JINSI YA KUMUANDAA MAITI BAADA YA KUFA


image


Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.


Mambo Anayofanyiwa Mtu mara tu baada ya Kufa

Baada ya kushuhudia kuwa ndugu yetu ameshakata roho vyema tuseme na kuzingatia maneno yafuatayo kama alivyotufahamisha Allah (s.w)
“... Hakika sisi ni wa Allah na kwake tutarejea ...” (2:156).

 


Maneno haya ni ya msingi sana katika hali hii ya kufiwa, kwani yanawaliwaza wafiwa na kuwaepusha na fadhaa zinazoweza kutokea juu ya kifo cha marehemu. Ukizingatia maneno ya aya hii utaona kuwa kwa vyovyote iwavyo, kurejea kwa Allah ni jambo lisilozuilika. Hivyo, chochote kile kitakachokuwa ndio sababu ya kifo cha marehemu kitakuwa ni sababu tu ya kifo hicho aliyoiweka Allah (s.w)

 


Baada ya maliwazo haya maiti ile yapasa kufanyiwa yafuatayo:

 

1. Kwa taratibu rudishia mdomo usibakie wazi kwa kufunga kidevu kwa kitambaa na kukizungushia kichwani.

 


2. Funga macho ya marehemu kwa taratibu na huku ukisoma:

 


“Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah. Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake baadaye. Na jaalia atakayokutana nayo yawe bora kuliko aliyoachana nayo”.

 


3. Lainisha viungo vya maiti kwa kukunja na kukunjua pole pole sehemu zote zenye viungo katika mikono na miguu. Kama patakuwa na ugumu wowote katika kumnyoosha viungo hivyo, maji ya moto au mafuta yanaweza kutumika ili kulainisha. Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na alazwe huku uso ukielekea Qibla kwenye kitanda kisichokuwa na godoro.

 


4. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo kisha kumgubikwa kwa shuka kubwa, pia ni vyema afungwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu chenye uzito kidogo juu ya tumbo ili lisifutuke sana.

 


5. Marashi na ubani vitumike sana mahali alipo maiti ili kuzima harufu ya uvundo itokayo kwa maiti.Mwanaadamu ni msafi sana anapokuwa hai. Lakini muda mfupi tu baada ya kufa huanza kutoa harufu kali ya uozo.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...

image Tarstibu za kulipa swaumu ya Ramadhani
Hapa utajifunza namna ambayo utatakiwa kulipa funga ya Ramadhani kwa siku ambazo hukufunga Soma Zaidi...

image Nini maana ya kusimamisha swala?
Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu? Soma Zaidi...

image Fadhila za usiku waalylat al qadir
Zijuwe fadhila za usiku wenye cheo kuliko nyusiku ya miezi 1000. Soma Zaidi...

image Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa
Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

image Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu. Soma Zaidi...

image Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir Soma Zaidi...

image Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

image Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?
Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha. Soma Zaidi...