image

Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.

Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake.

6.4.Kusimamisha Swala za Faradh katika nyakati za Dharura.

-   Swala imepangiwa muda maalumu, isiswaliwe nje ya muda wake ila kwa udhuru wa kisheria.

-   Hapana ‘kadha’ (kulipa swala) au kuswali swala nje ya wakati wake bila dharura kisheria.

     Rejea Qur’an (4:103), (2:286), (2:185), (5:6).

 

  1. Ameruhusiwa kutayammamu iwapo hawezi kutumia maji.

      Rejea Qur’an (4:43) na (5:6).

 

2. Kama mgonjwa hajimudu kujitwaharisha kwa maji au tayammamu na hana mtu wa kumsaidia, basi atatayammamu kwa ishara na kuswali kwa ishara (kifikra) pia.

      Rejea Qur’an (5:6).

 

3. Mgonjwa anaruhusiwa kuswali akiwa amekaa na kuelekea Qibla kama anaweza, na atarukuu na kusujudu kwa kukaa au kwa ishara jinsi atakavyoweza.

 

4. Iwapo hawezi kukaa basi ataswali akiwa amelala kwa ubavu akiwa ameelekea Qibla kama anaweza, vinginevyo ataelekea popote na kulala chali au kulala vyovyote awezavyo.

 

5. Mgonjwa anaruhusiwa kuchanganya swala na kuzifupisha kama msafiri kulingana na hali ya ugonjwa na mazingira yake.

-     Muislamu akiwa safarini anawajibika kutekeleza swala kama ifuatavyo;

      Rejea Qur’an (5:6), (4:101) na (2:238-239).

  1. Anaruhusiwa kutayammamu kama maji yatakosekana au hakuna uwezekano wa kuyatumia ndani ya kipando. Kutayammamu kunafaa kwa kutumia ukuta wa chombo cha usafiri pia.

 

2. Anaruhusiwa kupunguza swala zenye rakaa 4 na kuswali rakaa mbili mbili ambazo ni Adhuhuri, Alasir na Ishaa tu.

 

3. Pia msafiri ameruhusiwa kuunganisha swala 2, Adhuhur na Alasir, Magh’rib na Ishaa tu kwa kuziswali muda mmoja, kwa kuzitanguliza muda wa swala ya mwanzo (Jamu’ Taq’diim) au kuzichelewesha na kuziswali muda wa swala inayofuata (Jamu’ Ta’akhiir)

 

4. Pia msafiri anaruhusiwa kuswali huku akiwa anatembea au anaendelea na safari kwenye kipando chake.

 

Kusimamisha swala ya faradh katika uwanja wa vita ni kama ifuatavyo;

Rejea Qur’an (4:102-103).

 

-     Askari wagawanyike katika makundi mawili, ambayo yataswalishwa jamaa na imamu mmoja.

 

-     Swala itafupishwa kama ilivyo katika swala ya safari, kwa kuswaliwa rakaa mbili yenye rakaa 4.

 

-     Kundi moja litaanza kuswali na imamu likiwa na silaha zao na jingine likiwa katika ulinzi.

 

-     Imamu ataswali rakaa moja ya mwanzo na kundi la mwanzo, na watakaponyanyuka rakaa ya pili, kila askari atamalizia rakaa ya pili kivyake haraka na baada ya kutoa salaam atarudi kuchukua nafasi ya ulinzi.

 

-     Imamu atabakia amesimama katika rakaa ya pili mpaka kundi la pili litakapounga jamaa nyuma yake ndipo ataendelea kumalizia rakaa yake ya pili.

 

-     Imamu atakapomaliza rakaa ya pili atatoa salaam na kila askari atasimama na kivyake kumalizia rakaa ya pili haraka na kutoa salaam pia.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1418


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Wanaowajibika kuhijji
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali juu ya Nguzo za uislamu
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Riba na Madhara Yake Katika Jamii
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara. Soma Zaidi...

Nguzo za uislamu:Shahada
Nguzo za uislamu: Shahada (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

familia
Soma Zaidi...

Watu wanaolazimika kufunga mwezi wa Ramadhani
Hapa utajifunza watu ambao wanalazimika kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...

Haki ya kumiliki mali katika uislamu
Soma Zaidi...

Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini, pamoja na swala za qabliya na baadiya
Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid. Soma Zaidi...

Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...

haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu
Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Soma Zaidi...

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza
Funga za Sunnah. Soma Zaidi...

malezi ya mtoto mchanga baada ya talaka
Soma Zaidi...