image

Kisiwa cha uokozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za safari saba za Sinbad

KISIWA CHA UOKOZI

Nilikwenda mpaka nikakuta misitu minene na nisijuwe pa kuenda. Kwa ghafla nikasikia sauti za watu wanaowinda na kwa uchovu nilonao nilianguka chini na kwa njaa nilonayo nilipootelewa na fahamu. Hapo sikujuwa kilichoendelea hata nikashituka nipo kwenye kitanda safi na pembeni kuna binti mzuri ananiwekea chakula tayari kwa kuniamsha ili nipate kula chakula. Bila hata kujaribu kuniamsha niliamka kwa upole na kumuuliza swali “eti unaitwa nani, na nimefikaje hapa?”. “naitwa ‘Aisha ni mtoto wa mfalme, umeokotwa porini na baba alipokuwa akiwinda”. Ni maneno aliyoyasema bint Aisha mtoto mfalme.

 

Nikanawa maji tayari kwa kuanza kula, baada ya muda wa dakika takriban 10 aliingia mfalme, na nilimtambua kwa mavazi yake. Baada ya utambulisho nikawaelezea kila kilichonikuta. Na akazungumza kuwa kwa uda wa miaka 10 wamekuwa wakikitafuta kijiji hiko bila mafanikio. Inadaiwa kuwa wakazi wa kijiji hiko sio watu wa kawaida hivyo walishangaa kuniona mimi nimeweza kutoroka kwenye kijiji kile kisichofikika. Basi mfalme aliniuliza mengi kuhusu Baghadad na bila kusita nikawa namjibu kwa uwazi kabisa. Kwa hakika alivutiwa sana na majibu yangu.

 

Mfalme alinitambulisha kwenye baraza lake na kunifanya mimi mmoja ya washauri wake na watu wa karibu. Niliishi pale kwa muda wa wiki moja hata siku hiyo baada ya swala ya magharibi nikasikia mlango unagongwa. Nikaenda kufunguwa nikamkuta mfalme na mkewake. Kwa heshima kubwa nikawakaribisha na walionesha uso wa furaha hata nisiijue sababu ya ujio wao. Baada ya kuwapatia maji ya kunywa mfalme akaanza kuzungumza.

 

“mwanangu, ujio wetu hapa mimi na mama yako ni kutaka ushauri wako. Kama ujuavyo sisi tuna mtoto mmoja tu naye ni wa kike. Pia binti yetu ameonesha kuvutiwa sana na wewe. Hivyo tumekuja kukuomba uwe mkwe wetu na mrithi wa utawala huu baada ya kufa kwangu”. Kimoyoni nilifurahi sana japo nikamwambia mfalme “nashukuru sana kwa maneno yako baba yangu mtukufu mfalme. Naomba muda nifikirie na nitakujibu baada ya mshuko wa swala ya ijumaa keshokutwa in shaa Allah” Basi mfalme akakubali kunipa muda ule na kuondoka.

 

Nilitafakari sana nini nifanye na nikikubali kuoa pale nitaondoaje kwenda Baghadad. Nitakuwa mkwe na mtoto wa kiume wa mfalme, na nitatakiwa kuurithi ufalme ule, hivyo ndoto zangu za akurudi nyumbani zitakuwa zimekwisha. Siku ilofata asubuhi nikaenda kwa rafiki yangu ambaye mkewe alikuwa akiumwa na tumbo. Nikaenda kumuomba ushauri lakini nikamkuta analia sana. Sikuweza kumuomba tena ushauri badala yake nikamuuliza kinachomliza zaidi. “rafiki yangu, tambuwa kuwa katika nchi yetu hii, akifa mke mume atazikwa pamoja na mkewe akiwa hai, na akifa mume mke atazikwa na mkewe akiwa hai. Hivyo nalia kama mke wangu akifa na mimi ndo mwisho wangu.

 

Niliposikia maneno yale pale moyo wnagu ulipasuka na kudunda haraka. Nikaanza kutetemeka miguu na meno. Jasho jingi lilinitoka japo kulikuwa na baridi wakati ule. Yote hayo yalitokea nilipokuwa nawaza nni nitamjibu mfalme. Maana nikikubali kuoa nikifa mimi wa kwanza sio taabu ana ila akitangulia kufa mtoto wa mfalme nitazikwa pamoja naye nikiwa hai. Mawazo haya yaliniumiza sana hata nikakosa hamu ya kula kabisa. Jioni ile mmnikapita nyumbani kwa mfalme na kumkuta binti yake akiumwa eti amekataa kula mpaka asikie jibu langu kwanza.

 

Hali ile ikazidi kuniogopesha zaidi pale niliposikia kuwa binti mafalme ameahidi kujiuwa kama nitamkataa. Nikaogopa zaidi niliposikia hivi. Nilijihisi uchovu na nikaelekea nyumbani kulala. Siku ilofata ilikuwa ndio siku ya ijumaa ambapo mfalme nimemuahidi kumpatia jibu juu ya kumuoa mwanae. Niliamka mapema sana siku ile na kuoga kisha nikaenda msikitini na kuwahi mstari wa mbele. Niliswali rakaa mbili na kufanya istikhara yaani kumuomba Mungu anipe majibu ya maswali yangu.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1508


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya chongo wa tatu mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa pili mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI YA MFALME NA WAZIRI WAKE
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MFALME NA WAZIRI WAKE Basi tambueni enyi rafikizangu kuwa mimi na waziri wangu huyu hatutokani na familia za kifalme wala mimi baba yangu hahusiani hata kidogo na ufalme. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA WANAWAKE WATATU NA CHONGO WATATU
Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

MFUGAJI NA MKEWE
Download kitabu Hiki Bofya hapa KISA CHA MFUGAJI NA MKEWE. Soma Zaidi...

Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya Khalid mwenye kuneemeshwa na Jalid
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA SAFARI SABA ZA BAHARIA SINBAD
SAFARI SABA ZA SINBADKatika nchi ya Baghdad kulikuwepo na kijana aliyejulikana kama Sinbad mbeba mizigo. Soma Zaidi...

Hadithi ya jini na mfanya biashara
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya chongo wa kwanza mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...