Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Haki ya Kutaliki
Katika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Kalika sheria ya Klislamu haki ya kutoa talaka iko kwa wote, mume na mke.

 

(a)Haki ya Mume kutoa talaka
Ilivyo katika kawaida ya maumbile mwanamume ndiye anayeanza kutoa posa au pendekezo Ia kuoana. Katika sheria ya Kiislamu, mwanamume pia ndiye anayepaswa kutoa mahari kumpa anayemtaka waoane, ndiye mwenye jukumu Ia kumlisha mkewe na kukidhi haja zake zote, na ndiye kiongozi wa familia. Kwa kuzingatia ukweli huu. Uislamu umempa haki ya kutoa talaka lakini iwe inapokuwa hapana budi na iwe ni kwa wema na kwa kutekeleza masharti yaliyowekwa na sheria.

 


(b)Haki ya mke kumwacha mumewe
Ndoa katika Qur-an imeelezwa kuwa lengo lake ni kuleta upendo na huruma kati ya mume na mke - (Rejea Qur-an, 30:21). Endapo mwanamke ataona sababu za msingi ambazo, zinaifanya ndoa yao isifikie lengo hili, mwanamke anapewa uhuru wa kudai talaka kwa mumewe. Mumewe akimkatalia, anaruhusiwa mwanamke kwenda mbele ya vyombo vya Sheria ya Kiislamu na kudai talaka. Itabidi mume alazimishwe kutoa talaka iwapo vyombo hivi vya sheria vitashindwa kuwasuluhisha. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kumtaliki mumewe bila hata ya kukubaliana naye au kupitia mahakamani. Inawezekana hivi kwa namna mbili:

 


(i)Kama tangu mwanzo, katika kufunga mkataba wa ndoa mume alikubaliana na mkewe kuwa atakuwa na uhuru wa kuvunja ndoa, endapo mume atamfanyia au atafanya jambo fulani asilolipenda; basi atakapovunja ahadi hiyo, mkewe atakuwa na uhuru wa kumwacha bila ya kudai talaka kwake au mahakamani. Kwa maana nyingine mwanamume tangu mwanzo katika mkataba wao wa ndoa, amempa mkewe haki ya kumtalakisha, endapo atafanya au atamfanyia jambo fulani asilolipenda. Talaka ya ama hii huitwa "Khul".

 


(ii)Kama katika mkataba wa ndoa, mwanamume alitoa haki yake ya "kutamka" talaka na kumpa mkewe ili kumpa uhuru na uwezo zaidi wa kuvunja mkataba wa ndoa endapo ataona haifikii lengo lake.

 


(c)Kuvunja ndoa kwa makubaliano ya mume na mke:
Wakati mwingine, mume na mke wote baada ya kuona kuwa hawaishi kwa maelewano kama ilivyotarajiwa, wana uhuru wa kukubaliana kuachana kwa wema. Mahakama ya Kiislamu haitaingilia kati, labda itokee kuvunjwa kwa sheria nyingine kutokana na kuachana kwao huko. Ama hii ya Talaka huitwa "Mubarat".

 


(d)Haki ya Mahakama ya Kiislamu katika kuvunja Ndoa
Wakati mwingine, hata bila ya makubaliano ya mume na mke, mahakama ya Kiislamu ma uwezo wa kuvunja ndoa. Kwa mfano talaka ya ama ya "Li'aan" husimamiwa na serikali.

 

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/19/Friday - 06:17:44 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 969

Post zifazofanana:-

Je ni nani mwenye haki ya kutaliki
Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye. Soma Zaidi...

Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Talaka katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha. Soma Zaidi...

Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke. Soma Zaidi...

Zijuwe aina kuu 6 za talaka katika uislamu
Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu. Soma Zaidi...

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi Soma Zaidi...

Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake. Soma Zaidi...

Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu
Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi? Soma Zaidi...

Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa
Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii. Soma Zaidi...

Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu
Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili. Soma Zaidi...