Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

4. Swala ya Tahajjud

Swala ya Tahajjud ni miongoni mwa swala zilizokokotezwa sana katika Qur-an na Hadithi. Neno “Tahajud” lina maana ya kuamka kutoka usingizini. Swala hii huswaliwa usiku wa manane, hasa katika theluthi ya mwisho wa usiku karibu na al-Fajiri.

 


Swala hii vile vile hujulikana kwa jina la “Qiyaamul-layl”. Yaani kisimamo cha usiku kwa sababu inakuwa na visimamo virefu ambapo Qur-an husomwa kwa urefu. Mkokotezo wa swala ya Tahajjud unadhihirika katika aya za Qur-an zifuatazo:

 

Na katika usiku jiondoshee usingizi (kid ogo) kwa (kusoma) hiyo (Qur-an ndani ya Swala).Hiyo ni (Ibada) zaidi kwako. Huwenda Mola wako akakuinua cheo kinachosifika. (17:79).

 


Miongoni mwa sifa za waja wema wa Allah (s.w) ni pamoja:

 

“Na wale wanaopitisha baadhi ya saa za usiku kwa ajili ya Mola wao kwa kusujudu na kusimama ”. (25:64).
J e , afanyaye ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama na kuogopa Akhera na kutarajia rehema ya Mola wake (ni sawa na asiyefanya hayo)? Sema: “Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu. (39:9)

 

Pia Mtume (s.a.w) amekokoteza Swala za Usiku kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo.

 


Abu Umamah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Jizoesheni kusimama Usiku (kwa swala) kwa sababu ilikuwa ndio tabia ya Wacha-Mungu w aliokutangulieni na ni njia ya kukukurubisheni karibu na Mola wenu na ni njia ya kufutiwa dhambi na ni kizuizi cha kutenda maovu (dhambi)”. (Tirmidh).

 


Idadi ya rakaa alizoswali Mtume (s.a.w) katika hii swala ya Tahajjudi ni nane (8) na kisha akamalizia na rakaa tatu za Witri. Katika hizi rakaa nane alitoa salam kila baada ya rakaa mbili. Mtume (s.a.w) alikuwa akisoma Qur-an kwa kitambo kirefu kwa kila rakaa kiasi kwamba miguu yake ilikuwa inavimba kama tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:-

 


“Mughirah (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama katika (sw ala ya usiku) kwa kitambo kirefu kiasi kw amba miguu yake ilivimba, akaulizwa: Kwanini unafanya hivi ambapo umesamehewa dhambi zako zilizotangulia na zitakazokuja? Akauliza: “Nisiwe mja mwenye Shukrani?” (Bukhari na Muslim).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 5968

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 web hosting    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran

Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo.

Soma Zaidi...
Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga.

Soma Zaidi...
Wanaostahiki kupewa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...