Ijue dawa ya sulphadoxine na pyrimethamine (sp)

Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.

Ijue dawa ya  Sp.

1. Kama tulivyotangulia kusema kwamba ni dawa ambayo ina majina mawili ambayo ni sulphadoxine na pyrimethamine ambayo uunda dawa hii ya Sp, dawa hii iko kwenye mfumo wa vidonge ambapo kila sehemu ina milligrams zake ambapo sulphadoxine ina milligrams miatano na pyrimethamine ina miilgram ishirini na tano jumla kuu ufanya miligramu mia tano ishirini na tano.

 

2. Dawa hii utumika sana kwa wanawake wajawazito na haipendekezwi kama mojawapo ya dawa za kutibu malaria kwa sasa, ila kwa wajawazito ikitokea wakapata malaria ingawa wanatumia sp matibabu yao wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya ili wawaeleze cha kufanya.

 

3. Kwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutumia vidonge hivi vya sp pindi wanapogundua kwamba ni wajawazito kwa sababu vidonge hivi vikimezwa uenda moja kwa moja mpaka kwenye sehemu ya mwanzo ya kondo la nyuma na kuweza kuzuia wadudu wanaosababisha malaria kutoingia kwenye kondo la nyuma na kusababisha madhara mbalimbali kama vile mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, mtoto kutokuwa na afya nzuri akiwa tumboni, au mimba kutoka.

 

4. Kwa hiyo akina mama wanapaswa kujua kabisa kwamba hizi dawa ni za muhimu sana wakati wa ujauzito kwa sababu bila matumizi ya dawa hizi madhara makubwa yanaweza kutokea ambayo usababisha kukosa mtoto, au mimba kutoka, mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, haya matatizo utokea kwa sababu ya kuwepo kwa wadudu wa malaria kwenye kondo la nyuma na kusababisha uharibifu kwenye sehemu hiyo.

 

5. Akina mama wote wanapaswa kutumia dawa hizi isipokuwa wale wenye aleji na sulphur , au wanaotumia dawa ambazo kwa kitaalamu huitwa cotrimoxazole au wale wamama ambao wamegundulika na malaria kwa hiyo wanapaswa kufuata kawaida ya matibabu ya ugonjwa wa malaria kadri ya wataalamu wa afya.

 

6. Kwa hiyo akina mama wenye imani potovu kuhusu dawa hizi wanapaswa kujua kwamba dawa hizi ni za muhimu sana na kutotumia dawa hizi ni hatari sana hasa kwa afya ya mtoto.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 4066

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini

Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.

Soma Zaidi...
Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole

Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu maumivu ya jino

Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.

Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa.

Soma Zaidi...
Tiba ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tiba ya minyoo

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili

Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio

Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.

Soma Zaidi...