Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuandaliwa Muhammad (s.a.w) kabla ya kupewa Utume.
- Maandalizi (mafunzo) haya yalikuwa ya Kiil-hamu ambayo hata Muhammad mwenyewe na jamii haikujua kuwa anaandaliwa, na yalikuwa kama ifuatavyo;
- Kuzaliwa katika kabila tukufu la Kiqureish ambalo ni kizazi cha Nabii Ibrahim (a.s) kupitia kwa Nabii Ismail (a.s).
Rejea Qur’an (2:129).
- Kupewa jina la Muhammad na babu yake lililo na maana sawa na ‘Ahmad’- Mshukuriwa, alilotabiriwa nalo katika Injili, na Qur’an pia.
Rejea Qur’an (61:6).
- Malezi bora aliyopata kupitia Mama yake mzazi, Bi Halimah, babu yake Abdul-Muttalibu na Ami ya Abu Talibu pamoja na kuwa alikuwa yatima.
Rejea Qur’an (93:6).
- Tabia yake njema isiyo na mfano kuanzia utotoni hadi utuuzima wake kutoathiriwa na kila aina ya ubaya.
Rejea Qur’an (68:4).
- Ndoa yake Muhammad (s.a.w) na Bi Khadija bint Khuwailid, aliiandaa Allah (s.w) ili kumuwezesha Muhammad kuitumikia jamii hata kabla ya utume.
Rejea Qur’an (93:8).
- Kuchukia kwake maovu na kujitenga pangoni ili kutafuta msaada ulio nje ya uwezo wa kinaadamu baada ya kufanya jitihada mwisho wa uwezo wake.
Rejea Qur’an (93:7) na (94:1-3).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
tarekh11
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.
Soma Zaidi...