image

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

7.Swalatudh-Dhuhaa

Swala ya Dhuhaa ni sunnah inayoswaliwa kati ya kipindi cha baada ya jua kupanda juu kiasi cha mita tatu hivi na kabla ya jua kufikia katikati. Lakini ni bora kuswali katikati ya kipindi hicho.

 


Swala hii inaswaliwa kwa rakaa mbili mbili hadi zitimie nane, lakini kwa uchache unaweza kuswali rakaa mbili tu na pia unaweza kuswali zaidi ya rakaa nane.


Umuhimu wa swala ya Dhuhaa uko wazi. Kipindi kati ya swala ya Alfajir na Dhuhuri ni kirefu sana kiasi kwamba mja anaweza kusahau kumkumbuka na kumtaja Allah (s.w). Kama tunavyofahamu kumkumbuka Allah (s.w) kila wakati ndio ngao pekee ya kumzuia mja na mambo maovu na machafu. Hivyo Swalatudh-Dhuhaa kwa mtu mwenye wasaa katika kipindi hicho cha harakati nyingi za kutafuta riziki, itampa msukumo mpya wa kumkumbuka na kumuabudu Allah ipasavyo.

 


Kutokana na hadith iliyopokelewa na Abu Daud na Ahmad, Buraidah (r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Katika mwili wa binaadam kuna viungo (joints) 360 na binaadam ni lazima akitolee sadaka kila kiungo kimoja”. Watu wakauliza:“Nani awezaye kufanya hivyo ewe Mjumbe wa Allah?”Mtume akawajibu: “Mtu anaweza kufanya hivyo kwa kuondosha kitu chenye madhara njiani. Na iwapo hatoweza, kufanya hivyo basi rakaa mbili za Dhuhaa zitamtosheleza ”.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2064


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Ni nini maana ya uchumi katika uislamu
Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi. Soma Zaidi...

Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu. Soma Zaidi...

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Soma Zaidi...

Twahara na namna ya kujitwaharisha, nguzo zake na sunna zake
Soma Zaidi...

Ni mali ipi inatakiwa kutolewa zaka?
Soma Zaidi...

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija
Soma Zaidi...

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii
(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi. Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

Hukumu na taratibu za mirathi na kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...

Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno
Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana. Soma Zaidi...

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI SWALA YA IJUMAA, JENEZA, SWALA YA JAMAA NA SWALA YA SUNNHA (tarawehe, tahajudi na qiyamu layl)
1. Soma Zaidi...