na Figo.

 

4. Dawa hii inatumika na watu wenye ukoma na pia wale ambao Wana dalili za ukoma na haujajitikeza kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii ni wale wenye aleji na dapson drug na pia wale ambao maudhi madogo madogo yamekuwa mengi kiasi cha kwamba hawezi kuendelea kutumia dawa hii.

 

5. Pia katika matumizi dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile kichefuchefu na kutapika, kuharisha mapigo ya moyo kwenda mbio, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu kukosa hamu ya kula,ikiwa maudhi haya yameongezeka zaidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na pia maudhi madogo madogo kwa wagonjwa wa ukoma ni makubwa kidogo kwa hiyo jamii inapaswa kuwa karibu na wagonjwa hawa kuepuka tabia mbaya ya kuwanyanyapaa na kuona  kwamba sio binadamu , wanapaswa kutunzwa vizuri kwa sababu dawa wanazozitumia ni kali.

 

6. Pia kwa wale walio na matatizo ya moyo na presha wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa Ili kuweza kupata ushauri zaidi na pia dawa hizi hazitolewi kiholela holela Bali ni kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Jifunze fiqh    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)
Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin, Nuprin. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya marcolides dawa ya kuuwa bakteria, kwenye mfumo wa hewa
Post hii inahusu zaidi dawa ya macrolide ni mojawapo ya dawa ya kutibu au kupambana na bakteria na upambana na bakteria wafuatao streptococcus pyogenes, staphylococcus aureus na haihusiki na haemophilia influenza ambao usababisha maambukizi kwenye mfumo wa hewa. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya griseofulvin
Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi. Soma Zaidi...

image Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu. Soma Zaidi...

image Ijue dawa ya sulphadoxine na pyrimethamine (sp)
Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria. Soma Zaidi...

image Ijue dawa ya kutibu ugonjwa wa ukoma
Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu ukoma,na dawa hiyo ni dawa ya Dapsoni, hii dawa usaidia kuzuia nerve zisiendelee kupoteza kazi yake pia na ngozi iendelee kuwa kawaida Soma Zaidi...

image Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini
Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya propranolol ambayo hutibu magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo. Soma Zaidi...

image Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.
Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea. Soma Zaidi...