picha

Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa

Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid

Dalili za kifafa 

  Kifafa kina dalili ambazo huonekana na mtu ukiziangalia unajua kuwa Ni mojawapo ya kifafa na dalili hizo Ni pamoja na;

 

1.mwenye kifafa lazima ataonyesha dalili ya kupoteza fahamu ; yaani hawezi kusikia,hawezi kuona, hawezi kusikia maumivu kwa huo muda yaani hatakuwa na ushirikiano wowote ule (unresponsive).

 

2.lazima atupe au kurusha rusha mikono na miguu,pamoja na kichwa kukigeuza geuza na huo muda mauvu anakuwa hasikii kabisa.

 

3.kuchanganyikiwa kwa mda

 

4.mate yenye mchanganyiko wa mapovu kutoka Mdomoni kwa huo muda aliopata kifafa( udenda)

 

5. Mwenye dalili za kifafa huwa anaduwaa kipindi kifafa kinamtokea.

 

  Sababu za kifafa

1.kurithi; kifafa huweza Kurithi kutoka kizazi hadi kizazi.

 

2.magonjwa ya kuambukiza Kama vile ukimwi,au uti wa mgongo huweza kusababisha kifafa.

 

3.madhara kwenye ubongo; Kama vile maji kujaa kwenye ubongo, uvimbe kwenye ubongo, bacteria na virusi vinavyoshambilia ubongo husababisha kifafa pia.

 

4. Kichwa kuumia (head injury) mfano ukipata ajali ya kichwa pia husababisha kifafa.

 

     Huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa

Kifafa huweza kutibiwa nyumbani na kupona Kama hakijawa sugu au ikiwa Ni kifafa kilichopo na huwa mnamfanyia huduma ya kwanza anapona , namna ya kumpatia huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa;

 

1.hakikisha sehemu aliyoangukia Ni Safi na Haina vitu vya kumuumiza ili anapopata fahamu asiwe na maumivu ya kuchomwa na kitu .

 

2.mgeuze mgonjwa alale upande (kiubavu) ili akicheua,akimeza mate au kutapika asipate shida maana yanaweza kurudi kwenye Koo la hewa na kumsababishia shida nyingine au yanaweza kumkaba.

 

3.mwekee kitu kilaini kwenye kichwa ili awe vizuri (comfortable).

 

4.mkague Kama amevaa hereni,cheni,au kitu kinachoweza kumuumiza umtoe .

 

5.mwache mgonjwa apate hewa watu wasimzunguke maana anaweza akakosa hewa.

 

6.usimzuie mgonjwa kurusha miguu na mikono hauruhusiwi kumshika mwache arushe akipata fahamu ataacha.

 

7. Usimpatie au kuweka chochote Mdomoni mwake Mana anawaze kutapika, kukabwa, au kurudi kwenye Koo la hewa na kupaliwa.

 

8.kaa na mgonjwa mapaka atakaporudi katika Hali yake na umuangalie yupo katika Hali gani Kama Ni mzuri au mbaya.

 

9kama mgonjwa Yuko katika Hali mbaya Sana au amechuku muda mrefu zaidj ya lisaa limoja haja pata fahamu fanya mipango sasa ya kumpeleka hospitali kwaajili ya matibabu .

 

Mwisho; Kama mgonjwa wa kifafa ndio Mara yake ya kwanza au ameanguka akachukua mda mrefu na Kama ana Hali ya kifafa na hajawahi kwenda hospitalini kwaajili ya uchunguzi Ni vyema kumpeleka akafanyiwe uchunguzi na vipimi na ushauri zaidi.

    

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/12/11/Saturday - 05:46:01 pm Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3654

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Umuhimu wa kupumzika kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupumzika kiafya, kwa kawaida mwili na viungo vingine vya mwili uweza kufanya kazi zaidi pale mtu akiwa amepumzika.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu.pua ni mlango wa fahamu ambao uhusika na kupumua.

Soma Zaidi...
Viwango vitatu vya kuungua.

Posti hii inahusu zaidi viwango vitatu vya kuungua. Ili tuweze kujua mtu ameunguaje Kuna viwango vitatu vya kujua kiasi na namna mtu alivyoungua

Soma Zaidi...
Upungufu was fati

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu was fati

Soma Zaidi...
Njia ambazo maradhi huambukizwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa

Soma Zaidi...
Vyakula vya madini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya madini mwilini

Soma Zaidi...
Huduma kwa watu waliodhani wamepatwa na maambukizi.

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo utolewa kwa watu wanaodhani wamepatwa na maambukizi ya virus vya ukimwi.

Soma Zaidi...
Msaada kwa wenye tonsils

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa wenye tonsils, kwa wale wenye tonsils wanapaswa kufanya yafuatayo ili kuweza kupambana na ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Nini husababisha kizunguzungu?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo mbalimbali ambayo husababisha kizunguzungu.

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng,area na wadudu

Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza kwa mtu aliyengatwa na wadudu. Wadudu ni viumbe vidogo ambavyo hukaa sehemu mbalimbali kama vile kwenye miti na sehemu kama hizo

Soma Zaidi...