KIUNGULIA NA TIBA ZAKE KWA WAJAWAZITO.


image


Posti hii inahusu kiungulia kwa wanawake wajawazito na tiba yake, ni ugonjwa au hali inayowapata wajawazito walio wengi kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito.


Kiungulia na tiba zake kwa wajawazito.

1. Kwanza kabisa kiungulia uwapo wanawake wajawazito wakiwa kwenye wiki kuanzia ya thelathini mpaka arobaini,hali huu utokea kwa sababu progesterone homoni inalegeza cardiac sphincter za tumboni  na kusababisha acid kurudi kwenye oesophagus na kusababisha kiungulia, kwa hiyo wajawazito walipatwa na hali kama hizi hawapaswi kuogopa au kuwa na wasiwasi wajue kuwa ni kitu cha kawaida utokea na uisha tu baada ya kujifungua. Na pia wauguzi wanapaswa kuwaambia wazi wajawazito ili watambue Dalili kama hizi wakati wa ujauzito.

 

2. Hili kupunguza hali hii ya kiungulia wanawake wenye mimba wanapaswa kuepuka  kuinama kwa mda mrefu  wakati wanapokuwa wanafanya kazi zao za kila siku, kwa hiyo wanapaswa kujua hali yao kwa hiyo ni vizuri kufanya kazi wakiwa wamesimama pindi wakisikia hali ya kiungulia au wanaweza kuwekewa kiti au meza wakati wa kufanya kazi kama vile kuosha vyote na kufua wakafanya wakiwa wamesimama na pia wote waliowazunguka wanapaswa kujua hali huu na kuwasaidia akina mama wajawazito ili waweze kufanya kazi zao bila kuinama.

 

3. Kama hali ya kiungulia imezidi sana wajawazito wanapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa siku ili kuepuka hali ya kupata kiungulia kwa mfano anaweza kula saa mbili, saa nne, saa sita, saa nane, saa kumi, saa kumi na mbili na kuendelea mpaka mda wa kulala, kwa kufanya hivyo anaweza kuepuka kupata kiungulia mara kwa mara, nimesema hivyo kwa sababu kuna akina mama wajawazito wanaopata kiungulia cha hali ya juu sana kuliko wengine na pia watu wa karibu wanapaswa kujua hili na kuona kuwa ni hali ya kawaida na kuendelea kumjali Mama katika kupambana na hali yake ya mda mfupi tu.

 

4. Pia wanawake wajawazito wanapaswa kulala wakiwa na mito ya kutosha ili kuepuka kiungulia na pia wajawazito kama hawajalala na mito ya kutosha wanaweza kuteseka sana wakati wa usiku au mda wowote wa kupumzika kwa hiyo wauguzi na wataalam wengine wa afya wanapaswa kumweleza mama huduma hii ya kutumia mito ili kupunguza kuwepo kwa kiungulia na pia watu wa karibu wa Mama mjamzito wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mito kadiri ya uhitaji.

 

5. Pia hali huu ya kiungulia ikizidi hata kama ni kawaida kwa wajawazito wanaweza kwenda hospitalini, kwa maana kuna dawa ambazo utibu ugonjwa huu dawa hizi ni kama vile  anti acid na sawa nyingine kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, kwa hiyo tunapaswa kuwaambia ukweli pale hali ikizidi wajawazito wanapaswa kwenda hospitalini kupata dawa za kuwatuliza hali zao.

 

6. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa wanawake wenye mimba Upata magonjwa madogo madogo kama kiungulia na wanapaswa kupata huduma za muhimu kwao kwa hiyo jamii inapaswa kuwaelewa na kuwahudumia kwa kadiri inavyowezekana na kuwa pamoja nao kwa sababu haya matatizo madogo kama kiungulia ni ya mda tu na Mama akijifungua yanapotea mara moja.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    4 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya php    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Dalili za mimba ya siku 4
Unaweza kutaka kujuwa je naweza kupata dalili za mimba baada ya siku nne toka ujauzito kutungwa? ama baada ya siku nne toka kushiriki tendo la ndoa. Makala hii itakwenda kujibu maswali haya na mengineyo. Soma Zaidi...

image Huduma ya Kwanza kwa aliyeng'atwa na nyuki
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyuko Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa degedege na dalili zake
Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa kuungua Mdomo (mouth burning syndrome)
Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuwaka moto mara kwa mara mdomoni bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea ya mdomo wako wote. Ugonjwa wa mdomo unaoungua hutokea ghafla na unaweza kuwa mbaya. Soma Zaidi...

image Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke Soma Zaidi...

image Zijue hasara za magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi hasara za magonjwa ya ngono, ni magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana bila kutumia kinga. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa Kuvimba ubongo (Encephalitis)
Post hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa ubongo ambao kitaalamu huitwa Encephalitis, Ni Maambukizi ya virusi ni sababu ya kawaida ya hali hiyo. Ugonjwa wa Kuvimba ubongo unaweza kusababisha dalili zinazofanana na Homa, kama vile Homa au maumivu makali ya kichwa. Inaweza pia kusababisha mawazo kuchanganyikiwa, mishtuko ya moyo, au matatizo ya hisi au harakati. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili inavyoshambulia ini.
Ugonjwa huu hupelekea kuvimba kwenye ini yako ambayo hutokea wakati mfumo wa kinga ya mwili wako unaposhambulia ini lako. Soma Zaidi...

image Makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu Soma Zaidi...