image

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii

Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?

Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke?

Kama tulivyojifunza katika Qur-an (4:4), mahari ni hidaya kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa maana nyingine, mahari ni mali anayoitoa mwanamume kumpa mwanamke anayetaka kumuoa kwa ajili ya kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu (s.w) aliyemuamrisha kutoa mali hiyo iii kumhalalishia mwanamke anayemtaka awe mkewe wa ndoa. Na mwanamke anapokea mahari hayo ikiwa ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa mtazamo huu wa Uislamu mwanamume anapotoa mahari hatakuwa na hata chembe ya hisia kuwa ni bei ya mwanamke anayemuoa. Hali kadhalika, kwa mtazamo huu, mwanamke atakapopokea mahari yake hatakuwa na hata chembe ya hisia kuwa amejiuza kwa mume anayemuoa.

 


llivyo, ni kwamba katika jamii nyingi zisizo za Kiislamu, mahari imefanywa kama bei ya kumnunulia mke inayotozwa na wazazi au walezi wa mwanamke anayeolewa. Ni katika mtizamo huu wa biashara unaowafanya wale wajiitao watetezi wa Haki na Hadhi ya Mwanamke, waishutumu mahari kuwa imetoa mchango mkubwa katika kumnyanyasa mwanamke katika jamii. Ni kweli kabisa kuwa mwanamke, kwa kisingizio cha mahari, amekandamizwa na kunyanyaswa kiasi kikubwa na wanaume katika jamii nyingi za Kikafiri.

 

Lakini, ni kweli kuwa mahari waliyotoa wanaume katika jamii hizi ndio hasa sababu ya kuwashusha wanawake hadhi zao na kuwakandamiza? Je, mahari yakiondolewa kama watetezi wa haki za wanawake wanavyodai, wanawake watapata haki zao na hadhi yao ikarudi mahali pake? Ukweli ni kwamba tatizo haliko kwenye mahari bali tatizo liko kwenye kukiuka maamrisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu (s.w) katika utoaji wa hayo mahari na katika kuendesha maisha ya kila siku kwa ujumla.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 834


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Faida za kuswali swala za sunnah
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah. Soma Zaidi...

Kumuandaa Maiti kabla ya kufa ama kukata roho
Soma Zaidi...

Mgawanyo na matumizi ya mali katika uislamu
6. Soma Zaidi...

Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...

Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

Haki za mwanamke katika uislamu
Soma Zaidi...

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii. Soma Zaidi...

Swala ya maiti, namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake na suna zake, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

hukumu na taratibu za biashara ya ushirika na hisa katika uislamu
Soma Zaidi...

Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...