Kumsaidia sliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo
Posti hii inahusu namna ya kumsaidia mgonjwa aliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo.
Namna ya kumsaidia aliyepungukiwa na damu kwas sababu ya kuwepo kwa minyoo.
1. Kwanza tibu tatizo la upungufu wa damu kwa kutumia vyakula vyenye madini ya chuma na vyakula vyenye protini, kwa kutumia vyakula hivi damu inaweza kuongezeka kwa haraka zaidi kuliko kawaida,maana hata kama shida ni minyoo Anemia ndiyo inapaswa kutibiwa haraka kwa sababu damu ikipungua sana inaweza kuleta shida.
2. Kama Kuna dalili zozote za Anemia na zinaonekana wazi, inabidi kuangalia wingi wa damu na kuona kiasi kilichomo kama kiasi Cha wingi wa damu ni zaidi ya 5g/l vyakula na dawa mbalimbali vinaweza kutumika Ili kuongeza damu na mboga mboga za majani zinaweza kutumika Ili kuongeza damu, kama kiwango Cha damu ni Chini ya 5g/l mgonjwa inabidi aongezewa damu mara Moja. Tujue kuwa damu ni muhimu kwa binadamu kwa hiyo ni muhimu kuongeza mara Moja ikiisha.
3. Baada ya kuongeza damu mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuondoa minyoo kama vile mebendazole na albendazole hizi dawa zinapaswa kutumiwa kwa maagizo ya wataalamu wa afya na sio kutumia dawa tu, na tujue mtu akiwa anatumia dawa za minyoo hapaswa kunywa pombe maana ni hatari kwa kuchanganya dawa za minyoo na pombe.
4.Baada ya kumpatia mgonjwa dawa uangalizi unapaswa kuwepo Ili kuhakikisha kuwa mgonjwa anapona kabisa na pia mgonjwa anapaswa kupima wingi wa damu Ili kuangalia kama kiwango Cha damu mwilini kipo kwenye hali ya kawaida kabla hajaruhisiwa kutoka hospitalini, na pia mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuongeza damu na kutumia vyakula vyenye wingi wa protein na vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma.
5. Elimu inabidi utolewa kwa mgonjwa na wote waliomzunguka kuhusu namna ya kujikinga na ugonjwa wa upungufu wa damu hasa kuhusu namna ya kupambana na minyoo kwenye mazingira na kuchimba choo, kunywa maji masafi,kuepuka kucheza kwenye maji yaliyotuhama hasa kwa watoto wadogo na kutumia dawa za minyoo kwa mda Ili kama Kuna Aina yoyote ya minyoo itaondoka na kiwango Cha damu kitakuwa kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 web hosting π3 Kitau cha Fiqh π4 kitabu cha Simulizi π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.
Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...Homa za mara kwa mara: Chanzo chake na nini cha kufanya.
Homa sio ugonjwa; ni silaha ya mwili wako. Inapopanda, inamaanisha mfumo wako wa kinga unawaka moto kupambana na adui aliyepo ndani. Lakini, je, inakuwaje unapopata homa hizo mara kwa mara? Homa za mara kwa mara ni kengele ya onyo kwamba kuna kitu hakiko sawa ambacho hakijatibiwa kikamilifu. Makala haya yanakusaidia kutambua nini cha kufanya ili kuondokana na mzunguko huu wa maumivu
Soma Zaidi...Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?
Dalili za mimba zinaweza kuanzia kuonekana mapema ndani ya wiki ya kwanza, japo sio rahisi nabhakuna uthibitishobwa uhakika juu ya kauli hii. Makala hii itakwebda kujibubswali la msingi la muuulizaji kama maumivu ya tumbo ni dalili ya ujauzito.
Soma Zaidi...Chakula kinachosaidia kupunguza gesi tumboni.
βGesi tumboni (bloating au flatulence) ni tatizo la kawaida linaloweza kusababisha usumbufu mkubwa na kupoteza kujiamini. Makala haya yanachunguza kwa kina vyakula bora vinavyosaidia kupunguza uzalishaji wa gesi, kuelezea sayansi nyuma ya usagaji chakula, na kutoa mikakati ya lishe kwa maisha yenye afya na utulivu wa tumbo.
Soma Zaidi...