image

Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Haki ya Kutaliki
Katika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Kalika sheria ya Klislamu haki ya kutoa talaka iko kwa wote, mume na mke.

 

(a)Haki ya Mume kutoa talaka
Ilivyo katika kawaida ya maumbile mwanamume ndiye anayeanza kutoa posa au pendekezo Ia kuoana. Katika sheria ya Kiislamu, mwanamume pia ndiye anayepaswa kutoa mahari kumpa anayemtaka waoane, ndiye mwenye jukumu Ia kumlisha mkewe na kukidhi haja zake zote, na ndiye kiongozi wa familia. Kwa kuzingatia ukweli huu. Uislamu umempa haki ya kutoa talaka lakini iwe inapokuwa hapana budi na iwe ni kwa wema na kwa kutekeleza masharti yaliyowekwa na sheria.

 


(b)Haki ya mke kumwacha mumewe
Ndoa katika Qur-an imeelezwa kuwa lengo lake ni kuleta upendo na huruma kati ya mume na mke - (Rejea Qur-an, 30:21). Endapo mwanamke ataona sababu za msingi ambazo, zinaifanya ndoa yao isifikie lengo hili, mwanamke anapewa uhuru wa kudai talaka kwa mumewe. Mumewe akimkatalia, anaruhusiwa mwanamke kwenda mbele ya vyombo vya Sheria ya Kiislamu na kudai talaka. Itabidi mume alazimishwe kutoa talaka iwapo vyombo hivi vya sheria vitashindwa kuwasuluhisha. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kumtaliki mumewe bila hata ya kukubaliana naye au kupitia mahakamani. Inawezekana hivi kwa namna mbili:

 


(i)Kama tangu mwanzo, katika kufunga mkataba wa ndoa mume alikubaliana na mkewe kuwa atakuwa na uhuru wa kuvunja ndoa, endapo mume atamfanyia au atafanya jambo fulani asilolipenda; basi atakapovunja ahadi hiyo, mkewe atakuwa na uhuru wa kumwacha bila ya kudai talaka kwake au mahakamani. Kwa maana nyingine mwanamume tangu mwanzo katika mkataba wao wa ndoa, amempa mkewe haki ya kumtalakisha, endapo atafanya au atamfanyia jambo fulani asilolipenda. Talaka ya ama hii huitwa "Khul".

 


(ii)Kama katika mkataba wa ndoa, mwanamume alitoa haki yake ya "kutamka" talaka na kumpa mkewe ili kumpa uhuru na uwezo zaidi wa kuvunja mkataba wa ndoa endapo ataona haifikii lengo lake.

 


(c)Kuvunja ndoa kwa makubaliano ya mume na mke:
Wakati mwingine, mume na mke wote baada ya kuona kuwa hawaishi kwa maelewano kama ilivyotarajiwa, wana uhuru wa kukubaliana kuachana kwa wema. Mahakama ya Kiislamu haitaingilia kati, labda itokee kuvunjwa kwa sheria nyingine kutokana na kuachana kwao huko. Ama hii ya Talaka huitwa "Mubarat".

 


(d)Haki ya Mahakama ya Kiislamu katika kuvunja Ndoa
Wakati mwingine, hata bila ya makubaliano ya mume na mke, mahakama ya Kiislamu ma uwezo wa kuvunja ndoa. Kwa mfano talaka ya ama ya "Li'aan" husimamiwa na serikali.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1157


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Fadhila za kufunga mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

Usimamizi wa Haki na haki za binadamu Katika Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana. Soma Zaidi...

Umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu
Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kuhiji, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

sunnah za swala
Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi. Soma Zaidi...

nini maana ya hadathi na ni zipi aina za hadathi na uchafu katika uislamu
Soma Zaidi...

Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran
Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo. Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

Haki na wajibu wa mke kwa mumewe na familia
Soma Zaidi...

Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10. Soma Zaidi...

Fadhila za usiku waalylat al qadir
Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000. Soma Zaidi...