JINSI MIMBA INAVYOTUNGWA NA NAMNA AMBAVYO JINSIA YA MTOTO INAVYOTOKEA


image


Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaume  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.


KASORO KATIKA MFUMO WA UZAZI KWA MWANAUME 

1.kutokana na hapo awali tunaongelea kuhusu kutatua kasoro katika mfumo wa uzazi kwa upende wa mwanaume na mwanamke kasoro zipo nyingi .ila tuanze na kasoro kwa upende wa mwanaume ambapo  wanaume wengi upatwa na kasoro kadhaa katika mfumo wao moja ya kasoro ambayo uweza kuwapata wanaume ni ugumba .hii ni hali ya mwanaume kushindwa kutungisha mimba .

 

Ugumba kwa mwanaume hisababishwa na mambo mbalimbali ikiwemo kutoa mbegu ambazo zinakuwa chache sana hivo inapelekea kupunguza uwezekano kulifikia yai la mwanamke .kasoro nyingine ni kuwa na mbegu dhaifu ambazo zina upungufu kwa mfano kukosa mikia ,kuwa na mikia miwili ,kukosa kichwa au kuwa na umbo lisilo la kawaida yaani tunasema mbegu inakuwa haina umbo mahalamu kama mbegu zingine

 

Pia inapelekea kinga ya mwili inaweza kushambulia mbegu za kiume na hivyo kupunguza idadi yake vilevile kasoro nyingine korodani ya mwanaume hazitakuwa na uwezo wa kutengeneza mbegu za kiume kutokana na magonjwa au upungufu wa homoni .kasoro nyingine ya ugumba ni mirija ya kupitisha mbegu za kiume kuziba kutokana na magonjwa ya ngono kama ,vile kaswende na kisonono kwahiyo inashauriwa tusifanye ngono zembe bila kinga itatupelekea kupata matatizo ya ugumba  .na kama utaona hizo kasoro ina bidi kufika kituo cha hospitali kabla ya tatizo kuwa kubwa.tumeweza kuona hio kasoro kwa upende wa mwanaume.

 

2. Kutokana na kasoro hizo hii ni kasoro katika upande wa uzazi wa mwanamke  kama ilivyokuwa kwa mwanaume pia na mwanamke ana kasoro zake katika mfumo wake wa uzazi mojawapo ya kasoro ni ugumba kwa upande wake na tumeona mwanaume ana ugumba pia na mwanamke anaweza kuwa na ugumba unasababishwa na mambo mbalimbali ikiwemo mayai yake kushindwa kufanya kazi au kupevuka pia hali hii utokana matatizo ya utoaji wa homoni.

 

Matatizo hayo yanaweza kusababisha na tezi ya pituitari kushindwa kutoa homoni .vilevile,ovari kushindwa kutoa homoni ya oestrojeni au projesteroni ya kutosha .Adha ,ugumba unaweza kusababishwa na kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai kutokana na magonjwa ya ngono kama vile kisonono,kaswende na pangusa .

 

Magonjwa haya yanaweza kufanya mirija iwe myembamba au iwe na makovu hivyo kuzuia yai lisiweze kupita .vilevile ugumba kwa wamama  unaweza kusababiswa na uvimbe kwenye mji wa mimba ambapo hisababisha kiinitete kisiweze kujishikiza vizuri na hivyo usababisha matatizo ya mimba kutoka na hii shida ipo sana kwa wanawake kutokwa na mimba .

 

 Utatuzi wa kasoro katika mfumo wa uzazi.

Kutokana na hayo matatizo au kasoro za mfumo wa uzazi kwa mwanaume na mwanamke matatizo hayo yote yanatibika kama mtu atawahi kwenda kituo cha afya kupata matibabu na ushauri nasaha kwa madaktari pia na kumsikiliza na kwenda kuyafanyia kazi.

