Kumsaidia sliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo
Posti hii inahusu namna ya kumsaidia mgonjwa aliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo.
Namna ya kumsaidia aliyepungukiwa na damu kwas sababu ya kuwepo kwa minyoo.
1. Kwanza tibu tatizo la upungufu wa damu kwa kutumia vyakula vyenye madini ya chuma na vyakula vyenye protini, kwa kutumia vyakula hivi damu inaweza kuongezeka kwa haraka zaidi kuliko kawaida,maana hata kama shida ni minyoo Anemia ndiyo inapaswa kutibiwa haraka kwa sababu damu ikipungua sana inaweza kuleta shida.
2. Kama Kuna dalili zozote za Anemia na zinaonekana wazi, inabidi kuangalia wingi wa damu na kuona kiasi kilichomo kama kiasi Cha wingi wa damu ni zaidi ya 5g/l vyakula na dawa mbalimbali vinaweza kutumika Ili kuongeza damu na mboga mboga za majani zinaweza kutumika Ili kuongeza damu, kama kiwango Cha damu ni Chini ya 5g/l mgonjwa inabidi aongezewa damu mara Moja. Tujue kuwa damu ni muhimu kwa binadamu kwa hiyo ni muhimu kuongeza mara Moja ikiisha.
3. Baada ya kuongeza damu mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuondoa minyoo kama vile mebendazole na albendazole hizi dawa zinapaswa kutumiwa kwa maagizo ya wataalamu wa afya na sio kutumia dawa tu, na tujue mtu akiwa anatumia dawa za minyoo hapaswa kunywa pombe maana ni hatari kwa kuchanganya dawa za minyoo na pombe.
4.Baada ya kumpatia mgonjwa dawa uangalizi unapaswa kuwepo Ili kuhakikisha kuwa mgonjwa anapona kabisa na pia mgonjwa anapaswa kupima wingi wa damu Ili kuangalia kama kiwango Cha damu mwilini kipo kwenye hali ya kawaida kabla hajaruhisiwa kutoka hospitalini, na pia mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuongeza damu na kutumia vyakula vyenye wingi wa protein na vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma.
5. Elimu inabidi utolewa kwa mgonjwa na wote waliomzunguka kuhusu namna ya kujikinga na ugonjwa wa upungufu wa damu hasa kuhusu namna ya kupambana na minyoo kwenye mazingira na kuchimba choo, kunywa maji masafi,kuepuka kucheza kwenye maji yaliyotuhama hasa kwa watoto wadogo na kutumia dawa za minyoo kwa mda Ili kama Kuna Aina yoyote ya minyoo itaondoka na kiwango Cha damu kitakuwa kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 ai web app 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)
maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri
Soma Zaidi...Dalilili za tetekwanga
posti hii inazungumziaTetekuwanga . Tetekwanga(varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, kama vile upele. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya mara kwa mara
Soma Zaidi...Dalili na Ishara za mawe kwenye figo
Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako.
Soma Zaidi...Dalili za uti kwa wanaume na wanawake
tambuwa chanzo na dalili za UTI na tiba yake, pamoja na njia za kupambana na UTI
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...