Kumsaidia sliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo
Posti hii inahusu namna ya kumsaidia mgonjwa aliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo.
Namna ya kumsaidia aliyepungukiwa na damu kwas sababu ya kuwepo kwa minyoo.
1. Kwanza tibu tatizo la upungufu wa damu kwa kutumia vyakula vyenye madini ya chuma na vyakula vyenye protini, kwa kutumia vyakula hivi damu inaweza kuongezeka kwa haraka zaidi kuliko kawaida,maana hata kama shida ni minyoo Anemia ndiyo inapaswa kutibiwa haraka kwa sababu damu ikipungua sana inaweza kuleta shida.
2. Kama Kuna dalili zozote za Anemia na zinaonekana wazi, inabidi kuangalia wingi wa damu na kuona kiasi kilichomo kama kiasi Cha wingi wa damu ni zaidi ya 5g/l vyakula na dawa mbalimbali vinaweza kutumika Ili kuongeza damu na mboga mboga za majani zinaweza kutumika Ili kuongeza damu, kama kiwango Cha damu ni Chini ya 5g/l mgonjwa inabidi aongezewa damu mara Moja. Tujue kuwa damu ni muhimu kwa binadamu kwa hiyo ni muhimu kuongeza mara Moja ikiisha.
3. Baada ya kuongeza damu mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuondoa minyoo kama vile mebendazole na albendazole hizi dawa zinapaswa kutumiwa kwa maagizo ya wataalamu wa afya na sio kutumia dawa tu, na tujue mtu akiwa anatumia dawa za minyoo hapaswa kunywa pombe maana ni hatari kwa kuchanganya dawa za minyoo na pombe.
4.Baada ya kumpatia mgonjwa dawa uangalizi unapaswa kuwepo Ili kuhakikisha kuwa mgonjwa anapona kabisa na pia mgonjwa anapaswa kupima wingi wa damu Ili kuangalia kama kiwango Cha damu mwilini kipo kwenye hali ya kawaida kabla hajaruhisiwa kutoka hospitalini, na pia mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuongeza damu na kutumia vyakula vyenye wingi wa protein na vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma.
5. Elimu inabidi utolewa kwa mgonjwa na wote waliomzunguka kuhusu namna ya kujikinga na ugonjwa wa upungufu wa damu hasa kuhusu namna ya kupambana na minyoo kwenye mazingira na kuchimba choo, kunywa maji masafi,kuepuka kucheza kwenye maji yaliyotuhama hasa kwa watoto wadogo na kutumia dawa za minyoo kwa mda Ili kama Kuna Aina yoyote ya minyoo itaondoka na kiwango Cha damu kitakuwa kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dalili za maambukizi kwenye figo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.
Soma Zaidi...Dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanawake
Somo hili linakwenda kukuletea dalili za fangasi wa sehemu za Siri kwa wanawake
Soma Zaidi...Njia ambazo VVU huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
Soma Zaidi...Watu walio hatarini kupata UTI
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI
Soma Zaidi...Namna ya kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Posti hii inahusu zaidi njia zinazotumika ili kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu
Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.
Soma Zaidi...