Menu



Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

7.Swalatudh-Dhuhaa

Swala ya Dhuhaa ni sunnah inayoswaliwa kati ya kipindi cha baada ya jua kupanda juu kiasi cha mita tatu hivi na kabla ya jua kufikia katikati. Lakini ni bora kuswali katikati ya kipindi hicho.

 


Swala hii inaswaliwa kwa rakaa mbili mbili hadi zitimie nane, lakini kwa uchache unaweza kuswali rakaa mbili tu na pia unaweza kuswali zaidi ya rakaa nane.


Umuhimu wa swala ya Dhuhaa uko wazi. Kipindi kati ya swala ya Alfajir na Dhuhuri ni kirefu sana kiasi kwamba mja anaweza kusahau kumkumbuka na kumtaja Allah (s.w). Kama tunavyofahamu kumkumbuka Allah (s.w) kila wakati ndio ngao pekee ya kumzuia mja na mambo maovu na machafu. Hivyo Swalatudh-Dhuhaa kwa mtu mwenye wasaa katika kipindi hicho cha harakati nyingi za kutafuta riziki, itampa msukumo mpya wa kumkumbuka na kumuabudu Allah ipasavyo.

 


Kutokana na hadith iliyopokelewa na Abu Daud na Ahmad, Buraidah (r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Katika mwili wa binaadam kuna viungo (joints) 360 na binaadam ni lazima akitolee sadaka kila kiungo kimoja”. Watu wakauliza:“Nani awezaye kufanya hivyo ewe Mjumbe wa Allah?”Mtume akawajibu: “Mtu anaweza kufanya hivyo kwa kuondosha kitu chenye madhara njiani. Na iwapo hatoweza, kufanya hivyo basi rakaa mbili za Dhuhaa zitamtosheleza ”.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2914

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutwaharisha Aina mbalimbali za Najisi katika uislamu

Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuosha maiti wa kiislami mwanaume au mwanamke

Post hii inakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kumuosha maiti wa kiislamu

Soma Zaidi...
maana ya uchumi kiislamu

Maana ya UchumiMfumo wa maisha wa Kiislamu humuelekeza binaadamu kujenga na kudumisha uhusiano wake na Al-lah (s.

Soma Zaidi...
Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume.

Soma Zaidi...