Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

Download Post hii hapa

Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu



Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo:
Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.Tunajifunza katika Qur-an kuwa jambo la kwanza alilotunukiwa Adam (a.s) mara tu baada ya kuumbwa kwake ni kupewa elimu.


“Na (Mwenyezi Mungu) akamfundisha Adam majina ya vitu vyote...” (2:3 1)
“Majina ya vitu vyote” katika aya hii inaashiria fani zote za elimu ambazo anahitajia mwanaadamu hapa duniani ili afikie kwa ufanisi lengo la kuumbwa kwake. Pia tunajifunza katika Quran kuwa mwenye elimu na hekima amepewa kheri nyingi.


(Mungu ) humpa hikma amtakaye, na aliyepewa hikma bila shaka amepewa kheri nyingi. Na hawakumbuki ila wenye akili. (2.269).
Kutafuta elimu (kusoma) ni amri ya kwanza kwa mwanaadamu. Tunajifunza kutokana na historia ya kushushwa Qur-an kuwa Wahay wa kwanza kumshukia Mtume (s.a.w) ambao ndio ulimtawazisha rasmi kuwa mtume ni ule unaopatikana katika aya tano za mwanzo za Suratul-’Alaq:


“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.Ambaye amemuumba mwanaadamu kwa ‘Alaq (kitu chenye kuning’inia). Soma na Mola wako ni karimu sana. Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu (chungu ya) mambo aliyokuwa hayajui”.(96:1-5)
Kutokana na aya hizi, kwa muhtasari, tunajifunza yafu atayo:



1. Kusoma kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ni jambo la kwanza waliloamrishwa wanaadamu na Mola wao.



2. Kusoma kwa jina la Mola wako ni kusoma kwa ajili ya kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu au ili kuweza kumwabudu Allah(s.w) inavyostahiki na kusimamisha Uislamu katika jamii.



3. Radhi za Mwenyezi Mungu zitapatikana pale mwanaadamu atakapoweza kufikia lengo la maisha yake la kumuabudu Allah (s.w) kwa kuzingatia maamrisho na mipaka ya Mwenyezi Mungu katika kila kipengele cha maisha.



4. Amri hii ya kusoma hailengi fani maalum tu ya elimu; bali kila fani itakayomuwezesha mwanaadamu kufikia lengo la maisha yake kwaufanisi.



5. Chanzo au chimbuko la fani zote za elimu ni Allah (s.w). Hivyo kwa Muislam mlango wa kwanza wa elimu ni kusoma kwa mazingatio Qur-an na hadithi sahihi za Mtume (s.a.w) na kusoma maarifa ya Uislamu kwa ujumla kutokana na vyanzo hivi viwili.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1755

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba

Nini kilichangia ongezeko la uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba.

Soma Zaidi...
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA.

Soma Zaidi...
Dua Sehemu ya 02
Dua Sehemu ya 02

Zijuwe nyakati ambazo dua inakubaliwa kwa haraka zaidi. Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hitakubaliwa.

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.

Soma Zaidi...
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI

DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI.

Soma Zaidi...
ni nyakati zipi ambazo dua hukubaliwa kwa haraka?
ni nyakati zipi ambazo dua hukubaliwa kwa haraka?

Dua ni moja ya ibada ambazo zinamfanya mja awe karibu na Mweznyezi Mungu. Allah amesisitiza tumuombe dua kwa shida zetu zote, pia akaahidi kuwa atatujibu maombi yetu muda wowote tutakao muomba. Sasa ni zipi nyakati nzuri zaidi kuomb adua?

Soma Zaidi...