 

  JINSI YA  KUTUNGA MIMBA.                       1. Mwanaume na mwanamke wana huwezo wa kutunga mimba pale gameti za kike na za kiume kuungana au wengine wanasema ,zaigoti, wakati wa kujamiana mwanaume hutoa manii zenye gameti ume kutoka kwenye korodani kupitia mirija ya manii , urethra hadi uume .manii zenye gameti gameti ume huingia katika mwili wa mwanamke kupitia sehemu ya uke.mwanamke hutoa gameti uke kutoka kwenye ovari na kushuka kupitia mirija ya falopio.kama kama gameti ume zikiungana na gameti uke mimba utungwa .apo ndo jinsi mimba inatungwa kwa mwanaume na mwanamke  pia apo apo tunaweza kupata watoto

 

 Kuna njia za kupata au kutunga mimba ya pacha

1.hiii kwa jamii zingine zinaeleza kwamba ukipata pacha wawili nyie mnakuwa mna mikosi au mmeraniwa na mwenyezi mungu ambacho kitu sio cha ukweli kwahio inabidi jamii itambuwe kwamba watoto mapacha sio mikosi bali watoto mapacha wanapatikana pale.mwanamke anapojifungua mtoto mmoja kwa kila ujauzito .

 

Hata hivyo.mara chache mwanamke anaweza kujifungua wawili au zaidi kwa mpigo mmoja tu .mwanamke akijifungua watoto wawili au zaidi kwa ujauzito mmoja ,watoto hao huitwa pacha a aa. Pacha hao wanaweza kufanana au kutofanana.

 

Tuangalie kidogo apa jinsi ya mtoto kutokwa.Gameti uke kutoka kwenye ovari imebeba chembeuzi ya aina mmoja inayoitwa x hivyo,kila yai linalotoka tayari kwa kurutubishwa hubeba chembeuzi X.Gameti imebeba moja Kati ya chembeuzi za aina mbili yaani X au Y endapo chembeuzi X kutoka kwa mwanaume itakutana na chembe X  kutoka kwa mwanamke.mtoto wa kike hutungwa .

 

Kama chembeucheuzi Y kutoka kwa mwanaume itakutana na chembe X kutoka kwa mwanamke .mtoto wa kiume hutungwa .hivyo basi anayehusika na upatikanaji wa jinsi ya mtoto ni mzazi wa kiume.

 

 



Sponsored Posts


  👉    1 Jifunze fiqh       👉    2 Magonjwa na afya       👉    3 Mafunzo ya php       👉    4 Maktaba ya vitabu       👉    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       👉    6 Madrasa kiganjani    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Je chuchu zikiwa nyeusi Nini kinasababisha,, kando ya kuwa mjamzito? Na Kama sio mjamzito sababu ya chuchu kua nyeusi ni nini
Chuchu kubadilika range ni mojavkatika mabadiliko ambayo huwapa shoka wengi katika wasichana. Lucinda nikwambie tu kuwa katika hali ya kawaida hilo sio tatizo kiafya. Soma Zaidi...

image Mambo muhimu kuhusu mbegu za kiume
Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutokutunza vizuri mbegu za kiume. Soma Zaidi...

image Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo. Soma Zaidi...

image Kwa nini hujapata siku zako za hedhi.
Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako. Soma Zaidi...

image Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?
Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito. Soma Zaidi...

image mpenzi wangu nimeshiriki nae tendo la ndoa akiwa siku zake za hatar kwa siku 3 lakin hajashika mimba tatizo linaweza kuwa ni nini?
Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili. Soma Zaidi...

image Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa
Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mara nyingi kwenye kifua, pelvis au matako. Mapacha walioungana wanaweza pia kushiriki kiungo kimoja au zaidi cha ndani. Mapacha wengi walioungana huzaliwa wakiwa wamekufa au hufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa. Baadhi ya mapacha waliosalia walioungana wanaweza kutenganishwa kwa upasuaji. Mafanikio ya upasuaji wa kutenganisha mapacha walioungana inategemea mahali ambapo mapacha wameunganishwa na wangapi na viungo gani vinashirikiwa, na pia juu ya uzoefu na ujuzi wa timu ya upasuaji. Soma Zaidi...

image Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi. Soma Zaidi...

image Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtoto zaidi. Soma Zaidi...

image Nimegundua ni mjamzito na kibaya zaid namtoto mchanga nimefanyiwa opaleshen naomba ushauli wako mkuu
Inatakiwa angalau nafasivkati ya mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Soma Zaidi...