picha

Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa

Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid

Dalili za kifafa 

  Kifafa kina dalili ambazo huonekana na mtu ukiziangalia unajua kuwa Ni mojawapo ya kifafa na dalili hizo Ni pamoja na;

 

1.mwenye kifafa lazima ataonyesha dalili ya kupoteza fahamu ; yaani hawezi kusikia,hawezi kuona, hawezi kusikia maumivu kwa huo muda yaani hatakuwa na ushirikiano wowote ule (unresponsive).

 

2.lazima atupe au kurusha rusha mikono na miguu,pamoja na kichwa kukigeuza geuza na huo muda mauvu anakuwa hasikii kabisa.

 

3.kuchanganyikiwa kwa mda

 

4.mate yenye mchanganyiko wa mapovu kutoka Mdomoni kwa huo muda aliopata kifafa( udenda)

 

5. Mwenye dalili za kifafa huwa anaduwaa kipindi kifafa kinamtokea.

 

  Sababu za kifafa

1.kurithi; kifafa huweza Kurithi kutoka kizazi hadi kizazi.

 

2.magonjwa ya kuambukiza Kama vile ukimwi,au uti wa mgongo huweza kusababisha kifafa.

 

3.madhara kwenye ubongo; Kama vile maji kujaa kwenye ubongo, uvimbe kwenye ubongo, bacteria na virusi vinavyoshambilia ubongo husababisha kifafa pia.

 

4. Kichwa kuumia (head injury) mfano ukipata ajali ya kichwa pia husababisha kifafa.

 

     Huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa

Kifafa huweza kutibiwa nyumbani na kupona Kama hakijawa sugu au ikiwa Ni kifafa kilichopo na huwa mnamfanyia huduma ya kwanza anapona , namna ya kumpatia huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa;

 

1.hakikisha sehemu aliyoangukia Ni Safi na Haina vitu vya kumuumiza ili anapopata fahamu asiwe na maumivu ya kuchomwa na kitu .

 

2.mgeuze mgonjwa alale upande (kiubavu) ili akicheua,akimeza mate au kutapika asipate shida maana yanaweza kurudi kwenye Koo la hewa na kumsababishia shida nyingine au yanaweza kumkaba.

 

3.mwekee kitu kilaini kwenye kichwa ili awe vizuri (comfortable).

 

4.mkague Kama amevaa hereni,cheni,au kitu kinachoweza kumuumiza umtoe .

 

5.mwache mgonjwa apate hewa watu wasimzunguke maana anaweza akakosa hewa.

 

6.usimzuie mgonjwa kurusha miguu na mikono hauruhusiwi kumshika mwache arushe akipata fahamu ataacha.

 

7. Usimpatie au kuweka chochote Mdomoni mwake Mana anawaze kutapika, kukabwa, au kurudi kwenye Koo la hewa na kupaliwa.

 

8.kaa na mgonjwa mapaka atakaporudi katika Hali yake na umuangalie yupo katika Hali gani Kama Ni mzuri au mbaya.

 

9kama mgonjwa Yuko katika Hali mbaya Sana au amechuku muda mrefu zaidj ya lisaa limoja haja pata fahamu fanya mipango sasa ya kumpeleka hospitali kwaajili ya matibabu .

 

Mwisho; Kama mgonjwa wa kifafa ndio Mara yake ya kwanza au ameanguka akachukua mda mrefu na Kama ana Hali ya kifafa na hajawahi kwenda hospitalini kwaajili ya uchunguzi Ni vyema kumpeleka akafanyiwe uchunguzi na vipimi na ushauri zaidi.

    

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3781

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Jinsi mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi

Post hii inahusu zaidi namna mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mimba kutungwa ni kitendo ambapo mbegu za kiume kuungana na yai la kike na kutengeneza zygote.

Soma Zaidi...
Kawaida Mtu anatakiwa na kiwango gani Cha presha

Nimeambiwa presha yangu umeshuka iko 90/60 na Nina umri wa miaka 26 KawaidaMtu anatakiwa na kiwango gani Cha presha

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma ya kwanza

Huduma ya kwanza ni huduma anayopewa mgonjwa au mtu yeyote aliyepata ajali kabla ya kumpeleka hospitalini

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyekazwa na misuli

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekazwa na misuli

Soma Zaidi...
Mambo yanayoweza kudhoofisha kinga ya mwili

Kinga ya mwili inapodhoofu mwili unakuwa hatarini kupata maradhi. Je unayajuwa mambo yanayodhoofisha kinga ysbmeili?

Soma Zaidi...
Zijue sababu za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo,ni sababu mbalimbali hasa za kiafya kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...