picha

Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

-    Maandalizi (mafunzo) haya yalikuwa ya Kiil-hamu ambayo hata Muhammad mwenyewe na jamii haikujua kuwa anaandaliwa, na yalikuwa kama ifuatavyo;

 

  1. Kuzaliwa katika kabila tukufu la Kiqureish ambalo ni kizazi cha Nabii Ibrahim (a.s) kupitia kwa Nabii Ismail (a.s).

Rejea Qur’an (2:129).

 

  1. Kupewa jina la Muhammad na babu yake lililo na maana sawa na ‘Ahmad’- Mshukuriwa, alilotabiriwa nalo katika Injili, na Qur’an pia.

   Rejea Qur’an (61:6).

 

  1. Malezi bora aliyopata kupitia Mama yake mzazi, Bi Halimah, babu yake Abdul-Muttalibu na Ami ya Abu Talibu pamoja na kuwa alikuwa yatima.

Rejea Qur’an (93:6).

 

  1. Tabia yake njema isiyo na mfano kuanzia utotoni hadi utuuzima wake kutoathiriwa na kila aina ya ubaya.

Rejea Qur’an (68:4).

 

  1. Ndoa yake Muhammad (s.a.w) na Bi Khadija bint Khuwailid, aliiandaa Allah (s.w) ili kumuwezesha Muhammad kuitumikia jamii hata kabla ya utume.

Rejea Qur’an (93:8).

 

  1. Kuchukia kwake maovu na kujitenga pangoni ili kutafuta msaada ulio nje ya uwezo wa kinaadamu baada ya kufanya jitihada mwisho wa uwezo wake.

   Rejea Qur’an (93:7) na (94:1-3).

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 1823

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
Kifo cha Nabii Sulaiman

Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine.

Soma Zaidi...
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Jitihada alizozifanya Khalifa wa Tatu katika kuilinda Quran

Soma Zaidi...